donimuya
JF-Expert Member
- Mar 1, 2011
- 272
- 55
KAZI ZA MBUNGE
1) Kuwawakilisha wananchi
2) Kutunga sheria
3) Kuisimamia Serikali
MBUNGE WAKO AMEFANYA HIVYO
Mimi kwangu Morogoro mjini. Wana morogoro tujiulize je ABOOD ametuwakilisha vizuri BUNGENI na kwenye vikao vya MADIWANI kwa kuchangia kutunga sheria nzuri zitakazotetea maslahi ya wananchi wa morogoro na kuzisimamia?
Je ameisimamia serikali kuhakikisha inatekeleza wajibu wake kwa wananchi? kwa mfano amefanya nini kuhakikisha VIWANDA haviuzwi kifisadi? au na yeye amekuwa sehemu ya wizi huo?
RUSHWA NA UFISADI mahospitalini, polisi, mahakamani, TRA na kwenye ofisi mbalimbali za umma, ABOOD ametuwakilishaje katika kukemea hilo? au ametumia nafasi hii ya ubunge kukwepa kodi, kujipatia mali zetu na kuziua?
MAJI yalikuwa yakipatikana karibu siku nzima baadhi ya maeneo, sasa imekuwa ya mgawo. ametuteteaje kwa kuibana serikali kuhakikisha maji yanapatikana kama zamani na kuongeza huduma ya maji ya bomba maeneo yasiyokuwa na maji?
ABOOD amefanya nini katika kuisimamia serikali ili itupatie huduma bora? mfano huduma za AFYA je amesiimamiaje serikali kutekeleza ahadi ya wazee kutibiwa bure na madawa kupatikana bila mizengwe?
Amesimamiaje upatikanaji wa ELIMU BORA na sio bora elimu katika shule zetu za kata?
Je amefanya nini kuhakikisha serikali inatutatulia kero zetu? mfano migogoro ya ardhi (mashamba na viwanja), unyanyasaji viwandani na wafanyakazi kulipwa mishahara midogo, au na yeye amekuwa sehemu ya unyanyasaji huo?
Amesimamiaje michango ya wazazi katika shule za kata kuhakikisha inatumika kwa kazi iliyokusudiwa au anatazama tu zikiliwa na wajanja wachache?
NADHANI HAJAFANYA KAZI ZA MBUNGE ipasavyo, kazi alizofanya (mfano kutoa bus la kuzikia au kusaidia vikoba kina mama) ni kama za kina Mengi, Manji, Bakharesa nk, ambapo lengo lao huwa ni kulinda maslahi binafsi.
TUNATAKA MBUNGE, anayejuwa kazi za mbunge na azitekeleze kwa vitendo, VIJANA wenye sifa kutoka chama chochote jitokezeni kugombea nafasi hii,
WANANCHI WA MOROGORO tuonyeshe mfano kwa kuonyesha kuwa tuna uelewa na siyo jinsi mikoa mingine wanavyotuchukulia. eti mara abood au shabib au sadiki nk.
MUNGU IBARIKI MOROGORO
na naamini mikoa mingine mtatutendea haki katika uchaguzi huu kwa kutuletea wabunge wenye sifa sahihi MUNGU IBARIKI TANZANIA
1) Kuwawakilisha wananchi
2) Kutunga sheria
3) Kuisimamia Serikali
MBUNGE WAKO AMEFANYA HIVYO
Mimi kwangu Morogoro mjini. Wana morogoro tujiulize je ABOOD ametuwakilisha vizuri BUNGENI na kwenye vikao vya MADIWANI kwa kuchangia kutunga sheria nzuri zitakazotetea maslahi ya wananchi wa morogoro na kuzisimamia?
Je ameisimamia serikali kuhakikisha inatekeleza wajibu wake kwa wananchi? kwa mfano amefanya nini kuhakikisha VIWANDA haviuzwi kifisadi? au na yeye amekuwa sehemu ya wizi huo?
RUSHWA NA UFISADI mahospitalini, polisi, mahakamani, TRA na kwenye ofisi mbalimbali za umma, ABOOD ametuwakilishaje katika kukemea hilo? au ametumia nafasi hii ya ubunge kukwepa kodi, kujipatia mali zetu na kuziua?
MAJI yalikuwa yakipatikana karibu siku nzima baadhi ya maeneo, sasa imekuwa ya mgawo. ametuteteaje kwa kuibana serikali kuhakikisha maji yanapatikana kama zamani na kuongeza huduma ya maji ya bomba maeneo yasiyokuwa na maji?
ABOOD amefanya nini katika kuisimamia serikali ili itupatie huduma bora? mfano huduma za AFYA je amesiimamiaje serikali kutekeleza ahadi ya wazee kutibiwa bure na madawa kupatikana bila mizengwe?
Amesimamiaje upatikanaji wa ELIMU BORA na sio bora elimu katika shule zetu za kata?
Je amefanya nini kuhakikisha serikali inatutatulia kero zetu? mfano migogoro ya ardhi (mashamba na viwanja), unyanyasaji viwandani na wafanyakazi kulipwa mishahara midogo, au na yeye amekuwa sehemu ya unyanyasaji huo?
Amesimamiaje michango ya wazazi katika shule za kata kuhakikisha inatumika kwa kazi iliyokusudiwa au anatazama tu zikiliwa na wajanja wachache?
NADHANI HAJAFANYA KAZI ZA MBUNGE ipasavyo, kazi alizofanya (mfano kutoa bus la kuzikia au kusaidia vikoba kina mama) ni kama za kina Mengi, Manji, Bakharesa nk, ambapo lengo lao huwa ni kulinda maslahi binafsi.
TUNATAKA MBUNGE, anayejuwa kazi za mbunge na azitekeleze kwa vitendo, VIJANA wenye sifa kutoka chama chochote jitokezeni kugombea nafasi hii,
WANANCHI WA MOROGORO tuonyeshe mfano kwa kuonyesha kuwa tuna uelewa na siyo jinsi mikoa mingine wanavyotuchukulia. eti mara abood au shabib au sadiki nk.
MUNGU IBARIKI MOROGORO
na naamini mikoa mingine mtatutendea haki katika uchaguzi huu kwa kutuletea wabunge wenye sifa sahihi MUNGU IBARIKI TANZANIA