Mbunge Cherehani: Kwanini wagonjwa wanalipa fedha kumuona daktari kwenye hospitali za umma

Mbunge Cherehani: Kwanini wagonjwa wanalipa fedha kumuona daktari kwenye hospitali za umma

Bawabu wa pili

Senior Member
Joined
Nov 14, 2025
Posts
147
Reaction score
432
Mbunge wa Jimbo la Ushetu Kahama, Emmanuel Cherehani amehoji utaratibu wa mgonjwa kulipia fedha ya kwenda kumuona daktari katika hospitali za Umma hapa nchini ambapo amedai wagonjwa hulipishwa kiasi cha shilingi 5,000 mpaka 30,000.

Soma pia: Dkt. Seif Shekalaghe: Marufuku hospitali kudai fedha kwa wagonjwa wa dharura kabla ya huduma

Cherehani ameuliza swali hilo hii leo Januari 29, 2026 wakati wa kipindi cha maswali na majibu kwa Waziri Mkuu ambapo ameitaka serikali itoe kauli juu ya tozo hiyo ambayo imekuwa ikiwafanya wagonjwa kuteseka ilihali ya miundombinu kuboresha na madaktari kulipwa stahiki zao kutoka serikalini.

“Mheshmiwa Waziri Mkuu kumekuwa na malalamiko makubwa sana hapa nchini kwa Wananchi wetu wanaoenda kupata matibabu hospitali na zahanati zetu hata wakati mwingine kwenye Hospitali zetu zile za Rufaa wakifika wanaambiwa kutoa fedha za kumuona daktari maeneo mengine wanatozwa 5,000 mpaka 30,000 ilhali madaktari hawa ni waajiriwa wa Serikali wanalipwa na Serikali”

Akijibu swali hili Waziri Mkuu amesema “Mheshimiwa Spika kwa mujibu wa sheria ya bima ya afya kwa wote, utaratibu tulio jiwekea kama taifa kwenye maswala ya afya ni kuchangiana kwenye vitita mbalimbali ambavyo vinatolewa kama ambayo imeainishwa katika bima mbalimbali. Kwa wale ambao wanakuwa nje ya utaratibu wa bima ya Afya kwa wote ndio ambao wanakutana na changamoto ya kuchangia pale wanapofika katika hospitali zetu”

Hata hivyo Waziri Mkuu ameiagiza Wizara ya Afya kuharakisha kutungwa kwa sheria ambayo itaweka viwango hivyo wanavyotozwa wagonjwa viwe sawa kwa nchi nzima badala ya kila eneo kuwa na utaratibu wake.
 
Hatuna PM ndio kajibu nini sasa? Mwigulu tuombe sana Mungu asije kuwa Rais wa Nchi...hanaga huruma kabisa na mwananchi. Anajaribu kujifanya kibri na sio mwenye kujali...

Mama kakosea sana kumpa U-PM huyu bwana mdogo..
 
Swali muhimu kwa Watanzania
Lina jibiwa kipuuzi
Mnategemea hawa wanauchungu na wananchi kweli?
Kilicho ulizwa na kilicho jibiwa ni vitu tofauti
Tunaongozwa na watu wenye uwezo mdogo sana
 
Yaani nimekula msuli wa PCB nikahenya miaka mitano + internship napambana nakuwa specialist halafu mpumbavu mmoja asiyejua umuhimu wa daktari anafanya decision jinsi nitakavyolipwa??

I swear nikimkuta mbunge Jamii ya cherehani casuality, castration ndio mpango mzima ili asizae wapumbavu wenye mawazo kama yake.
 
Yaani nimekula msuli wa PCB nikahenya miaka mitano + internship napambana nakuwa specialist halafu mpumbavu mmoja asiyejua umuhimu wa daktari anafanya decision jinsi nitakavyolipwa??

I swear nikimkuta mbunge Jamii ya cherehani casuality, castration ndio mpango mzima ili asizae wapumbavu wenye mawazo kama yake.
Usifanye hivyo utawaumiza wengi! Tuelimishe basi hapa juu ya malipo ya kumwona Dr Huwa mnalipwaje? Inawekwa kwenye mshahara au mnalipwa tofauti na mshahara? Anachohoji mbunge ni kwanini ninyi mnakuwa na double payment ilihali watumishi wengine hawapewi hizo prevelegde? Au madaktari na polisi ndio watumishi wateule wa nchi hii? Hizo posho zienee kwa watumishi wote wa serikali ili kuondoa double standard basi.
 
Yaani nimekula msuli wa PCB nikahenya miaka mitano + internship napambana nakuwa specialist halafu mpumbavu mmoja asiyejua umuhimu wa daktari anafanya decision jinsi nitakavyolipwa??

I swear nikimkuta mbunge Jamii ya cherehani casuality, castration ndio mpango mzima ili asizae wapumbavu wenye mawazo kama yake.

Hoja yake ni kwenye Hospitali za Umma. Kwanini kumuona Daktar unalipa kuanzia 5k hadi 30k?.

Wakat Serikali inamlipa Daktar.

Sera ya taifa ya Afya inasema Kwa Hospital za Umma, mwananchi anapaswa kuchangia gharama kidogo ya matibabu kwenye kila stage .
(Kuandikisha kumuona daktar, vipimo, iwe vidogo au vikubwa kama xray , mri nk. Na matibabu. Iwe dawa au upasuaji).

Ila hivi viwango vimetofautiana.
Ipo haja ya kuweka vikawa fixed.
Hasa kwenye dispensary na kwenye hosp kubwa na za Rufaa.

Nakumbuka sera inasema wajawazito, Watoto under 5 yrs of age na wazee over 65 yrs hawa ni bure kumuona dokta. Ila gharama kidogo utaingia kwenye vipimo na madawa.

Je hili linafanyika?.

Bima ya afya kwa wote ni mapema kuihukumu. Last week nimezisoma package zake. Zinaanzia 192k kwa mwaka kwa kaya moja ya watu 6.
Mmmh hii itakuwa ya Hovyo tu.
 
Yaani nimekula msuli wa PCB nikahenya miaka mitano + internship napambana nakuwa specialist halafu mpumbavu mmoja asiyejua umuhimu wa daktari anafanya decision jinsi nitakavyolipwa??

I swear nikimkuta mbunge Jamii ya cherehani casuality, castration ndio mpango mzima ili asizae wapumbavu wenye mawazo kama yake.
Mkuu usitumia hasira kufanya maamuzi. Castration!! Dah.
 
Back
Top Bottom