Magazeti mengi sasa hivi yamekua yanatabia za Ki-udakuudaku tu U-shankupeshankupe tu.
Tanzania kwa sasa tumebakia na magazeti machache sana ambayo mtu mwenye akili timamu iliyotulia na wala sio shankupe unaweza nunua na kusoma.
Waandishi wengi wa habari wananjaa sana kuliko hata njaa waliyokuanayo mabaamedi. Tasnia ya habari inaendelea kuiweka nchi pabaya kwa sababu ya njaa zao ambazo haziwezi kuisha kwa vijisenti wanavyo hongwa. Wanahabari wananafasi kubwa tu ya kuifanya nchi ikapata viongozi bora ambao wanaweza kuijenga nchi na kuiendeleza nchi yetu. Lakini kwa njaa zao wameshindwa hata kujithamini juu ya umuhimu wao. Magazeti kama haya hayapaswi kunuliwa, na yanatakiwa kupigwa vita kwa namna yeyote ile.
Tatizo lenu ni kutopokea mitazamo tofauti na kilke mnachokiamini. Kwa sababu tu habari haisifii CDM basi waandishi wanasumbuliwa na njaa kama ma barmaid, poleni sana.
Nadhani wengi hamzifahamu siasa za Mbeya au ni ushabiki tu, Mwaiseje alikaa term moja baada ya kushindwa kutekeleza yale aloahidi, CCM imetawala muda mrefu baadaye.
Asipojirekebisha Sugu naye ni mbunge wa term mmoja, na hili hata ndani ya CDM Mbeya linafahamika, anaendesha siasa za kitoto, kila siku ni ugomvi na matusi dhidi ya viongozi hapa mkoani, wengi wamemchoka, amebaki na wapigadebe pale Kabwe.
Sugu alianza kuporomoka muda mfupi sana baada ya uchaguzi, bahati yake ni upunzi wa Meya Kapunga na aliyekuwa RAS, Mama Swai waliokuwa na ajenda yao ya kuwang,oa Mkurugenzi na Mkuu wa Mkoa, wakatumia machinga wa Mwanjelwa kwa kutengua kinyemela maamuzi yao wenyewe kisha kutamka kuwakomoa vijana pale mwanjelwa, mgogoro huo ndio uliomrudisha tena kwenye chart, lakini hakuielewa katika picha hiyo, hivyo hajafanya la maana kulishikilia hilo kundi.
Mbeya watu wanabadiliko kulingana na mtu unavyo perform na hawaleweshwi na jina la mtu au umaarufu wake.