Uchaguzi 2020 Mbeya ya Magufuli na Maendeleo yake hii hapa

jijiletublog

Member
Jul 23, 2020
31
74
Miradi iliyotekelezwa na inayotekelezwa kwa mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2019/2020 katika halmashauri ya wilaya ya Mbeya ni pamoja na ujenzi wa stendi ya Mbalizi kiasi cha shilingi milioni 150 zilizopelekwa na serikali ya awamu ya tano, SAT.

mradi wa ujenzi wa zahanati katika shule ya wasichana Galijembe milioni 60 zilipelekwa, zahanati hii ni faida kwa wanafunzi, walimu na wananchi kwa ujumla kwani inawarahsishia kupata huduma za afya kwa wakati.

Ujenzi wa ukamilishaji wa soko la tunduma road, Ujenzi wa machinjio ya muda Utengule Usongwe jumla ya shilingi milioni 25 zilipelekwa. Kukamilika kwa ujenzi wa maeneo haya kunawaongezea wananchi fursa ya kufanya biashara katika mazingira salama ikiwa ni kwa wote, wfanyabiashara wakubwa na wadogo.

Ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa na ofisi moja katika shule ya sekondari Usongwe kiasi cha shilingi milioni 10 zilipelekwa. Pongezi ziende kwa raisi wetu JPM na serikali yake ya awamu ya tano Pamoja na watanzania kwa ulipaji wao wa kodi kwani ndiko mafanikio yalikotokea.

Halmashauri ya wilaya ya Mbeya, chini ya uongozi wa raisi JPM katika kuongeza vyanzo vya mapato ya ndani imeamua kugharamia ujenzi wa soko la Tunduma Road lenye jumla vichanja 521 ili kuwawezesha wafanyabiashara wa eneo hilo kufanya biashara katika mazingira mazuri.

SAT, chini ya uongozi wa raisi JPM imewezesha utoaji wa ruzuku ya msingi kwa walengwa wa TASAF katika vijiji 105 katika kata 28, ambapo jumla ya Tshs. 1,135,452,000.00 zililipwa kwa walengwa 9,460.

Shule ya sekondari wasichana Galijembe iliyopo katika Tarafa ya Tembela, Kata ya Tembela katika kijiji cha Galijembe ilianza kujegwa na wananchi kwa kushirikiana na wadau wafanya biashara kuanzia mwaka fedha 2008 ilipo anza kujegwa shule hii hadi mwaka huu 2019/2020, ujenzi wa shule hii umetumia jumla ya shilingi TSHS. 794,453,610.04 milioni. Pongezi kwa SAT kwa kushirikiana na wananchi katika kulifanikisha suala hili.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 27 Aprili, 2019 alifungua barabara ya lami ya Mbeya – Chunya na aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya lami ya Chunya – Makongolosi, zote zikiwa ni sehemu ya barabara kuu ya Mbeya – Makongolosi – Rungwa yenye urefu wa kilometa 528. Ujenzi wa barabara ya lami ya Mbeya – Chunya yenye urefu wa kilometa 72 umegharimu shilingi Bilioni 140 na ujenzi wa barabara ya Chunya – Makongolosi uliopangwa kukamilika Januari 2020 uligharimu shilingi Bilioni 62.7, fedha zote zimetolewa na Serikali ya Tanzania, chini ya uongozi wa JPM.

UJENZI WA MELI
SAT, chini ya ungozi wa raisi JPM, imehakikisha Ujenzi wa meli tatu zinazogharimu kiasi cha shilingi bilioni 20.1 katika bandari ya Itungi. Ujenzi huo wa meli unatekelezwa na kampuni ya kitanzania Songoro Marine umejumuisha ujenzi wa meli mbili za mizigo zenye uwezo wa kubeba tani 1000 za mizigo kila moja na meli ya abiria na mizigo yenye uwezo wa kubeba abiria 200 na tani 200 za mizigo.

Ujenzi wa meli mbili za mizigo za MV Njombe na MV Ruvuma ulikamilika mwezi Julai, 2017 na kusajiliwa na Mamlaka ya udhibiti wa shughuli za vyombo vya majini, (TASAC) na kuanza safari zake za awali kwenda Mbamba Bay Ruvuma na Nkhata Bay nchini Malawi mwezi Septemba, 2017 kwa MV Njombe na Januari, 2018 MV Ruvuma. Na meli ya MV Mbeya II hatimaye ilianza safari zake tarehe 5 october , 2020.

IMG-20201021-WA0047.jpg
 
Alisema mwenyewe hadharani kwamba yeye anasikiliza zaidi wanawake weupe kuliko weusi! Hivi huyu naye mweupe kweli au macho yangu yana ukungu?
Uwe unapanua zaidi masikio Ili kusikia na ubongo ufanye kazi yake Ili uelewe zaidi hata kama umeishia darasa la Saba,

Hivi Umesahau hata zile Nahau na methali?
 
20 October 2020
Mbeya, Tanzania

CHADEMA 2020 Mbeya mjini
'Prime minister' wa Mbeya mjini kamanda John Mwambigija alonga maneno mazito akiwa kata ya Nsalaga mjini Mbeya akiwa ziarani mitaani kuongezea mtaji wa kura walizopata CHADEMA2015 ili kumaliza ubishi 2020

 
Mizizi ya CHADEMA jijini Mbeya imetoka mbali na ni juhudi za bure kutaka kuiungoa CHADEMA katika jimbo la Mbeya mjini

 
Watinga Mbeya kujaribu kuokoa jahazi

UVCCM waingia katika dakika za lala salama kujaribu kusaidia jahazi linalozama baada ya kimbunga cha CHADEMA2020, je wataweza ?

Pamoja na viongozi wa kitaifa CCM kufika Mbeya, ukiwatazama na kusoma nyuso zao na lugha ya miili yao (body language) viongozi wa CCM Mkoa wa Mbeya waliopo meza-kuu waonesha wamepoa, hawajiamini na wanajua Mbeya ni pagumu CCM kushinda yaani mission impossible (harakati-shindwa)
 
Watinga Mbeya kujaribu kuokoa jahazi

UVCCM waingia katika dakika za lala salama kujaribu kusaidia jahazi linalozama baada ya kimbunga cha CHADEMA2020, je wataweza ?

Huyu mtoto wa Dada anapiga Siasa za miaka ya Sabini
 
Miradi iliyotekelezwa na inayotekelezwa kwa mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2019/2020 katika halmashauri ya wilaya ya Mbeya ni pamoja na ujenzi wa stendi ya Mbalizi kiasi cha shilingi milioni 150 zilizopelekwa na serikali ya awamu ya tano, SAT.

mradi wa ujenzi wa zahanati katika shule ya wasichana Galijembe milioni 60 zilipelekwa, zahanati hii ni faida kwa wanafunzi, walimu na wananchi kwa ujumla kwani inawarahsishia kupata huduma za afya kwa wakati.

Ujenzi wa ukamilishaji wa soko la tunduma road, Ujenzi wa machinjio ya muda Utengule Usongwe jumla ya shilingi milioni 25 zilipelekwa. Kukamilika kwa ujenzi wa maeneo haya kunawaongezea wananchi fursa ya kufanya biashara katika mazingira salama ikiwa ni kwa wote, wfanyabiashara wakubwa na wadogo.

Ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa na ofisi moja katika shule ya sekondari Usongwe kiasi cha shilingi milioni 10 zilipelekwa. Pongezi ziende kwa raisi wetu JPM na serikali yake ya awamu ya tano Pamoja na watanzania kwa ulipaji wao wa kodi kwani ndiko mafanikio yalikotokea.

Halmashauri ya wilaya ya Mbeya, chini ya uongozi wa raisi JPM katika kuongeza vyanzo vya mapato ya ndani imeamua kugharamia ujenzi wa soko la Tunduma Road lenye jumla vichanja 521 ili kuwawezesha wafanyabiashara wa eneo hilo kufanya biashara katika mazingira mazuri.

SAT, chini ya uongozi wa raisi JPM imewezesha utoaji wa ruzuku ya msingi kwa walengwa wa TASAF katika vijiji 105 katika kata 28, ambapo jumla ya Tshs. 1,135,452,000.00 zililipwa kwa walengwa 9,460.

Shule ya sekondari wasichana Galijembe iliyopo katika Tarafa ya Tembela, Kata ya Tembela katika kijiji cha Galijembe ilianza kujegwa na wananchi kwa kushirikiana na wadau wafanya biashara kuanzia mwaka fedha 2008 ilipo anza kujegwa shule hii hadi mwaka huu 2019/2020, ujenzi wa shule hii umetumia jumla ya shilingi TSHS. 794,453,610.04 milioni. Pongezi kwa SAT kwa kushirikiana na wananchi katika kulifanikisha suala hili.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 27 Aprili, 2019 alifungua barabara ya lami ya Mbeya – Chunya na aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya lami ya Chunya – Makongolosi, zote zikiwa ni sehemu ya barabara kuu ya Mbeya – Makongolosi – Rungwa yenye urefu wa kilometa 528. Ujenzi wa barabara ya lami ya Mbeya – Chunya yenye urefu wa kilometa 72 umegharimu shilingi Bilioni 140 na ujenzi wa barabara ya Chunya – Makongolosi uliopangwa kukamilika Januari 2020 uligharimu shilingi Bilioni 62.7, fedha zote zimetolewa na Serikali ya Tanzania, chini ya uongozi wa JPM.

UJENZI WA MELI
SAT, chini ya ungozi wa raisi JPM, imehakikisha Ujenzi wa meli tatu zinazogharimu kiasi cha shilingi bilioni 20.1 katika bandari ya Itungi. Ujenzi huo wa meli unatekelezwa na kampuni ya kitanzania Songoro Marine umejumuisha ujenzi wa meli mbili za mizigo zenye uwezo wa kubeba tani 1000 za mizigo kila moja na meli ya abiria na mizigo yenye uwezo wa kubeba abiria 200 na tani 200 za mizigo.

Ujenzi wa meli mbili za mizigo za MV Njombe na MV Ruvuma ulikamilika mwezi Julai, 2017 na kusajiliwa na Mamlaka ya udhibiti wa shughuli za vyombo vya majini, (TASAC) na kuanza safari zake za awali kwenda Mbamba Bay Ruvuma na Nkhata Bay nchini Malawi mwezi Septemba, 2017 kwa MV Njombe na Januari, 2018 MV Ruvuma. Na meli ya MV Mbeya II hatimaye ilianza safari zake tarehe 5 october , 2020.

View attachment 1606969
Pwenti
 
Kajengo ka CCM Mkoa Ni Kama choo Cha shule ya Msingi. Iko located kwenye mtaa Independence na mtaa wa Wageni nyumba namba mbili. CCM Mkoa inatazama shule ya Loleza na jengo la ghorofa la UMATI
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom