Kinyungu
JF-Expert Member
- Apr 6, 2008
- 17,365
- 33,004
MBUNGE wa Lindi Mjini, Salum Barwani (CUF) amesema anatekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010/15 kwa kuwa chama chake hakikushinda uchaguzi mkuu wa urais.
Barwani alisema hayo jana alipozungumza na gazeti hili ofisi kwake baada ya kuwasili jimboni kutoka kwenye Mkutano wa Bunge mjini Dodoma. Aliwataka wananchi wa jimbo lake kutambua kuwa maendeleo hayaji kwa miujiza, wala juhudi zake peke yake, ila yatakuja baada ya kuwa na mshikamano wa pamoja kati ya Serikali ya CCM, wananchi na yeye.
Ndugu zangu maendeleo ya Lindi hayawezi kupatikana kwa juhudi za mbunge peke yake, bali umoja na mshikamano ndiyo njia pekee ya kuleta maendeleo, mimi peke yangu siwezi kuleta maendeleo kama mnafikiria hivyo basi ni ndoto ya mchana, alisema.
Mbunge huyo pia alikiri kuwekwa kiti moto na baadhi ya wananchi aliokutana nao wakimtuhumu kukaa muda mrefu Dar es Salaam bila kwenda kuwaona.
Mbunge huyo alisema Baraza la Utendaji la Wilaya la CUF lilimwita na kumweka kikao Jumamosi na kumhoji sababu za kutumia muda mwingi Dar es Salaam na kutokwenda kuona wananchi baada ya Bunge la Bajeti.
Soma yote hapa: HabariLeo | Mbunge CUF aibeba CCM
Barwani alisema hayo jana alipozungumza na gazeti hili ofisi kwake baada ya kuwasili jimboni kutoka kwenye Mkutano wa Bunge mjini Dodoma. Aliwataka wananchi wa jimbo lake kutambua kuwa maendeleo hayaji kwa miujiza, wala juhudi zake peke yake, ila yatakuja baada ya kuwa na mshikamano wa pamoja kati ya Serikali ya CCM, wananchi na yeye.
Ndugu zangu maendeleo ya Lindi hayawezi kupatikana kwa juhudi za mbunge peke yake, bali umoja na mshikamano ndiyo njia pekee ya kuleta maendeleo, mimi peke yangu siwezi kuleta maendeleo kama mnafikiria hivyo basi ni ndoto ya mchana, alisema.
Mbunge huyo pia alikiri kuwekwa kiti moto na baadhi ya wananchi aliokutana nao wakimtuhumu kukaa muda mrefu Dar es Salaam bila kwenda kuwaona.
Mbunge huyo alisema Baraza la Utendaji la Wilaya la CUF lilimwita na kumweka kikao Jumamosi na kumhoji sababu za kutumia muda mwingi Dar es Salaam na kutokwenda kuona wananchi baada ya Bunge la Bajeti.
Soma yote hapa: HabariLeo | Mbunge CUF aibeba CCM