Mbunge Cosato Chumi: Serikali ione namna ya Kupunguza VAT, itawezesha Wananchi wengi kulipa Kodi na kwa hiyari

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,900
944

F-euUR4XIAAjGhK.jpg

Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini na Waziri Cosato Chumi ameshauri serikali kuona namna ya kuangalia ili iweze Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kupungua kidogo ili kuwawezesha watu wengi zaidi kulipa na kulipa kwa hiyari.

Mhe. Cosato Chumi ametoa ushauri huo leo Alhamisi Novemba 09, 2023 bungeni jijini Dodoma akichangia Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa pamoja na Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti kwa mwaka 2024/2025.

"Sisi pale Mafinga tuna shule ya msingi inaitwa Mwongozo ilikuwa na wanafunzi takribani 1,800, serikali ya awamu sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia imetupatia fedha za kutuwezesha kujenga shule nyingine pembeni yake inaitwa Muungano na imesaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi uliokuwepo hapo awali, kupitia hili nampongeza sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan" - Mhe. Cosato Chumi, Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini.

"Katika ukanda wa bahari kuna kitu kinaitwa Blue Carbon, inasiadia udhibiti katika hali ya hewa. Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kila mwaka anahudhuria mkutano wa mazingira, kama mkuu wa nchi tayari ameshatoa support katika hili la hewa ya ukaa. Kuna fedha nyingi katika biashara ya hewa ya ukaa" - Mhe. Cosato Chumi, Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini.

"Nawapongeza JKT Queens ambao wanatuwakilisha kwenye klabu bingwa ya Afrika, wanahitaji alama moja tu waingie nusu fainali, tuwaunge mkono, na tusiishie kuziunga mkono Simba na Yanga. Kitu kizuri wachezaji wa JKT Queens ni wazawa kwa 100%" - Mhe. Cosato Chumi, Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini.
 
Kwa upande wangu nashauri iwe 10%. Maana 18% haijakaa sawa hata kidogo.

Haiwezekani mfanyabiashara uhangaike kulipa marejesho ya benki peke yako, uhangaike juani na kwenye mvua kuuza bidhaa zako! Halafu serikali ichukur kirahisi tu 18% ya mapato yako, huku ikiwa haijakusaidia chochote.
 
Kwa upande wangu nashauri iwe 10%. Maana 18% haijakaa sawa hata kidogo.

Haiwezekani mfanyabiashara uhangaike kulipa marejesho ya benki peke yako, uhangaike juani na kwenye mvua kuuza bidhaa zako! Halafu serikali ichukur kirahisi tu 18% ya mapato yako, huku ikiwa haijakusaidia chochote.
Hii kitu kila siku watu huilalamikia kuhusu kodi kubwa lakin wapi
 
Back
Top Bottom