Mbunge Nape Nnauye amwita Raila Odinga kibaraka

Mbunge Nape Nnauye amwita Raila Odinga kibaraka

Sasa hapo nape kamtabiria vp uhuru kenyata ushindi wa urais kenya wakati tayari odinga kajitoa ktk uchaguzi huo?!
kilaza wahedi
Huyu jamaa tangu wamtumbue akili yake imeparararizi
 
"Nape Nnauye amefunguka na kumtabiria ushindi mgombea wa urais wa Kenya Uhuru Kenyatta"

Kweli anatabiri - sijui inataka utabiri ikiwa mgobea uraisi ni mmoja tu. Haya tutaona kama utabiri utakua kweli.
Ingekuwa vyema wanasiasa wa TZ kutoingilia au kuonesha kuunga mkono upande mmoja wa siasa nchini Kenya. Tuwaombee wakenya wapite salama kwenye hii changamoto kubwa ya kisiasa
 
Nape anamshika sharubu Baba J
Kifupi vijana akiwemo Nape wamemwabgusha magufuli simshangau teuzi sake nyingi kuweka watu wazima.many youth don't know how to behave.Kumwondoa uwaziri Nape magufuli alikuwa sahihi .Nape is still a playboy hakutakiwa kupewa ofisi kubwa kama ya uwaziri premature
 
Huyu jama akipokonywa na ubunge anaweza akaanza kuokota makopo barabarani.
 
Neno Uhuru Kenyatta kushinda Uraisi Kenya tena linamyima usingizi hata Raisi Magufuli kwahiyo hilo alilolisema Nape ni Dongo kwa CCM kumbuka Lowassa alikua Kenya anamkapenia nani! Hahahaaaa
 
Ni uendawazimu kufananisha uchaguz wa znz na wa Kenya.ikiwa Kenya ulifutwa uchaguz kisheria kupitia supreme Court na kutangazwa uchaguz mwingine ndani ya siku 60. Wakati wa znz ulifutwa na MTU anaitwa jecha chairman wa tume.akifuta uchaguz huo hapakuwapo na mpaka sasa hakuna sheria yyte inayompa mamlaka ya kufuta uchaguz.so ni cheap politics watu wa ccm mnataka kuleta humu jamvin.ambazo hazina nafasi katika karne hii ya utandawaz.
 
Neno Uhuru Kenyatta kushinda Uraisi Kenya tena linamyima usingizi hata Raisi Magufuli kwahiyo hilo alilolisema Nape ni Dongo kwa CCM kumbuka Lowassa alikua Kenya anamkapenia nani! Hahahaaaa
Mambo Ya Kenya waachieni wakenya kipindi hiki Nape kama mbunge wa CCM hakutakiwa kutoa tamko kama hilo.Yeye ni mbunge wa mtama tu sio msemaji wa CCM wa mambo ya nchi za nje.CCM Ina idara Ya mambo ya nje Nape asiwaingile kakiuka maadili Na protocol za chama.CCM mchukulieni hatua
 
Nafafananisha uchaguz wa marudio wa kenya na zanzibar

Wamefanana kila kitu.Seif alijitoa Shein akapita

nae odinga kajitoa Uhuru atapeta

Hapa ndo hua naamini kwanini CCM kinaitwa chama cha ukombozi Afrika,hivi vyote huiga ccm


Nafafananisha uchaguz wa marudio wa kenya na zanzibar

Wamefanana kila kitu.Seif alijitoa Shein akapita

nae odinga kajitoa Uhuru atapeta

Hapa ndo hua naamini kwanini CCM kinaitwa chama cha ukombozi Afrika,hivi vyote huiga ccm
ae373bba994f0e3a64c26dd93d736038.jpg

Hapa walikuwa wanamuiga Magufuli au CCM , au umejikuta mdomo na mkono vimepitwa?
 
Nappe Mzee wa bao la mkono au amesahau kuwa hata huo ubunge wake ni wa dhuluma dhidi ya Chadema.
ccm mnaanza kufunguka IPO Sikh mtafunguka juu ya uraisi wa "dinosaur wa Dodoma"
 
Nafafananisha uchaguz wa marudio wa kenya na zanzibar

Wamefanana kila kitu.Seif alijitoa Shein akapita

nae odinga kajitoa Uhuru atapeta

Hapa ndo hua naamini kwanini CCM kinaitwa chama cha ukombozi Afrika,hivi vyote huiga ccm
Siasa za kiafrika za hovyo kabisa.
Utajiondoaje kwenue kinyang'anyiro dakika za majeruhi?
Washabiki zake wamueleweje! Wagome kupiga kura, ili hata kwa uchache hasimu wake ahesabiwe ushindi? Inaudhi sana kwa kweli.
 
ae373bba994f0e3a64c26dd93d736038.jpg

Hapa walikuwa wanamuiga Magufuli au CCM , au umejikuta mdomo na mkono vimepitwa?
Kipindi hicho chadema pia walikuwa wakimuunga mkono odinga Na walipeleka hadi magari Na kumfanyia odinga kampeni pamoja Na kujua magufuli alikuwa naye hilo unalisemeaje?
 
mkubwa kama nape huwezi andika maneno kama hayo kama unajielewa upepo wa magu umemharibu
 
ge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amefunguka na kumtabiria ushindi mgombea wa urais wa Kenya Uhuru Kenyatta na kusema kuwa atashinda uchaguzi huo ambao utafanyika Alhamisi Oktoba 26, 2017 na kusema Uhuru ndiye anayestahili kuongoza nchi hiyo.

Nape Nnauye amedai kuwa Uhuru Kenyatta anastahili kuwa Rais wa Kenya kwa sababu yeye ni mwana demokrasia wa kweli hivyo anaamini raia wa Kenya watampa kura nyingi za kutosha na kumpuuza mpinzani wake Raila Odinga.

"Unastahili kuwa Rais wa Kenya Mwana demokrasia wa kweli. Naamini ndugu zangu wa Kenya watakuchagua kwa kishindo kesho na kumpuuza kibaraka".

Ameandika Nape Nnauye kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Nchi ya Kenya kesho inategemewa kufanya uchaguzi wa marudio wa nafasi ya urais kufuatia mahakama ya juu nchini humo kufuta matokeo ya urais.

Nape Nape Nape... hapana hapana hapana... wakati mwingine ni busara kuweka akiba ya maneno. Mshindani wa Uhuru Kenyata inajulikana ni Raila Odinga. Nape ni mtoto mdogo mno kuanza kumkashifu Raila Odinga.
 
Halafu mnajiita mashabiki wa Chadema hamjui kuwa hata mgombea wenu wa ubunge ambae alistahili ushindi alifungwa miezi sita jela kutokana na figisu za Nappe.

Kweli nyie ni zaidi ya Nyumbu.
Nasema hivyo kwasababu nape 2020 ni mbunge na waziri kupitia Chadema.Dude go BACK to school


Swissme
 
fb2d2ea8c737a6be38057bf2642586e6.jpg
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amefunguka na kumtabiria ushindi mgombea wa urais wa Kenya Uhuru Kenyatta na kusema kuwa atashinda uchaguzi huo ambao utafanyika Alhamisi Oktoba 26, 2017 na kusema Uhuru ndiye anayestahili kuongoza nchi hiyo.

Nape Nnauye amedai kuwa Uhuru Kenyatta anastahili kuwa Rais wa Kenya kwa sababu yeye ni mwana demokrasia wa kweli hivyo anaamini raia wa Kenya watampa kura nyingi za kutosha na kumpuuza mpinzani wake Raila Odinga.

"Unastahili kuwa Rais wa Kenya Mwana demokrasia wa kweli. Naamini ndugu zangu wa Kenya watakuchagua kwa kishindo kesho na kumpuuza kibaraka".

Ameandika Nape Nnauye kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Nchi ya Kenya kesho inategemewa kufanya uchaguzi wa marudio wa nafasi ya urais kufuatia mahakama ya juu nchini humo kufuta matokeo ya urais.



Nape anazungumzia Demokrasia ipi? Demokrasia Demokrasia au Demokrasia ya kiafrika????????
 
Halafu mnajiita mashabiki wa Chadema hamjui kuwa hata mgombea wenu wa ubunge ambae alistahili ushindi alifungwa miezi sita jela kutokana na figisu za Nappe.

Kweli nyie ni zaidi ya Nyumbu.
Wameanza kuwa na mahaba na Nape,kuliko Suleiman Mathew!!
 
Back
Top Bottom