Mbowe: Hali ya Lissu ni mbaya na yupo kwenye chumba cha upasuaji

Mbowe: Hali ya Lissu ni mbaya na yupo kwenye chumba cha upasuaji

Tofauti mie nadhani ipo! Hivi Muhimbili hupokea wagonjwa toka nchi jirani pia? (Hili swali langu ni kwa nia safi, nipopoe uone wakati mimi nataka kujuzwa tu)
Yah... tena saana tu.

Sent from "La -Vista"
 
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa na Kambi rasmi ya upinzani bungeni mheshimiwa Freeman Mbowe amesema Mhe.Lissu ameumizwa vibaya na yuko katika hali mbaya tangu saa 4 asubuhi hadi sasa yupo kwenye chumba cha upasuaji [HASHTAG]#Nairobi[/HASHTAG].

Chanzo: Redio One


Tundu Lissu afanyiwa upasuaji wa pili

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu Chadema amefanyiwa upasuaji mara ya pili katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya.

Mkuu wa Idara ya Uenezi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Hemedy Ally amesema tangu alipoingizwa katika chumba cha upasuaji saa nne asubuhi leo Septemba 8, hadi saa tisa alasiri alikuwa hajatoka lakini madaktari wamesema upasuaji huo unaendelea vizuri.

“Tangu jana alipofika alifanyiwa ‘stabilization’ ili aweze kukabiliana na upasuaji na zoezi hilo lilifanikiwa vizuri na madaktari wametueleza kuwa hakuna hali yoyote ya hatari na matibabu yake yanaendelea kwa mafanikio,” amesema.

Lissu aliwasili jijini Nairobi jana saa saba usiku akitokea mjini Dodoma katika Hospitali ya Mkoa ambako alipokelewa na timu ya madaktari katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta na kuanza kumtibu katika gari ya wagonjwa (Ambulance).

Wakati huo huo, balozi mbalimbali nchini ikiwamo Ubalozi wa Marekani na Umoja wa Nchi za Ulaya na taasisi za kitaifa na kimataifa zimeendelea kutuma salam za pole kwa Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), ambapo pamoja na mambo mengine wamelaani tukio hilo na kuitaka polisi kuchukua hatua

Lissu alipigwa risasi jana nyumbani kwake Area D, mjini Dodoma wakati akitokea katika kikao cha Bunge cha mchana.

Chanzo: Mtanzania

Bwana kasema nami kwamba mambo yatakuwa mazuri. Shetani alilokusudia, Mungu ataligeuza
 
*_Baba askofu Gwajima!!! Atangaza kuwa jumapili atakuwa na ibada ya maombezi kwaajili ya muheshimiwa Tundu Lissu kanisani kwake, ambapo maombi hayo yataambatana na kukemea na kulaani kitendo alichofanyiwa Rais wa Chama cha mawakili ambaye pia ni mbunge wa singida mashariki. Wale wote watakao guswa kuhudhuria ibada hiyo baba askofu anawakaribisheni._*

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walau jema moja alilowahi kulifanya...mh LISU limpe uhai arudi kututumikia wananchi wake...Eh Mungu Muweza wa yote mpe uponyaji wa haraka
 
Baba wewe ni Mungu wa wenye haki, unafanya njia pasipokuwa na njia , wewe ni Mungu usiyeshindwa !! Tunaomba umsimamie shujaa huyu aweze kupona kabisa na kurudi ktk majukumu yake ..
ameen

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukifikiria kibinadamu hiki si kitu kizuri, km wabunge wa chadema kutwa kukamatwa kwa kuongea kweli, km matawi ya chadema na wakiwa vikaoni wanavamiwa na kutishiwa kila siku hivi kwa tukio hili ni nani anayehusika km si selikari! Watu wanafungwa vinywa kwa nguvu hakuna uhuru, mm naona wazi chuki hofu kubwa wanatujengea, na km leo mwenzetu kafanyiwa ukatili huu ina maana hata wao watakuja kufanyiana tu, damu ya mtu huwa haimwagiki bure.

Tunapoelekea si pazuri tukitengeneza visasi hivi hapa patakuaje, bado tunajidanganya kazi nzuri inayofanywa! Hivi juzi tumeshuhudia msimamo wa wakenya lakini ss ni maneno na ujuaji tu hakuna hata mmoja wa kujaribu kupinga ili kupata ukweli ni mmoja tu ambaye leo tumeona wazi amekuwa adui!

Kwa kitendo hiki wametuonyesha kuwa wao ni watu gani, eti Mungu ibariki Tanzania atabariki kwa kipi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante kwa taarifa...

Shambulizi la watu waoga lipate kushindwa....

Wekeni silaha chini tubishane kwa hoja....

Eeh Mwenyezi Mungu weka mkono wako katika matibabu ya Mh TL....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu ukiandika "we are hardly praying for you...."means that we are not praying at all or just find it dificult to pray.
Nyoosha sentensi zako au rudi kwenye lugha yetu mama

Sent using Jamii Forums mobile app
If you are not a linguist be careful in criticism pertaining to grammar. It may be hardly praying as the person isn't happy, can't do it properly! Perhaps because of being sad, crying or in a critical condition.
 
Back
Top Bottom