Mbeya imepotea na Mark Mwandosya?

Lugombo Nsesi

Senior Member
Joined
Jun 16, 2016
Posts
126
Reaction score
149
Kustaafu kwa mwanasiasa mkongwe na nguli katika mkoa huo, kumepelekea mkoa mzima kupooza kabisa. Mwanasiasa huyo aliwaminisha watu wa Mbeya kwa kiasi kikubwa sana kuwa ana uwezo na ni kweli aliweza kuwatumikia wananchi wa mkoa huo kwa nguvu zake zote, aliaminika mnoo!
Amestaafu siasa mkoa mzima umepoa kabisa.

Nasikitika kuona wapinzani hasa CHADEMA kuota mizizi mkoani humo. Wapo viongozi wakongwe mkoani humo ila hawafani kazi Kama Mark Mwandosya, tunakoelekea Mbeya itakua ngome ya upinzani.

Viongozi wa kitaifa ni kama hawaujui vizuri mkoa huo, ukiwasikiliza zaidi wananchi wa huko wanasema eti wameachwa, au wametelekezwa.

Wanadai mikoa ya Kaskazini imependelewa zaidi. Waliotoa malalamiko yao wanatoa mfano kua hata miradi ya nyumba za NHC jijini humo hakuna ili kuufanya mkoa huo kua na mandhali nzuri.

Mbeya na Mark Mwandosya ni Kama wote wanapotea!!
 

Mkuu matatizo ya Mark Mwandosya na Mkoa wa Mbeya yalianza na Mtandao wa Kikwete.
Kosa ilikuwa kuwa wa tatu katika kinyang'nyiro cha urais mwaka 2005.

Jamaa alipgwa vita na Lowasa , alipigwa vita na Mkuu wa Mkoa Mwakipesile, alipigwa vita na hata CCM yenyewe mpaka ikawa mbaya.
Watu wa Mbeya nawafahamu, vijana kuingia kushabikia CHADEMA ilikuwa a direct reaction kwa nguli wao kupigwa vita vya wazi wazi.
Nakumbuka Waziri Mkuu Lowasa wakati huo alipotembelea Mbeya, Mwandosya aliimbiwa "Raisi...raisi....raisi..." na vijana wa Mbeya mjini.
Kitendo hicho kilimuudhi sana Lowasa, lakini hiyo ilielezea jinsi Mwandosya alivokubalika sana mkoani Mbeya, tena na makabila yote mkoani.

The powers that be wakati huo waliamua kumdhibiti Mwandosya kisiasa.
Kugombea NEC mwaka 2007 walimwekea kijana mdogo anaitwa Thomas Mwang'onda, mtoto wa kigogo wa sekta ya intellijensia, Abson Mwang'onda.

Fedha nyingi sana zilitumika kumnadi Thomas, kiasi kufikia bilioni moja.
Lakini kijana Thomas aliangukia pua!
Mwandosya aliwahi kulalamika katika kitabu kimoja jinsi alivyokuwa akipigwa rafu, na serikali yake, na chama chake CCM!
Hatuwezi kuunganisha , lakini mara Mwandosya aliyekuwa akionekana fit na anafanya mazoezi kila alipopata wasaa mitaani, akaanza kuugua.
Wengine wanadai aliwekewa sumu kama ile ya Dr Harrison Mwakyembe, lakini hilo halijathibitishwa.

Kugombe tena mwaka 2015 ilikuwa just going through the motions, Mwandosya alisha umizwa vibaya.
Mwishoni alipoishiwa nguvu masikini Mwandosya akaamua kurudi kupumzika kijijini kwake Lufilyo, Zaidi ya kilometa 100 toka hata mjini tukuyu.

Kwa maoni yangu serikali ya CCM ndiyo iliyo utoa mkoa wa Mbeya kwenda CHADEMA, kwa kumdhibiti kipenzi cha wana Mbeya, Prof Mark mwandosya.
Mategemeo ni ingalau Mheshimiwa John Pombe Magufuli atupie jicho mkoa huu wenye potential kubwa sana,
 
Akina Mwakyembe wako wapi sasa?
Wangesaidia kazi za Mzee Mwandosya

Ni Kama nao hawapo huko, wakati furani walivuma sanaa
 
Alipokuwa waziri wa mawasiliano,akawajengea kiwanja cha ndege Songwe Airport,wanambeya watamkumbuka kwa Hilo.
Songwe kujengwa ni kwa sababu ya strategic reasons, kufungua mikoa ya nyanda za juu kusini ili kupata fursa za SADC na wale tuliowasaidia wakat wa harakati za ukombozi. Ni makosa kuamin uwanja ulijengwa kwakuwa Mwandosya alikuwa uchukuzi na mawasiliano. Umewahi kusikia kuhusu Mtwara corridor? Ilikuwaje mwanataaluma asiye na mizizi kwenye chama kushika nafasi ya tatu mwaka 2005 nyuma ya Kikwete na Salimu? Hapo kuna jibu la kwann uwanja wa songwe.
 
Profesa mzima tena wa Engineering kweli anakuwa mwanasiasa?
Kwan alikuwa profesa wa engineering MIT au hapa udsm katika nchi ambayo bajeti yake ya utafiti ni 1/5 ya bajeti ya Kenya ya utafiti? Kuwa mwanataaluma sio Ishu ktk nchi hii, ukitaka kufanya mabadiliko ya kweli inabidi uingie kwenye siasa ili wababaishaji wote wasipate fursa ya kutuongoza. Baada ya Mwalimu Nyerere, ungetegemea tupate vichwa kweli kutuongoza, lakini wapi.
 
Kwa nini asihame au ni lazima agombee kupita CCM? naona hajiamini hata kidogo, wanaume ni kaskazini wana maamuzi ya kweli
Mkuu Mwandosya anajua Zaidi, he knows better kuliko kukosaliti chama chake.
Sasa ni wakati wa chama kusahihisha makosa yake kwa mkoa wa Mbeya.
 
Nasikitika kuona wapinzani hasa CHADEMA kuota mizizi mkoani humo. Wapo viongozi wakongwe mkoani humo ila hawafani kazi Kama Mark Mwandosya, tunakoelekea Mbeya itakua ngome ya upinzani.


Hao wapinzani ni foreigners? kaeni chini kuandika mambo ya maendeleo kwa mkoa wenu, mnapokanyagana na kulumbana kila usiku na mchana mnapoteza muda
 
Makosa ya kudidimia kwa CCM mkoani Mbeya culprit ni CCM yenyewe.
 
Tukuyu hadi Lufilyo ni kama kilometres 50 hivi
 
Wewe unijua mbeya au umendika habari za kuhadithiwa maana yake habari yote ya mwandosya na sifa ulizompa si za kweli.kama umelipwa kumtakasa huyo bwana umepitwa na wakati
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…