Watu wa Mby walimpa kura Sugu kwakuwa hawakuwa na chaguo lingine bora. Yaani mtu mwenye akili timamu hawezi kufanya alichafanya Sugu(kama hii habari ni ya kweli) kwasababu Mkoloni ni mwenyeji wa Tanga na sio Mby. Sugu kama mbunge anajukumu la kutatua matatizo ya ajira ya vijana wa Mby waliomwezesha kwa kumpigia kura na kuzilinda pale DSA, sasa ungetegemea ajira kwama hiyo ampe mwenyeji (mtu wa jimbo lake) anayeyajua matatizo na matarajio ya watu wa Mby. Siamini kama Sugu amekosa vijana wa Mby wenye sifa ya kazi hiyo na badala yake akampata Mkoloni.
Na hapa sio ishu ya ukabila au ukanda. Ni suala la mwakilishi(Mbunge) wa wananchi kujua matatizo ya wananchi na kuyapatia ufumbuzi. Kisiasa, hili ni kosa kubwa kwa Sugu, kama kuna watu makini ndani na nje ya Chadema, wanaweza wakalitumia kumwangusha(pamoja na mambo mengine) 2015. So far amepwaya ktk kujenga hoja na kuwakilisha hoja za wananchi. Chadema itawalazimu kuwa makini zaidi ktk kuchagua mgombea ubunge wa Mby mjini 2015, kwasabau wananchi wa Mby wanaweza wasisite kurudia kile walichomfanyia Polisya Mwaiseje(NCCR Mageuzi) ambaye alitumikia kw kipind kimoja tu(1995-2000).