Mafwi Munda
JF-Expert Member
- Nov 30, 2017
- 1,750
- 1,599
Wanaombewa wasife.Kwahiyo hao wagonjwa waliopo muhimbili wanafanya nini?
Tena alimdhurumu dada yangu kabisa huyu pedeshee angekufa tuHili liwe fundisho kwa wanaccm wanaoshinda kwa kuiba kura , huyu ni miongoni mwa wanaccm walioingia bungeni kwa wizi wa kura .
Unajuaje labda walikuwa na wageni wengi huko kwao?!Sumaye alilazwa akapona pale, mama Janet magufuli, heche,mama mtanzania na wengine wengi.
Endelea kusikitika.Unajuaje labda walikuwa na wageni wengi huko kwao?!
Kama hao walikuwa wanaumwa kweli nasikitika kwanini shilawadu hawakusema mapema wangepelekwa india kutibiwa.
We utakuwa mwana ifakara bila shaka. Huyo alikuwa anagawa pesa kwa watu hovyo hovyoHuyu si alikuwa pedeshee anakuja Kilombero na hammer leo anaomba msaada kweli
Kuna anayeweza kuzuia kufa?Wanaombewa wasife.
HahahahaTena alimdhurumu dada yangu kabisa huyu pedeshee angekufa tu
Bima za matibabu za wabunge ni miaka mitanoMutu imepingwa risasi inaombwa saidia rais anakatala, lakini huyu papa maarufu ya kutuza watu kushoo za live bendi anahudumiwa na kodi za maraiaa, ina maanisha mbunge mustafu hana kubima ya afya, au bima yake iko na sawa na hizi zetu za wakulima
Kabla ya JPM mtandao wao ulikuwa mkubwa, hata uende wapi hupati sheria, haina tofauti kama ya yule mama aliyepoteza title 2 kwa mmiliki wa "Galaxy", huyu kina Katunzi, Papa Msofe, Ndama, Masawe, marehemu Khamis faraji n.k. ilikuwa nchi yao, kweli aliye juu msubiri chini, wameliza magari na majumba ya watu kinoma noma, makatili sana hawa..Tena alimdhurumu dada yangu kabisa huyu pedeshee angekufa tu
Tanzania ina mafukara wengi,wenye hari mbaya kuliko hata huyo mheshimiwa,Leo kwenye pitapita zangu mtandaoni nimekutana na video ya mbunge mstaafu wa Kilombero mh Abdul Mtegeta akimuomba Mh president msaada wa matibabu, imekuwa jambo la kawaida sasa au fashion watu maarufu wenye vipato kulialia mtandaoni wakiomba msaada.
Hivi najiuliza kipindi wakiwa kwenye form walishindwa fanya serving au kuwekeza kijiutega uchumi hata banda la kuuza samaki?
Basi hata bima ya afya imewashinda kukataa 1.2m sijui per year hata mimi nisiye na ajira maalumu na mudu?
=====
MBUNGE mstaafu wa Kilombero (CCM), Abdul Mteketa, ambaye aliomba msaada wa matibabu ya upasuaji wa magoti kwa Rais John Magufuli kupitia mitandoa ya kijamii, amesafirishwa kwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kutibiwa.
Jumamosi iliyopita, Mteketa alirekodi ujumbe wa video na kuuweka kwenye mitandao ya kijamii akimwomba Rais Magufuli amsaidie matibabu kwani hali yake kiuchumi ni mbaya.
Mteketa aliyetumikia jimbo la Kilombero kwa miaka mitano baada ya kushinda katika Uchaguzi Mkuu wa 2010, alishindwa kwenye mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM kwa ajili ya kutetea kiti hicho 2015.
Katika ujumbe wa video alioutuma Jumamosi, Mbunge huyo mstaafu alimweleza Rais Magufuli kuwa hali yake ya kiafya ni mbaya na kwamba amekuwa akibebwa kwenda maliwatoni na kuogeshwa.
"Mheshimiwa Rais John Magufuli, mimi ni Abdul Mteketa, Mbunge mstaafu wa Kilombero nipo hapa mbele yako kwa sababu nimejitahidi miaka yote kukufikia lakini nimeshindwa tangu uingie madarakani," alisema na kueleza zaidi:
"Hali yangu kiafya ni mbaya kama unavyoniona, nabebwa kwenda chooni, naogeshwa, kila kitu nategemea msaada wa mtu. Nimejitibu kwa mwaka mzima sasa lakini bila mafanikio.
"Nimeenda kwa madaktari wameniambia tatizo ni magoti, kwanza nimeumwa mguu huu madonda kila sehemu yamepona, magoti yangu yanatakiwa kufanyiwa upasuaji."
Siku iliyofuata, Mteketa aliweka tena ujumbe mwingine wakati akiwa kwenye gari la kubeba wagonjwa baada ya Rais Magufuli kumsaidia ambamo anamshukuru kiongozi huyo wa taifa.
Mteketa anasema katika ujumbe huo kuwa baada ya Rais Magufuli kuona ujumbe wake wa video aliyoituma kwenye mitandao ya kijamii Jumamosi, alichukua hatua ya kumsaidia.
"Jana (Jumamosi) nilituma ujumbe wa video ya hali yangu kuwa mbaya, niliyompelekea Rais, alipoiona leo (Jumapili) amechukua hatua; amenitumia gari la wagonjwa ambalo sasa hivi nipo ndani napelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili," anasema.
"Nakushukuru sana Rais, Chama cha Mapinduzi CCM na Watanzania waliopeleka ujumbe wa video yangu mpaka zimemfikia Rais. Naomba mniombee."
je kwa watanzania wasiojulikana wapatapo maradhi yanayohitaji fedha nyingi kutibibiwa si ndiyo wanajifia bila kusaidiwa?Yanii nimeshangazwa mpaka nikashindwa kushangaa hivi kweli Kama mbunge mstaafu analialia Bibi yangu kule marangu afanyaje Sasa?
mbona viongozi wengi hulia tu hawana fedha ili hali walikuwa na mafao makubwa tu.Kuna mkuu mmoja wa wilaya ya kinondoni naye aliwahi kulia asaidiwe matibabu.Ni ajabu viongozi kama hawa kulialia wasaidiwe matibabu wakati inajulikana walikuwa watumishi Wa super scale salaryBibi yangu amestafu uwalimu mwaka 1990 ila mpaka leo pesa ya kula matibabu hategemei mtu ukitaka kumpa Ni kwa hisani yako yupo fit balaa..Sasa huyu kastafu mafao zaidi ya 300m juzi tu hapo analialia huu Ni upuzi wa kiwango Cha Masters
ni kujiabisha.Watu wasio na kipato ndiyo sahihi kuomba msaadaMiaka hii watu kutumia mitandao.. unashangaaaa