MWENDOKASI MBEZI - KIMARA KARAHA TUPU
• Mfumo wa Kadi Waondolewa kwenye Magari
• Kadi zawa Lulu, Bei yake Kufuru
• Abiria warundikana Vituoni wakisubiri kupata Risti
Na Mbusule C. Shillu,
Usafiri wa Mwendokasi umekuwa Kero kwa Wakazi wa maeneo ya Mbezi ya Kimara na maeneo ya jirani kutokana na kujikita katika kufanya biashara badala ya huduma. Lengo lao ni kutengeneza faida kubwa zaidi (Super Profit) kuliko kuondoa Kero ya Usafiri kwa Abiria.
Mara tu baada ya Usafiri huu kuzinduliwa, ulianzishwa Mfumo wa Kadi ambazo ziliuzwa Tshs. 500 tu na abiria angeweka Salio la Nauli anayotaka ingawa kiasi cha juu (kikomo) ilikuwa Tshs. 30,000/- ambayo mtu angeitumia kwa muda mrefu kusafiri.
Nauli kwa kadi kutoka Mbezi kwenda Posta, Ubungo, Kariakoo, Kinondoni na kwingineko baada ya Kimara ikawa Tshs. 800/- tu na inaendelea mpaka sasa.
Hata hivyo, mfumo wa Risti uliendelea sambamba na mfumo wa Kadi kwa maelezo kuwa ulikuwa wa muda mfupi tu wakati abiria wakiendelea kukata Kadi. Risti kutoka Mbezi kwenda Kimara ikawa Tshs. 400/- na kutoka Kimara kwenda Kariakoo, Kivukoni, Morocco, Ubungo, Magomeni na kwingineko kuelekea Mjini ikawa Tshs. 650/- kwa route. Na kwa mantiki hiyo kufanya nauli ya route moja kutoka Mbezi kwenda Mjini kuwa Tshs. 1050/- ukiachilia mbali usumbufu wa kupanga foleni kukata Risti na kupoteza muda mrefu kusubiri gari.
Ghafla Kadi ziliadimika na hazijawahi kutolewa tena mpaka sasa na mbaya zaidi hivi karibuni Magari mengi ya kutoka Mbezi yameondolewa Mashine za kutumia Kadi kwa kile kinachoonekana wazi kuwa wanataka faida kubwa zaidi (Super Profit); yaani kupata Tshs. 1,050/- badala ya 800/-
Kutokana na "Vyuma Kukaza", biashara ya Kadi imepamba moto miongoni mwa abiria ambapo abiria mwenye Kadi anamuuzia Mhitaji kwa bei anayoona inafaa. Leo nimemshuhudia abiria akinunua kadi kwa Tshs. 50,000/- tena isiyo na Salio.
Changamoto zingine za Mfumo huu ni pamoja na;
1. Magari kuchelewa kufika Vituoni na hivyo kupelekea abiria kupoteza Muda mwingi wakingoja Gari. Hii inatokana haswa na Magari mengi kubaki "Depot" (Parking) ilhali uhitaji ni mkubwa vituoni.
2. Magari kujaza kupita kiasi hali inayopelekea abiria hasa wafupi kukosa hewa. Juzi nimemshuhudia Mmama akianguka kwa kukosa hewa. Bahati nzuri, dereva alikuwa mwelewa, akasimamisha gari na kwenda dukani kumtafutia Maji ya kunywa. Abiria walisikika wakisema, "Tutakufa" na walishuka Kituo kilichofuata nikiwemo mimi ingawa nilikuwa sijafika.
3. Kugoma mara kwa mara kwa Mfumo wa Mashine Vituoni. Mfumo wa kuongeza Salio kwenye Kadi mara nyingi hugoma na hivyo kumlazimu abiria kukata Risti.
4. Kukosekana kwa Uongozi. Abiria akiwa na kero Kituoni, hakuna namna ya kuiwasilisha kwa wakati ikafanyiwa kazi. Wafanyakazi waliopo Vituoni hawana majibu ya Kero za abiria.
Nini kifanyike?
1. Kuwe na Kampuni shindanishi la Usafiri. Hii itaongeza uwajibikaji na ufanisi kwa kuwa watajua wakizembea "watapigwa bao" na Mshindani wao. Mfano Mzuri ni kabla ya daladala za kawaida kuzuiliwa, Kadi zilitolewa na ufanisi ulikuwa juu.
2. Kuwepo kwa usimamizi wa Karibu kutoka Serikalini na hasa Sumatra kuhusu Bei, Ufanisi na Upatikanaji wa Kadi.
3. Mamlaka husika ziwe na utaratibu wa Ziara za Mara kwa Mara Vituoni ikiwa ni pamoja na kuhoji abiria.
4. Pawepo na Uongozi wa Kampuni lenyewe unaozungukia Vituo vya Usafiri na kufanyia Kazi Kero za Abiria ikiwa ni pamoja na Mfumo wa Kadi.
Hitimisho;
Mfumo huu wa Usafiri Ukiboreshwa na kusimamiwa vizuri ni mzuri sana na utastarabisha Jiji letu la Dar es Salaam. Lakini ukiendelea kuzorota kama ilivyo sasa, si tu utaumiza abiria lakini pia utakuwa fedheha kwetu na kwa wageni kutoka Mataifa mengine kwa kuwa Dar es Salaam ni USO wa Nchi yetu.
Mbusule Christopher Shillu
• Mfumo wa Kadi Waondolewa kwenye Magari
• Kadi zawa Lulu, Bei yake Kufuru
• Abiria warundikana Vituoni wakisubiri kupata Risti
Na Mbusule C. Shillu,
Usafiri wa Mwendokasi umekuwa Kero kwa Wakazi wa maeneo ya Mbezi ya Kimara na maeneo ya jirani kutokana na kujikita katika kufanya biashara badala ya huduma. Lengo lao ni kutengeneza faida kubwa zaidi (Super Profit) kuliko kuondoa Kero ya Usafiri kwa Abiria.
Mara tu baada ya Usafiri huu kuzinduliwa, ulianzishwa Mfumo wa Kadi ambazo ziliuzwa Tshs. 500 tu na abiria angeweka Salio la Nauli anayotaka ingawa kiasi cha juu (kikomo) ilikuwa Tshs. 30,000/- ambayo mtu angeitumia kwa muda mrefu kusafiri.
Nauli kwa kadi kutoka Mbezi kwenda Posta, Ubungo, Kariakoo, Kinondoni na kwingineko baada ya Kimara ikawa Tshs. 800/- tu na inaendelea mpaka sasa.
Hata hivyo, mfumo wa Risti uliendelea sambamba na mfumo wa Kadi kwa maelezo kuwa ulikuwa wa muda mfupi tu wakati abiria wakiendelea kukata Kadi. Risti kutoka Mbezi kwenda Kimara ikawa Tshs. 400/- na kutoka Kimara kwenda Kariakoo, Kivukoni, Morocco, Ubungo, Magomeni na kwingineko kuelekea Mjini ikawa Tshs. 650/- kwa route. Na kwa mantiki hiyo kufanya nauli ya route moja kutoka Mbezi kwenda Mjini kuwa Tshs. 1050/- ukiachilia mbali usumbufu wa kupanga foleni kukata Risti na kupoteza muda mrefu kusubiri gari.
Ghafla Kadi ziliadimika na hazijawahi kutolewa tena mpaka sasa na mbaya zaidi hivi karibuni Magari mengi ya kutoka Mbezi yameondolewa Mashine za kutumia Kadi kwa kile kinachoonekana wazi kuwa wanataka faida kubwa zaidi (Super Profit); yaani kupata Tshs. 1,050/- badala ya 800/-
Kutokana na "Vyuma Kukaza", biashara ya Kadi imepamba moto miongoni mwa abiria ambapo abiria mwenye Kadi anamuuzia Mhitaji kwa bei anayoona inafaa. Leo nimemshuhudia abiria akinunua kadi kwa Tshs. 50,000/- tena isiyo na Salio.
Changamoto zingine za Mfumo huu ni pamoja na;
1. Magari kuchelewa kufika Vituoni na hivyo kupelekea abiria kupoteza Muda mwingi wakingoja Gari. Hii inatokana haswa na Magari mengi kubaki "Depot" (Parking) ilhali uhitaji ni mkubwa vituoni.
2. Magari kujaza kupita kiasi hali inayopelekea abiria hasa wafupi kukosa hewa. Juzi nimemshuhudia Mmama akianguka kwa kukosa hewa. Bahati nzuri, dereva alikuwa mwelewa, akasimamisha gari na kwenda dukani kumtafutia Maji ya kunywa. Abiria walisikika wakisema, "Tutakufa" na walishuka Kituo kilichofuata nikiwemo mimi ingawa nilikuwa sijafika.
3. Kugoma mara kwa mara kwa Mfumo wa Mashine Vituoni. Mfumo wa kuongeza Salio kwenye Kadi mara nyingi hugoma na hivyo kumlazimu abiria kukata Risti.
4. Kukosekana kwa Uongozi. Abiria akiwa na kero Kituoni, hakuna namna ya kuiwasilisha kwa wakati ikafanyiwa kazi. Wafanyakazi waliopo Vituoni hawana majibu ya Kero za abiria.
Nini kifanyike?
1. Kuwe na Kampuni shindanishi la Usafiri. Hii itaongeza uwajibikaji na ufanisi kwa kuwa watajua wakizembea "watapigwa bao" na Mshindani wao. Mfano Mzuri ni kabla ya daladala za kawaida kuzuiliwa, Kadi zilitolewa na ufanisi ulikuwa juu.
2. Kuwepo kwa usimamizi wa Karibu kutoka Serikalini na hasa Sumatra kuhusu Bei, Ufanisi na Upatikanaji wa Kadi.
3. Mamlaka husika ziwe na utaratibu wa Ziara za Mara kwa Mara Vituoni ikiwa ni pamoja na kuhoji abiria.
4. Pawepo na Uongozi wa Kampuni lenyewe unaozungukia Vituo vya Usafiri na kufanyia Kazi Kero za Abiria ikiwa ni pamoja na Mfumo wa Kadi.
Hitimisho;
Mfumo huu wa Usafiri Ukiboreshwa na kusimamiwa vizuri ni mzuri sana na utastarabisha Jiji letu la Dar es Salaam. Lakini ukiendelea kuzorota kama ilivyo sasa, si tu utaumiza abiria lakini pia utakuwa fedheha kwetu na kwa wageni kutoka Mataifa mengine kwa kuwa Dar es Salaam ni USO wa Nchi yetu.
Mbusule Christopher Shillu