MBEYA: Wananchi wenye hasira kali wamshambulia mtuhumiwa wa wizi

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,621
8,411

Mwanamume ambaye hakutambulika jina lake mara moja amenusurika kifo baada ya kupata kipigo kwa raia wenye hasira kali kwa tuhuma za kuiba Pesa kwenye duka la Jumla jijini Mbeya.


Wananchi waliomkamata kijana huyo ambaye alikiri kuhusika tuhuma hizo za wizi alisema alikuwa na wenzake ambao walikimbia pasipo fahamika huku akionekana kuiuzongwa na wananchi waneneo hilo ambao wanadai kuwa marakadhaa kumekuwapo vijana wanaofanya uhalifu na kurudisha maisha nyuma.

Muda mfupi baada ya tukio hilo Jeshi la Polisi Mkoani humo lilifika na na kuokoa maisha ya kijana huyo ambayo yalikuwa hatarini na kumpakiza kwenye gari na kuondoka naye kwaajili ya mahojiano zaidi na kufahamu sababu za yeye kusadikiwa kuiba pesa duka la jumla.

Hata hivyo haikufahamika nikiasi gani cha fedha kilichokuwa kikiibiwa na Kijana huyo aliyekuwepo na wenzake katika duka hilo.

Chanzo: ITV
 
Wananchi wenye hasira za maisha wazimalizia hasira zao kwa mwizi, na hali inavyozidi kuwa ngumu mbona wezi watakoma.
 
Wezi wa dar huwa hawapigwi, wanabembelezwa sana km watoto wadogo. Dar kila kona ni wezi tu, upande kweny dala dala kuna wezi cha ajabu kuna sehemu wanaiba mchana kbsa. Dar unaishi maisha ya wasi was sana, iwe mchana au siku. Huwa nachoka, kuna vibaka sana,
MWANZA hata ukiiba karanga tu za 200 wanakuchoma moto.
 
Back
Top Bottom