Mbunge Nape Nnauye amwita Raila Odinga kibaraka

Mbunge Nape Nnauye amwita Raila Odinga kibaraka

Wewe unamuandikia nape kwani we we pekee huwezi kujiongoza?ni aibu sana Ku coly na Ku paste alichoandika MTU,tumia akili yako na sii kusubiri wenzio wakusaidie
QI yako iko below zero ndio maana hukuweza kung'amua kuwa thread hii zipo hapa JF kila siku.

Inamaana kesho kwenye magazeti kukiwa na habari hii watakuwa wamemuandikia Nape?
 
Sasa hapo nape kamtabiria vp uhuru kenyata ushindi wa urais kenya wakati tayari odinga kajitoa ktk uchaguzi huo?!
kilaza wahedi
Inaonekana wachangiaji wengi hawajui kinachoendelea kenya, na hawajui kuwa uhuru anagombea mwenyewe na mgombea ambaye hana juna kma Ethuro.
 
Wale wapenzi wa magoli ya mkono ni lazima watamuunga mkono Kenyata. Nape usijitoe ufahamu, Kenyata aliiba kura August 8, hilo halina ubishi hata Supreme court iliamua hivyo, sasa unachomsifia Kenyata ni nini? CCM nao ni wezi wa kura ndiyo maana lazima wamsifie mwizi mwenzao.


CHADEMA ndio walioweka bayana kumuunga mkono Uhuru kwa madai kuwa katika uchaguzi uliopita hapa nchini Odinga aliwasaliti na kumuunga mkono Magufuli.
 
Nappe Mzee wa bao la mkono au amesahau kuwa hata huo ubunge wake ni wa dhuluma dhidi ya Chadema.
Nyani haonagi kundu lake linalotia kinyaa. Huyo mbwatukaji wa zamani angekuwa anajitambua kuwa ndio mojawapo ya vinara wa kuchakachua Katiba ya Warioba, asingekuwa na guts za kujishebedua kwa watu. Alipaswa kutulia tu na kukumbuka madudu aliyoyafanya huko nyuma kwani anaowatumikia kwa sasa, nao watamtumia na kumtema kama toilet paper. He's no longer an asset rather a liability.
 
Siasa za kiafrika za hovyo kabisa.
Utajiondoaje kwenue kinyang'anyiro dakika za majeruhi?
Washabiki zake wamueleweje! Wagome kupiga kura, ili hata kwa uchache hasimu wake ahesabiwe ushindi? Inaudhi sana kwa kweli.

naona mkuu umenielewa,asante
 
CHADEMA watakisapoti kitakachotokea kesho Kenya , lkn wanakikataa kilichotokea zanzibar (ukandamizaji wa demokrasia uliofanywa na CCM ) , ila si shangai sifa ya mwanasiasa lazima uwe MNAFIKI.Nape si mshangai kwani chama, kishazoea kukandamiza demokrasia, kwa hiyo kwake anaona sawa.
 
Ni kweli? Kwa nini chadema haikufungua kesi?
KWANI HUJUI SHERIA YA NCHI HII KUWA TUME IKISHATANGAZA MSHINDI HAKUNA KESI YA KUPINGA? INA MAANA HATA KAMA USHINDI HUO UMETOJANA NA WIZI WA KURA BASI. KAA UKIJUA HILI
 
Anazidi kumkera mwenyekiti wake kwa kumtukana swaiba wake...!
 
Nape anaweweseka, bado anaulilia uwaziri, hautarudi ng'o! Nape arudi Mtama awasaidie wananchi wake wapate maji, ya Raila amwachie mwenyewe, Nape is no match to RAO!
 
fb2d2ea8c737a6be38057bf2642586e6.jpg
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amefunguka na kumtabiria ushindi mgombea wa urais wa Kenya Uhuru Kenyatta na kusema kuwa atashinda uchaguzi huo ambao utafanyika Alhamisi Oktoba 26, 2017 na kusema Uhuru ndiye anayestahili kuongoza nchi hiyo.

Nape Nnauye amedai kuwa Uhuru Kenyatta anastahili kuwa Rais wa Kenya kwa sababu yeye ni mwana demokrasia wa kweli hivyo anaamini raia wa Kenya watampa kura nyingi za kutosha na kumpuuza mpinzani wake Raila Odinga.

"Unastahili kuwa Rais wa Kenya Mwana demokrasia wa kweli. Naamini ndugu zangu wa Kenya watakuchagua kwa kishindo kesho na kumpuuza kibaraka".

Ameandika Nape Nnauye kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Nchi ya Kenya kesho inategemewa kufanya uchaguzi wa marudio wa nafasi ya urais kufuatia mahakama ya juu nchini humo kufuta matokeo ya urais.

Hivi kuna utabiri hapo tena jamani. Raila keshajitoa principally amebakia mgombea mmoja ambaye kwenye uchaguzi wa awali alipata majority votes... sasa unatabiri atashinda wakati yupo mwenyewe. Results of the elections are known watu wanaenda tu kupiga kura kutimiza matakwa ya kisheria
 
Back
Top Bottom