Nshomile wa Muleba
JF-Expert Member
- Dec 5, 2015
- 2,165
- 5,551
Jambo Jambo?
Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalotawaliwa na wabunge wa CCM, huwa linanishangaza kiasi kwenye uchagiaji wa upitishajishwaji wa bajeti za wizara kadha wa kadha za mwaka husika.
Mbunge anaweza akasimama na kuikosoa serikali vilivyo akatoa “point” za maana mpaka watazamaji/Wananchi mnasema “Yes” huyu mbunge anajua nini maana ya kuwawakikisha wananchi wake,Anaweza mpaka akawa anaongea kwa kufoka sana bungeni kuonyesha kuwa amekereka sana na uamuzi/mwenendo wa serikali kwenye hoja husika ila sasa cha kushangaza mwishoni utasikia;
“MHE. SPIKA NIMECHUKIZWA NA KITU A OR B LAKINI NAUUNGA MKONO HOJA”
Sasa huwa najiuliza, Kama mtu hukubaliani na bajeti iliyopendekezwa na wewe ukasimama kidete kwa kufoka na kukaripia serikali mwishooo kabisa unaunga mkono hoja tena kwa sauti laiiini na ya upole.
Kulikuwa na haja gani ya kuongea kwa sifa au kujifanya unatetea uchungu wa wananchi na walala hoi. Si bora utulie uongee kwa upole tu maana tunajua mwishoni utauunga mkono hoja
Ina maana huwa wanaambizana kwenye mikutano yao ya ndani ya chama kuwa leo wote muunge mkono hoja au?
Mtu anaweza akasimama na kusema TV sijui Gari ikija huku bara kwanini inalipa kodi wakati nchi zimeungana lakini unaweza ukashangaa mtu huyohuyo mwishoni “NAUUNGA MKONO HOJA”
Toka Bunge limeanza niambiani nani mara ya mwisho alisikia mbunge anasema hauungi mkono hoja ya bajeti ya wizara husika, niingie youtube sasa hivi niicheki
(Kama nitakuwa nimekosea mahala, niko tayari kurekebishwa)
Inshomile
Kagera, Tanzania
Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalotawaliwa na wabunge wa CCM, huwa linanishangaza kiasi kwenye uchagiaji wa upitishajishwaji wa bajeti za wizara kadha wa kadha za mwaka husika.
Mbunge anaweza akasimama na kuikosoa serikali vilivyo akatoa “point” za maana mpaka watazamaji/Wananchi mnasema “Yes” huyu mbunge anajua nini maana ya kuwawakikisha wananchi wake,Anaweza mpaka akawa anaongea kwa kufoka sana bungeni kuonyesha kuwa amekereka sana na uamuzi/mwenendo wa serikali kwenye hoja husika ila sasa cha kushangaza mwishoni utasikia;
“MHE. SPIKA NIMECHUKIZWA NA KITU A OR B LAKINI NAUUNGA MKONO HOJA”
Sasa huwa najiuliza, Kama mtu hukubaliani na bajeti iliyopendekezwa na wewe ukasimama kidete kwa kufoka na kukaripia serikali mwishooo kabisa unaunga mkono hoja tena kwa sauti laiiini na ya upole.
Kulikuwa na haja gani ya kuongea kwa sifa au kujifanya unatetea uchungu wa wananchi na walala hoi. Si bora utulie uongee kwa upole tu maana tunajua mwishoni utauunga mkono hoja
Ina maana huwa wanaambizana kwenye mikutano yao ya ndani ya chama kuwa leo wote muunge mkono hoja au?
Mtu anaweza akasimama na kusema TV sijui Gari ikija huku bara kwanini inalipa kodi wakati nchi zimeungana lakini unaweza ukashangaa mtu huyohuyo mwishoni “NAUUNGA MKONO HOJA”
Toka Bunge limeanza niambiani nani mara ya mwisho alisikia mbunge anasema hauungi mkono hoja ya bajeti ya wizara husika, niingie youtube sasa hivi niicheki
(Kama nitakuwa nimekosea mahala, niko tayari kurekebishwa)
Inshomile
Kagera, Tanzania