Kuna wakati niliwahi kuwaza kuwa kuwa tuchimbue na kuzamisha kina cha mto 1. Msimbazi tuunganishe na Bahari kupitia pale Salender Bridge, tujenge ukuta pale daraja la salender lenye Geti, maji yakija (kujaa) tuyaruhusu kuingia na ya kiondoka (kupwa) tunafunga turbine ya umeme hapo na tunafungulia maji yanaanza kuzungusha turbine na tunapata umeme rafiki kabisa.
2. Pia tunaweza kuyafungia huku huku juu bila kuyaruhusu maji hayo wakati wa kupwa , sasa mto uliosafishwa na wenye kina ukatumika katika utalii kwa kuweka boti humo watu wanazunguka kutoka salender, muhimbili, jangwani...tunaweza tukatanua hilo bonde mpaka kigogo...! NA hapa serikali ikapata ela ya kuboresha miradi ya maendeleo kwa watanzania wote.
3.Twaweza pia, kuhakikisha maji taka yote tunayapitisha kwenye bomba moja kubwa na yakamwagwa kilindini huko bahari, na hakuna mtu wala kiwanda kutupa taka kwenye mto huo bira kupitia bomba hili. sasa tukiwa na maji ya mto safi tunaweza kufuga samaki humo, tukawa na uhakika kabisa wa kitoweo safi.
Kupanga ni kuchagua.