Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,755
- 218,373
Taarifa ikufikie popote ulipo kwamba , Mbunge ajaye wa Mbeya Mjini , ambaye pia ni Mfanyabiashara na Mwekezaji wa Kimataifa , Bilionea Joseph Mbilinyi , Yeye badala ya kuwaita watanzania wenzake jina la kikatili na la kijinga la WANYONGE , ameamua kuupiga vita Umasikini kwa kutafuta wawekezaji wa Uturuki , kwa ajili ya mazao ya kilimo na madini .
Taarifa zaidi zinaonyesha kwamba lengo kuu la Sugu ni kuhakikisha Wakulima wa Mbeya na Tanzania wanapata soko la Uhakika la kuuzia Matembele yao , michicha na kabichi zao , Mchele wa Kyela , Mbarali na keingineko Nchini , badala ya kupata hasara kwa bidhaa hizo na nyingine kuozea shambani .
Kwa niaba yangu na kwa niaba ya Watanzania wote nampongeza sana Sugu kwa huruma yake na utu wake kwa watanzania wenzake na kuamua kuwatafutia soko la uhakika la mazao yao , ana roho ya kitajiri sana