UWEZO_WAKO
Member
- Nov 17, 2010
- 39
- 4
MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe, amedai kwamba chama chake kimebaini mpango wa CCM kutaka kukidhoofisha chama hicho bungeni na kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa NMC mjini hapa juzi, Mbowe alidai kwamba chama hicho tawala kinatumia dola kutekeleza mpango wake huo. Alikuwa akizungumza katika mkutano uliondaliwa na chama chake baada ya Mahakama kumvua Ubunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.
"Tunaionya Serikali ya CCM ijue kamwe hawatafanikiwa katika njama hizi na hata wakitupiga risasi mimi na Dk Willibrod Slaa, bado nguvu ya mageuzi nchini haitafutika kwani kuna makamanda wengi wapo ambao wanataka mabadiliko ya kweli katika nchi hii," alisema Mbowe.
Alisema nguvu ya chama hicho, bungeni haitapungua kutokana na kuondolewa Lema, bali imeongeza kiu ya kuendelea kupigania utawala wa haki.
"Tutakwenda bungeni kutetea mihimili mitatu ambayo ni Bunge, Mahakama na Serikali kutoingiliwa na kila kimoja kifanye kazi yake inavyostahili," alisema Mbowe.
Mbowe aliionya Polisi na Idara ya Usalama wa Taifa kuacha kuingilia mambo ya siasa kwa kukipendelea CCM huku akitamba kwamba kina uhakika wa kushinda Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Nape: Mbowe hana hoja
Alipoulizwa kuhusu madai hayo ya Mbowe, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema: "Hana hoja ya msingi."
Aliendelea: "Huwezi ukaiba halafu ukataka usishtakiwe. Wao (Chadema) wanatapatapa kwa kuwa wanajua walicheza rafu nyingi kwenye uchaguzi na wanajua mahakama itatenda haki."
"Ninawaomba Watanzania wawapuuze na namtaka Mbowe aziache Mahakama zifanye kazi yake ya kutenda haki. Mahakama ni chombo huru na kinapaswa kufanya kazi kwa uhuru bila kuingiliwa," alisema.
Rufani kesho
Chadema leo kinatarajia kufikisha Mahakama Kuu rufani ya kupinga kutenguliwa kwa matokeo ya ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini.
"Tutakwenda Jumanne Mahakama ya Rufani kwa majaji watatu kusikiliza rufani yetu, hatutaki majaji watupendelee Chadema au CCM. Tutawaomba watende haki kwani umma wa Watanzania unasubiri kwa hamu uamuzi wao,"alisema Mbowe.
Alisema kutokana na mazingira ya kesi hiyo na mahitaji ya Jimbo la Arusha Mjini kuwa na mwakilishi bungeni, wana imani rufani hiyo haitachukua muda mrefu kutolewa uamuzi.
Katika huku yake ya Aprili 5, mwaka huu, Jaji Gabriel Rwakibarila alitengua matokeo ya ubunge katika jimbo hilo na kumzuia Lema kugombea nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka mitano, baada ya kujiridhisha kuwa alitumia maneno ya kashfa, matusi na udhalilishaji dhidi ya aliyekuwa mgombea wa ubunge wa CCM, Dk Batilda Burian.
Source: Mwananchi
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa NMC mjini hapa juzi, Mbowe alidai kwamba chama hicho tawala kinatumia dola kutekeleza mpango wake huo. Alikuwa akizungumza katika mkutano uliondaliwa na chama chake baada ya Mahakama kumvua Ubunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.
"Tunaionya Serikali ya CCM ijue kamwe hawatafanikiwa katika njama hizi na hata wakitupiga risasi mimi na Dk Willibrod Slaa, bado nguvu ya mageuzi nchini haitafutika kwani kuna makamanda wengi wapo ambao wanataka mabadiliko ya kweli katika nchi hii," alisema Mbowe.
Alisema nguvu ya chama hicho, bungeni haitapungua kutokana na kuondolewa Lema, bali imeongeza kiu ya kuendelea kupigania utawala wa haki.
"Tutakwenda bungeni kutetea mihimili mitatu ambayo ni Bunge, Mahakama na Serikali kutoingiliwa na kila kimoja kifanye kazi yake inavyostahili," alisema Mbowe.
Mbowe aliionya Polisi na Idara ya Usalama wa Taifa kuacha kuingilia mambo ya siasa kwa kukipendelea CCM huku akitamba kwamba kina uhakika wa kushinda Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Nape: Mbowe hana hoja
Alipoulizwa kuhusu madai hayo ya Mbowe, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema: "Hana hoja ya msingi."
Aliendelea: "Huwezi ukaiba halafu ukataka usishtakiwe. Wao (Chadema) wanatapatapa kwa kuwa wanajua walicheza rafu nyingi kwenye uchaguzi na wanajua mahakama itatenda haki."
"Ninawaomba Watanzania wawapuuze na namtaka Mbowe aziache Mahakama zifanye kazi yake ya kutenda haki. Mahakama ni chombo huru na kinapaswa kufanya kazi kwa uhuru bila kuingiliwa," alisema.
Rufani kesho
Chadema leo kinatarajia kufikisha Mahakama Kuu rufani ya kupinga kutenguliwa kwa matokeo ya ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini.
"Tutakwenda Jumanne Mahakama ya Rufani kwa majaji watatu kusikiliza rufani yetu, hatutaki majaji watupendelee Chadema au CCM. Tutawaomba watende haki kwani umma wa Watanzania unasubiri kwa hamu uamuzi wao,"alisema Mbowe.
Alisema kutokana na mazingira ya kesi hiyo na mahitaji ya Jimbo la Arusha Mjini kuwa na mwakilishi bungeni, wana imani rufani hiyo haitachukua muda mrefu kutolewa uamuzi.
Katika huku yake ya Aprili 5, mwaka huu, Jaji Gabriel Rwakibarila alitengua matokeo ya ubunge katika jimbo hilo na kumzuia Lema kugombea nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka mitano, baada ya kujiridhisha kuwa alitumia maneno ya kashfa, matusi na udhalilishaji dhidi ya aliyekuwa mgombea wa ubunge wa CCM, Dk Batilda Burian.
Source: Mwananchi