Mbunge aliyedai waongezewe mshahara atakiwa aachie jimbo, CCM nao watoa kauli

 

Attachments

Sasa kwann chongolo anamtolea maneno ya kibabe kiasi hiki. Hajui nyuma ya kauli hii Kuna robo tatu ya wabunge wa chama chake?
Kwamfumo wa CCM watamfanya nini? Kumbuka ndiye mwenyekiti wa kikao cha Halamashauri Kuu ya CCM ambao wanapanga nani aishi na nani heeee!!!!... Samahani jamani nilikuwa nameza K Vant.
 
 

Attachments

Kwa namna nilivyomsikiliza siku moja anahojiwa alitaja sababu kadhaa kwamba;

1. Wakati anaomba lidhaa ya kuwa mbunge alitumia kama 72m na kunawengine walitumia zaidi ya 600m kuingia bungeni.

2. Kuna asilimia kubwa ya wabunge hawakai majimboni mwao sababu wanaongoza watu wengi na wengi wanashida mbalimbali na kunawalio na akili na wasio na akili. Akatoa mfano kwamba kazi za mbunge hauwezi kufananisha na mwalimu au daktari.

3. Hoteli anayokaa dodoma niyahadhi kubwa hivyo akipata mshahara wa 3.8 haiwezi kumudu gharama anazo zitumia na akabaki na chochote.

4. Akiwa nyumbani kwake anadai akiamka asubuhi watu wengi wanakuja kwake na shida mbalimbali akienda mahospitali inamlazimu atembee na chochote mwisho wa siku anajikuta anaingia mpaka kwenye biashara zake kwaajili ya kusaidia watu.

5. Mshahara wake bado hajawalipa wasaidizi wake, katibu na dereva nk.


Sasa mkuu Sexless unaona kunahoja gani kuntu hapo isiyoweza kujibika kwa akili ya kawaida ...?
 
 

Attachments

Kwanini uhonge hela ili upate ridhaa ya kutumikia wananchi?
Hafu bungeni sio sehemu ya biashara na inabidi marupirupu yapunguzwe wawe wanalipwa ka walimu ndo tutapata wazalendo.
 
SOONER OR LATER YOU WILL OWN GENERAL TIRE...niliipenda saana hii kauli mbiyu wakati wa kiwanda cha General Tire
 
Mimi siipendi CCM lakini sina shida na Kauli ya huyu mbunge. Jamani, tupo kwenye zama za mawazo huru na majadiliano. Mungu amenijalia akili na maarifa. Kwa maana hiyo siamini kama kuna swali lisilo na jibu.

Tukiwananga watu wanaotoa mawazo yao eti kwa sababu tu ya kutofurahishwa na wazo hilo itakuwa ni kosa na tunarudi kulekule. Kutofautiana hasa kimawazo na kifikra ndio rutuba yenyewe ya mwafaka.

Tujifunze kukubaliana kuto kukubaliana. Cha msingi tutende haki. Ni maoni yake ambayo yanaweza kujibiwa na wahusika wa swali. Kwangu mimi sioni kosa lake, maana ametoa maoni yake. Kwani maana ya uhuru wa mawazo ni nini?

Anayetaka kumjibu amjibu ila asihukumu. Kwa mfano, majibu ya swali lake yanaweza kuwa haya:
1. Bado uchumi wetu hautuwezeshi kuongeza mishahara ya watumishi wetu mbalimbali wakiwemo wabunge. Pale hali ya uchumi itakapotengemaa vizuri tutafanya hivyo.

2. Kwa kweli hoja yake ni nzuri maana inalenga ustawi wa wabunge na watumishi wengine wa bunge na wa sekta mbalimbali za serikali. Tunajitahidi kuweka mazingira mazuri ya kazi na uwekezaji ili tuwe na uwezo kama serikali wa kuwahudumia watu wengi wa makundi mbalimbali wakiwemo wabunge. Tunaamini tutafanikiwa na ikiwa hivyo hatutasita kuboresha maslahi wa watumishi na maisha ya watanzania kwa ujumla wao.

3. Yeye ni mbunge na anatamani angekuwa nacho kingi ili atatue shida za wananchi. Ni jambo jema, hata mimi natamani ningekuwa nacho kingi kuliko nilichonacho na kila mpenda maendeleo hupenda leo awe bopra na awe na vingi kuliko jana ili kutatua changamoto mbalimbali za kwake binafsi na za wananchi wake. Huwezi kutimiza matamanio hayo kwa kuwa na kiasi kidogo cha raslimali ikiwemo fedha. Tukifanikiwa kuwa na akiba ya kutosha ya fedha tunaboresha kipato cha mtu mmoja mmoja na makundi mbalimbali ya kijamii ikiwemo bunge.
 
Kuwatumikia wananchi lkn kwa malipo stahiki
Aachie ngazi, akaendelee na uchimbaji kwani wabunge sio sehemu ya wafanyakazi wa serikali??Raisi kesha weka wazi uchumi wetu bado hauko sawa kufanya nyongeza ya mishahara, wiki moja baadae Mbunge analeta hoja bungeni mishahara ya wabunge iongezwe tena kwa kufananishwa na mabunge mengine,mkuu kiuhalisia huyu mbunge ana bahati JIWE kaenda angedeal nae directly moto wake ungemuunguza na angejuta kwa nini aliongea hayo, kwanza amepelekwa tu bungeni kama hao wengine,huko ni kupingana na Raisi. kuitwa ngazi za juu za chama ni dhahiri,nina shaka pia na kisomo chake asije akawa ni wale msukuma &co.
 
Sasa mkuu @Sexless unaona kunahoja gani kuntu hapo isiyoweza kujibika kwa akili ya kawaida ...?
Ktk hoja zake, hoja na 4 inaonesha wazi kwamba huyu mbunge hayafahamu kabisa majukumu yake. Mbunge siyo mfadhili ama msamalia mwema. Na wala siyo kazi yake kuwagawia misaada wananchi.

Anapaswa kujenga mifumo bora ya wananchi kujipatia kipato.

Anyway, mkuu NestoryJ , mm nilitaka KM Chongolo atumie platform sahihi kumpa majibu ama elimu mbunge huyu. Angeweza kumuita, ama kumpigia simu, ama kuwa na kikao na wabunge wote, n.k badala ya kumtishia na kumtweza.
 
Aache kazi ana skills gani za kuajiriwa. Wametoka kupata millioni 400 kwa kukaa Dodoma for 3 months. Wana akili ya kuku viongozi wetu. Yeye analipwa allowance kwa kwenda kazi. Imbecile MPs. CCM has the power of expelling their members, this one has to go. He gets 12 million just for opening his mouth and vomiting uharo. Do we need MPS I really don’t understand their role, no one questions the government programs.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…