Mbowe asalimu amri kwa Slaa

Mbowe asalimu amri kwa Slaa

Status
Not open for further replies.

Egnecious

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2015
Posts
894
Reaction score
994
Baada ya mwenendo wa Kampeni kuonekana kuwa mgumu huku kila alichoahidi Lowassa kutotimia mwenyekiti wa Chadema Taifa Freeman Mbowe aamua kukutana na aliyekuwa katibu wake Dkt. Wilbroad Slaa nchini Marekani.

Taarifa za uhakika ni kuwa Mbowe aliondoka nchini toka juzi na kupokelewa na wanachama wa Chadema tawi la DMV aliposhuka Uwanja wa Kimataifa wa Dulles huko Marekani ambapo Dkt. Slaa alimtangulia muda kidogo.

Taarifa zilizopatikana toka kwa moja ya viongozi wa tawi hilo aliyejulikana kama Kalley Pandukizi amesema ni kweli Mbowe na Slaa tumewapokea na wapo hoteli moja hapa Ohio kwa ajili ya mazungumzo binafsi. Amekiri baada ya kumpokea Mwenyekiti wao Mh. Mbowe walimpeleka moja kwa moja hotelini ambapo ndipo walipomkuta Dkt. Slaa.

Tetesi zaidi zinasema Mbowe amemuomba msamaha sana Dkt. Slaa na kumueleza walipotoka kwani mgombea waliomchukua anadhoofika kiafya kila kukicha kiasi kwamba mikutano mingine wananchi hawamsikii anapohutubia vile vile hakuna hata moja alilotimiza katika makubaliano kabla hatujampokea zikiwemo fedha za kampeni hivyo chama kinapata wakati mgumu wa kufanya kampeni kikamilifu.

Inasemekana Mbowe amemueleza Slaa kuwa ujio wa Lowassa umeigharimu Chadema kwani mpaka sasa John Mnyika hajakubali kupanda majukwaani kumnadi Lowassa kitu ambacho ni tabu zaidi kwao. Pamoja na vijana wa Lowassa kuuteka mchakato mzima wa kampeni hali inayokiuka makubaliano tuliyompa.

Kikubwa ni kuwa taarifa za ujumbe mfupi toka kwa Bi. Helen Ongara ambaye ni katibu wa BAWACHA tawi hilo la DMV ni kuwa Mwenyekiti huyo amepoteza tumaini hasa alipowapa video ya Mgombea akiomba kura kwa kigezo cha ulutheri kimewagharimu zaidi hivyo amedai watapigana ili wapate viti vya ubunge ila urais watapoteza.

Hata hivyo aliwadokeza kuwa kampeni zinaratibiwa na Lissu lakini wanafikiria kuchukua maamuzi magumu ya kuwatosa UKAWA ili wabaki wao kama wao kuliko sasa ambapo wanavibeba vyama vya NCCR MAGEUZI, NLD na CUF. Ambapo hata hivyo hali ya mpasuko imeanza kuonekana kupitia vyama vya CUF na NCCR MAGEUZI.

Walisahau Majuto ni mjukuu huja baadae!!

==========

Moderator:

Taarifa hii imekanushwa, mjadala unafungwa hadi itapoonekana unahitajika tena

attachment.php
 
Freedom is so close now, time will tell keep on dreaming
 
Bahati nzuri kama siyo mbaya kila mbinu mnazileta watunazijua yaani hata Aondoke huyo mbowe na wengine wengi Bado Lowasa ndiyo rais wa nchi Mwaka 2015 na kuendelea.
 
Watu wengine kwa kuchafua hewa hawajambo. Maccm mtaabika sana wiki ya tatu mwezi ujao.
 
Hapana shida kuwa mjinga,ila kuamua kufanya ujinga ni tatizo zaidi.
 
Ni kweli tangu Dk Slaa aondoke baadhi ya wafuasi wa CHADEMA asilia wamerudi nyuma.Ninavyoona kura watampa Magufuri.
 
Wakuombwa msamaha awe Dr.Slaa kweli!?, na mwombaji wa msamaha awe mbowe!!!!?.Hii itakuwa moja ya maajabu ya DUNIA.
 
Ngoja akome yeye mwenyewe si alisema lazima iwepo kafala sasa ameiona gharama ya kutoa kafala iliyo safi.
 
watu wanachanja mbuga kwenye kampeni kuelekea ikulu 52/10 wewe unazungumzia habari za slaa ambaye alishasaulika cdm
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom