ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,128
- 49,849
Mbunge wa Mtwara Vijijini kupitia tiketi ya CUF, Shamsia Mtamba amepata nafasi ya kutoa neno wakati msatara wa Rais Samia Suluhu Hassan uliposimama barabarani kwenye ziara ya kikazi jimboni humo, ambapo Shamsia amekiri kuridhishwa na uchapakazi wa Rais Samia huku akimuambia kuwa kwenye uchaguzi ujao wa 2025 atamuunga mkono.
Mbunge Shamsia ametaja baadhi ya changamoto zinazowakabiri wananchi wa jimbo lake ikiwemo kukosekana kwa vitambulisho wa NIDA kwa wananchi wengi na uhaba wa maji safi na salama hivyo amemuomba Rais Samia aongeze jitihada kumaliza matatizo hayo jimboni kwake.
Mbunge Shamsia ametaja baadhi ya changamoto zinazowakabiri wananchi wa jimbo lake ikiwemo kukosekana kwa vitambulisho wa NIDA kwa wananchi wengi na uhaba wa maji safi na salama hivyo amemuomba Rais Samia aongeze jitihada kumaliza matatizo hayo jimboni kwake.