Nakapanya
JF-Expert Member
- May 22, 2012
- 2,096
- 709
panapo majaliwa kesho nitakuwepo ndani ya sokoine stadium kushuhudia mtanange wa kukata na shoka kati ya Mbeya city (watoto wa jiji) na Tanzania Prison (wajela jela).
Kiufupi leo kutwa nzima hapa Mbeya mechi hiyo ndio inazumgumziwa sana na kila mtu ana morali ya kwenda kushuhudia kabumbu hilo huku Mbeya City wakionekana kupata spoti kubwa ya wanambeya.
Maeneo yote ya Mbeya kuanzia Igawilo,uyole,Sae,Ilomba,Mama John,Soweto,Kbwe mwanjelwa,Airport,Uhindini,Isanga,Ilemi,soko matola,majengo,Iyunga,Mabatini,Nzovwe na maeneo mengine yametawala rangi za zambarau na nyeupe kuonyesha kuwa wanaisapoti Mbeya City FC.
Wana Mbeya wengi wanaisapoti Mbeya City kama timu ya wananchi na kuichukulia kama ndio mwokozi wao ukilinganisha na Prison ambayo ipo chini ya Jeshi la Magereza,pia wana Mbeya wengi hawaipendi Prisoni na hii ni baada ya miaka ya nyuma Prison kuwahama Wana mbeya na kuhamia Dsm kabla hawajarudi tena mbeya kiyendo kilichowaudhi sana wana Mbeya.
Kwa kifupi mechi itakuwa kali sana na yenye ushindani huku Mbeya city wakipambana kuendelea kubaki katika nafasi za juu upande mwingine Prison wakitaka kujikwamua kutoka katika nafasi za chini.Historia inaonyesha ni Prison ndio waliwafunga Mbeya city katika ligi daraja la kwanza msimu wa 2012/13 (nisahihishwe kama nimekosea mwaka) mechi iliyopelekea Prison kupanda daraja na kuwanyima nafasi Mbeya city kuingia ligi kuu kabla hawajafinikiwa safari hii kuingia ligi kuu na kufanya maajabu.
Sasa je itakuwa ni zamu ya Mbeya City kulipa Kisasi au wataendelea kuwa wateja Prison?ikumbukwe mpaka sasa Mbeya City Fc haijafungwa hata mechi moja.
Stori zote tupige hapa na matokeo pia tupeane hapa.
Kiufupi leo kutwa nzima hapa Mbeya mechi hiyo ndio inazumgumziwa sana na kila mtu ana morali ya kwenda kushuhudia kabumbu hilo huku Mbeya City wakionekana kupata spoti kubwa ya wanambeya.
Maeneo yote ya Mbeya kuanzia Igawilo,uyole,Sae,Ilomba,Mama John,Soweto,Kbwe mwanjelwa,Airport,Uhindini,Isanga,Ilemi,soko matola,majengo,Iyunga,Mabatini,Nzovwe na maeneo mengine yametawala rangi za zambarau na nyeupe kuonyesha kuwa wanaisapoti Mbeya City FC.
Wana Mbeya wengi wanaisapoti Mbeya City kama timu ya wananchi na kuichukulia kama ndio mwokozi wao ukilinganisha na Prison ambayo ipo chini ya Jeshi la Magereza,pia wana Mbeya wengi hawaipendi Prisoni na hii ni baada ya miaka ya nyuma Prison kuwahama Wana mbeya na kuhamia Dsm kabla hawajarudi tena mbeya kiyendo kilichowaudhi sana wana Mbeya.
Kwa kifupi mechi itakuwa kali sana na yenye ushindani huku Mbeya city wakipambana kuendelea kubaki katika nafasi za juu upande mwingine Prison wakitaka kujikwamua kutoka katika nafasi za chini.Historia inaonyesha ni Prison ndio waliwafunga Mbeya city katika ligi daraja la kwanza msimu wa 2012/13 (nisahihishwe kama nimekosea mwaka) mechi iliyopelekea Prison kupanda daraja na kuwanyima nafasi Mbeya city kuingia ligi kuu kabla hawajafinikiwa safari hii kuingia ligi kuu na kufanya maajabu.
Sasa je itakuwa ni zamu ya Mbeya City kulipa Kisasi au wataendelea kuwa wateja Prison?ikumbukwe mpaka sasa Mbeya City Fc haijafungwa hata mechi moja.
Stori zote tupige hapa na matokeo pia tupeane hapa.