Wakuu mimi nina mawazo tofauti kidogo,
Inawezekana kabisa Lowassa wa sasa ni tofauti na wa miaka ileee na inawezekana pia na yeye leo ufisadi unamkera kama unavyokukera wewe na ameshagundua kuwa ndio utakaomfanya akose urais lakini anashindwa aanzeje kuukemea.
Tumpe muda labda kuna siku atafunguka na kuweka yote wazi ambapo kila mtu atabaki kushangaa kumbe tumdhaniye ndiye siye.
Mkuu hii ni kuchochea kuni tu na si vinginevyo, Hapa Mbowe anajaribu kuwaambia ccm kuwa Wamfukuze au wamzuie tu Lowassa kugombea kupitia Ccm, na hili likitokea ni Mende kudondoka juu ya Marumaru akiwa miguu juu mgongo chini kwa ccm.
Mbowe na upinzani mzima wanachochoa kuni kwenye tanuri..!!
Ccm wakimpitisha Lowassa....nchale, Wasipompitisha...... nchale!!!!! Unajua kwanini?
Wakimpitisha Lowassa ndipo watakumbana na maswali magumu toka kwa wananchi, Je lile walilokuwa wakidai kuwa ni Gamba, lini imepata kuvuliwa na kubaki ngozi nyororo..? Hapa wataanguka asubuhi saa tatu kwenye uchaguzi..!!!
Wasipompitisha Lowassa, ndiposa Lowassa atatangaza hadharani kwamba ule ufisadi wa Richmond ulikuwaje? Nani muhusika na alihusika vipi..!! Lowassa anasiri nyingi za ccm maufisadi yote iwe ni Tangilod, EPA, Escrow na ufisadi wote mwingine unaoujua..!!! Unapopambana na Lowassa unapambana na Chenge, unapambana na Rostam, Unapambana na makundi yote makuu ya ufiaadi ndani ya ccm..!! Haya ndiyo yaliyoapa Lowassa lazima awe mgombea ndani ya ccm. Lengo lao kuu ni kulipa kisasi kwa yaliyowapata kisiasa ndani ya utawala huu.
Kama wao walipata ajali ya kisiasa basi lazima watu fulani wapate kifo cha kisiasa...!!!
Hiviq unakumbuka namna Rostam Azizi alivyojiuzulu nyadhifa zake zote ikiwemo Ubunge na Ujumbe wa NEC?? Unadhani aliondoka kwa Amani??
Mwaka hui tutaona mengi we subiri
BACK TANGANYIKA