Mbowe adaiwa kuficha ‘madudu’ Karatu

Mbowe adaiwa kuficha ‘madudu’ Karatu

Kimbori

JF-Expert Member
Joined
Feb 21, 2012
Posts
6,292
Reaction score
4,785
MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe amedaiwa kuficha ubadhirifu wa fedha za miradi mbalimbali ndani ya halmashauri ya Karatu wakati akijaribu kutatua mgogoro uliopo ndani ya chama hicho mjini humo.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), kutoka Wilaya ya Karatu, Daniel Awakii alisema hayo jana na kuongeza kuwa kuficha ubadhirifu sio uongozi bora. "Mbowe aeleze ukweli juu ya mgogoro wa uongozi karatu na asimung'unye maneno kwani huo sio utawala bora," alisema.

Awakii alisema hayo jana alipokuwa akizungumza katika mkutano wake wa hadhara katika Kijiji cha Barazani, Kata ya Mang'ola wilayani humo. Alihoji kwa nini Mbowe hakutoa msimamo wa chama, ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua viongozi hao kutokana na tuhuma mbalimbali zinazowakabili na badala yake amefanya kazi ya kuwapatanisha jukwaani tu.

Alisema viongozi hao waliopatanishwa wakiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Karatu, Lazaro Maasai na Diwani wa Karatu mjini, Jubilate Mnyenya ambaye pia ni Mwenyekiti Bodi ya mradi wa maji vijijini wilayani humo (KAVIWASU), walikuwa wakituhumiana kwa ufisadi.

Alifafanua kuwa viongozi hao wawili wamekuwa wakituhumiana kuwa mradi huo wa maji umekuwa hauendi vizuri kama inavyotarajiwa kutokana na Mnyenya kushindwa kuisimamia vizuri bodi yake na kusababisha kukosekana kwa maji katika mabomba ya wananchi huku yeye akipata maji katika miradi na mashamba yake.

Lazaro pia anadaiwa amekuwa akimtuhumu Mnyenya kwa kutumia fedha zinazopatikana kutokana na ada zinazokusanywa kutoka kwa watumiaji wa maji huku mradi huo ukishindwa kujiendesha na kusababisha huduma kukosekana kwa wateja ambao ni wananchi.

Mnyenya naye inadaiwa amekuwa akimtuhumu Lazaro kwamba ameuza kwa matajiri maeneo ya wazi likiwemo lililokuwa likimilikiwa na magereza na kukabidhiwa kwa vijana ili waendeshe shughuli zao za ufundi gereji na kusababisha vurugu na maandamano ya vijana hao.

Pia alidai Lazaro amekuwa akituhumiwa kutoa fedha za maendeleo kwa madiwani katika kata mbalimbali kwa upendeleo hususani kwa wale wanaomuunga mkono, hali iliyosababisha baadhi ya kata kukosa fedha hizo na kudorora kimaendeleo.

"Hivi jamani wananchi wenzangu mnamuelewaje Mbowe? Anakuja hapa kuwapatanisha na kusema ni viongozi muhimu kwa chama chake na kwamba tuweke maslahi ya chama mbele badala maslahi yetu huku mali na fedha zetu zikiliwa huu si ndiyo ufisadi wenyewe," alihoji Awakii. Gazeti hili lilipomtafuta Mbowe kwa njia ya simu jana kuzungumzia kauli ya Awakii, simu yake haikupatikana.


Chanzo: HabariLeo la leo.
 
Kumbe Chanzo ni Habari Leo

Si hivyo tu, aliyenukuliwa, chanzo cha habari hiyo ni mmoja wa watu wanaoitwa wa-NEC ambao juzi tuliambiwa na kuthibitishiwa na Mwenyekiti wa CCM Jakaya Kikwete kuwa walipatikana kwa rushwa.

Walitegemea kuwa CHADEMA itayumba katika matatizo yaliyojitokeza Karatu, sasa walipoona Mwenyekiti Mbowe amesuluhisha na kuumaliza mgogoro wa huo, wanaanza kuweweseka.
 
Awakii atuambie fedha za Epa, rada, meremeta, kagoda na mabilioni ya ughaibuni yatarudi lini? Ikiwa ana uhakika serikali iliyopo madarakani si ya ccm? Anasubiri nini kuwapeleka kwenye mahakama za ccm? Acha kutudanganya wana wana wa Karatu.
 
  • Thanks
Reactions: JGG
Si hivyo tu, aliyenukuliwa, chanzo cha habari hiyo ni mmoja wa watu wanaoitwa wa-NEC ambao juzi tuliambiwa na kuthibitishiwa na Mwenyekiti wa CCM Jakaya Kikwete kuwa walipatikana kwa rushwa.

Walitegemea kuwa CHADEMA itayumba katika matatizo yaliyojitokeza Karatu, sasa walipoona Mwenyekiti Mbowe amesuluhisha na kuumaliza mgogoro wa huo, wanaanza kuweweseka.

hivi unamalizaje mgogoro kinyemela wakati kuna tuhuma za ufisadi hapo?...au ndo style yenu .
 
hivi unamalizaje mgogoro kinyemela wakati kuna tuhuma za ufisadi hapo?...au ndo style yenu .

Mbowe alitoa wito kwa mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali akafanye special audit ya hesabu za halimashauri ya karatu! Sasa ameficha nini si mkachunguze mkaguzi wa serikali si wenu? Majungu ya nini?
 
hivi unamalizaje mgogoro kinyemela wakati kuna tuhuma za ufisadi hapo?...au ndo style yenu .

Mnasubiri nini kwenda mahakamani wakati ninyi ndiyo tuliowapa dhamana ya kulinda rasilimali zetu? Chadema wakilalamika kwa wananchi sawa kwani hawana serikali lakini ccm ni unafiki, acheni kuwahadaa watanzania.
 
Hapa ndipo viongozi wa CCM waposahau na kujipiga risasi wenyewe mguuni.

Siyo tuhuma zote zinakuwa ni ukweli kama ni hivyo basi CCM na serikali yake kwa tuhuma zilizopo ingekuwa imeishalemewa na zigo la tuhuma.

Hata hivyo kuna vyombo vinavyoshughulika na ubadhilifu wa fedha za wananchi, na ofisi zake ziko wazi kufanya kazi hiyo, siyo kazi ya chama.

Chama kimeishafanya kazi yake ambayo ilikuwa ni kusuruhisha.
 
Nashindwa kuamini kweli kutakuwa na utofauti endapo CDM, kitaingia madarakani ? tuache ushabiki tujiulize kwa maana Tanzania kwanza vyama baaadaye. hivi ktk halmashauri ya karatu kulikuwa na mgogoro wa nini?

Kulikuwa / hakukuwa na mgogoro baina ya viongozi ndani ya CDM? au kulikuwa / hakukuwa na mgogoro ndani ya halmashauri ya karatu inayooongozwa na CDM. ili watanzania wapate taarifa sahihi majibu yatolewe ili tutofautishe je?

Kulikuwa na UFISADI au ni MAJUNGU au PATANENI KUFICHA AIBU YA CHAMA au TATIZO NI MGAO HUU HAPA , AMBAO HAMJAPATA GAWANENI MAMBO YAISHE. kuondoa hisia hizo chama kiweke taarifa ya upatanishi hadharani.
 
nashindwa kuamini kweli kutakuwa na utofauti endapo CDM, kitaingia madarakani ? tuache ushabiki tujiulize kwa maana Tanzania kwanza vyama baaadaye. hivi ktk halmashauri ya karatu kulikuwa na mgogoro wa nini? kulikuwa / hakukuwa na mgogoro baina ya viongozi ndani ya CDM? au kulikuwa / hakukuwa na mgogoro ndani ya halmashauri ya karatu inayooongozwa na CDM. ili watanzania wapate taarifa sahihi majibu yatolewe ili tutofautishe je? kulikuwa na UFISADI au ni MAJUNGU au PATANENI KUFICHA AIBU YA CHAMA au TATIZO NI MGAO HUU HAPA , AMBAO HAMJAPATA GAWANENI MAMBO YAISHE. kuondoa hisia hizo chama kiweke taarifa ya upatanishi hadharani.

Kwa hiyo DC, katibu tawala na DED wameteuliwa na Chadema?
 
hivi unamalizaje mgogoro kinyemela wakati kuna tuhuma za ufisadi hapo?...au ndo style yenu .

Ha ha ha.. Umesahau wale wezi wa EPA waliopewa muda na Presidaaa warudishe pesa walizoiba BoT ili tuhuma zao zifutwe..! Style ya ccm hiyo..
 
MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe
amedaiwa kuficha ubadhirifu wa fedha za miradi mbalimbali ndani ya halmashauri ya Karatu wakati akijaribu kutatua mgogoro uliopo ndani ya chama hicho mjini humo.

Mbona umsemirais wako ambaye ana kigugumizi kuwataja walioficha pesa uswisi kama una uchungu ungekiuliza chama chako kwanini hao watu hawatajwi au kuchukuliwa hatua....

Mbona umsemi rais wako ambaye ana kigugumizi kuwataja walioficha pesa uswisi kama una uchungu ungekiuliza chama chako kwanini hao watu hawatajwi au kuchukuliwa hatua
 
Well said Awaki

Mh!Well said what?Awakii ni fisadi mkuu na mharibifu wa mazingira pale Karatu esp. kata ya Eyasi!Anatumia nguvu ya pesa alizonazo kuwanyanyasa wananchi na kuwanyang'anya ardhi zao!Amefyeka sehemu ya hifadhi ya msitu na ambayo pia ni vyanzo vya maji na kuvigeuza mashamba ya vitungu!Tuseme hapa,siyo ufisadi!?Awaki ni fisadi namber 1,amefanya ufisadi mwingi.Tumemnyamazia!Tatizo nyani haon kundule.
 
Nilifikiri kweli,kumbe ni propaganda za magamba!
 
Back
Top Bottom