Mbatia kuongoza POAC!

Mbatia kuongoza POAC!

Status
Not open for further replies.
Hoja yako haina mantiki yeyote,hizo ni propaganda ambazo hazina tija,hoja yako bado haijaeleweka.
 
Kama kawaida yenu CHADEMA, mtaendelea kumwandama Mwenyekiti wetu hata lini? Kama watu wenu wamekula rushwa, hangaikeni na hilo na mjue namna ya kulishughulikia, sio kusingizia eti ni njama zinazohusiana na POAC au 2015.

Nawashaurini badala ya kujitahidi kuchafua watu wasiokuwa wa vyama vyenu kwa hofu ya kwamba wanaweza kuwaondoa katika nafasi zenu, wahakikishieni watanzania kwamba mnao uwezo wa kuwashughulikia wala rushwa wanaobainika miongoni mwenu.

Hamjamsoma Dr. Lwaitama leo? "Mmeshindwa kujipambanua kisera badala yake mmechagua uzushi na mashindano ya matusi"

Jiulize kwanini jk kamteua kuwa mbunge kwani ccm wameisha wa kuteuwa? Ukipata jibu nadhani ukweli wa hii thread utauona
 
sasa niwazi kuwa lile sakata linaloendelea ndani ya wizara ya madini na nishati linachukua sura mpya, wale mnaowaona wakipiga kelele ni kuwa si bure, vita yote hiyo nia ni kumngoa Zitto Kabwe na muda simrefu James Mbatia atateuliwa kuwa mwenyekiti wa POAC,
James Mbatia ni mwanasiasa mwenye utata mwingi kuhusu kile aanachosimamia, mfano:

1. ndiye aliyeongoza kampeni miaka ya nyuma ile ilyohakikisha CUF kule Zanzibar imekosa wabunge 6 wakati ule akitumiwa na CCM, na bado anajulikana kama mpinzani

2. alishiriki kikamilifu kuisambaratisha NCCR mageuzi wakati wa Mrema

3. alimfungulia kesi Halima Mdee kule Kawe huku akijua kuwa yeye alikuwa mshindi wa tatu, na kwa vyo vyote vile CCM wangekuwa beneficiary kama Mdee angeshindwa ile kesi.

4. alishiriki kumwengua David Kafulila uanachama na hivyo kuuweka ubunge huo mashakani

Ninazo habari za karibu kuwa mbatia anatumiwa na mafisadi walioko kwenye kambi za urais za CCM, wanampigia chapuo ili achukue nafasi ya Zitto huko POAC, ifikapo 2015 ameahidiwa kuwa atasaidiwa pesa za kampeni ili chama chake cha NCCR kipate wabunge angalua wengi kuliko CHADEMA na kuwa upinzani rasmi bungeni. FUATILIENI KWA KARIBU NA SIKU MOJA MTAKUMBUKA THREAD HII

Koteeee umekwenda sawa, hapo kwenye Red siamini hata kidogo, hao CHICHIEM ingekuwa ni matakwa yao yaani nadhani kusingekuwepo na vyama hata vya upinzani hata kama havina wabunge, sasa iweje leo wapate huruma ya kuki-support chma pinzani ikiwa kuwapo kwa Chama tu pinzani ni nongwa kwao!? umedanganya maono yako si ya kweli! lala tena uje na maonio mpya!!
 
Wampe tu.

Kwani hilo bunge wabunge wake wengi walitokana na rushwa & uchakachuaji. Halitokani na wananchi kwa uhalisia wa neno ndio maana limejaa maigizo, vijembe na ufisadi. Na wala bunge lemyewe halina maslahi ya Taifa ndani yake, so to make such a move will just make a cup full.
 
Jiulize kwanini jk kamteua kuwa mbunge kwani ccm wameisha wa kuteuwa? Ukipata jibu nadhani ukweli wa hii thread utauona

Siwezi kuwa na mtazamo wa namna hiyo kuhusu ukweli. Na hata wewe huwezi kusema kwa hakika ni kwanini aliteuliwa, unabaki na hisia hisia, shuku shuku tu, tena zinazochagizwa na ushabiki wa kisiasa. Tangia hapo yeye sio mpinzani wa kwanza kuteuliwa kuwa mbunge. Rejea pia kwenye misingi ya katiba na sheria, Katiba inayompa mamlaka rais kuteua wabunge, inamruhusu kumteua mtu yeyote bila kujali itikadi yake.
 
Mimi nilijiunga CHADEMA nikijua ni wapinga rushwa,nadhani wengi tulijiunga kwa sababu hiyo,kwamba cdm ilionekana ni mbadala kwa siasa za tz,ninaumia sana nikisikia CHADEMA wakihusishwa na rushwa,

Kwa akili zangu ili CHADEMA iendelee kuwa maarufu hapa tz, isipoteze mvuto wake kwa wananchi, ni busara kumfukuza zitto uanachama kama kweli itathibitika kuwa anahusika pamoja na wenzake akina sendeka,unapingaje mafisadi wakati wewe ni fisadi pia?

CHADEMA wasiogope hakuna aliye maarufu kuzidi chama chenyewe

tatiizo la wapinzani wengi wanatoka chini sana, zitto bila uzoefu mkubwa wa kazi akaingia bungeni na kuanza kazi vizuri kukosoa serikali huku akipata umaarufu mkubwa, na hili likawa tatizo mtu kama huyu hawezi kumudu umaarufu na nguvu aliyoipata ghafla na ukichukulia ametoka wapi....kitaalam tunaweza kusema ZZK grew beyond his limitation of character ni sawa na wale wanaoshinda lottery halafu unasikia wamefiliska. zzk alivyoanza kurub shoulder na jk na mawaziri akajiona basi sasa mungu anipe nini badala ya kujenga yale yaliyomfikisha hapo.

dalili zilianza pale aliposema mitambo ya dowans inunuliwe hata kama itakiuka kanuni hii ilikua red flag kubwa....sasa kama ni gamba CDM mtadili nalo
 
Ni mwenyekiti wa Nishati na madini au mashirika ya uma naona kama kuna kuchanganya madesa hapa........
 
Nitashangaa sana kama Spika atafanya blunder na kumuweka Mbatia maana kwa kufanya hivyo chama kikukuu cha Upinzani bungeni kitakuwa kimeondolewa kwenye kamati zote za 'oversight' kinyume na kanuni za bunge. Mrema anatoka TLP, na Mzee Cheyo ni UDP. Kamati wanazoongoza wawili hawa kama tungekuwa na Spika mwenye nia safi zilitakiwa ziwe chini ya CHADEMA, lakini (pengine kwa maagizo maalum) Spika alibadilisha 'tafsiri' ya neno upinzani na ndipo wakawapachika Mrema na Mzee Cheyo. Sasa atarudia mkorogo ule ule na kutoa kamati kwa NCCR- Mageuzi?
 
wahenga wanasema 'wenye busara husikiliza na kuangalia kabla ya kutoa kauli'. Bado nasikiliza uchunguzi utakuja na ushahidi wa kuwahusisha waliotuhumiwa? Innocent until proved guilty.
 
sasa niwazi kuwa lile sakata linaloendelea ndani ya wizara ya madini na nishati linachukua sura mpya, wale mnaowaona wakipiga kelele ni kuwa si bure, vita yote hiyo nia ni kumngoa Zitto Kabwe na muda simrefu James Mbatia atateuliwa kuwa mwenyekiti wa POAC,
James Mbatia ni mwanasiasa mwenye utata mwingi kuhusu kile aanachosimamia, mfano:

1. ndiye aliyeongoza kampeni miaka ya nyuma ile ilyohakikisha CUF kule Zanzibar imekosa wabunge 6 wakati ule akitumiwa na CCM, na bado anajulikana kama mpinzani

2. alishiriki kikamilifu kuisambaratisha NCCR mageuzi wakati wa Mrema

3. alimfungulia kesi Halima Mdee kule Kawe huku akijua kuwa yeye alikuwa mshindi wa tatu, na kwa vyo vyote vile CCM wangekuwa beneficiary kama Mdee angeshindwa ile kesi.

4. alishiriki kumwengua David Kafulila uanachama na hivyo kuuweka ubunge huo mashakani

Ninazo habari za karibu kuwa mbatia anatumiwa na mafisadi walioko kwenye kambi za urais za CCM, wanampigia chapuo ili achukue nafasi ya Zitto huko POAC, ifikapo 2015 ameahidiwa kuwa atasaidiwa pesa za kampeni ili chama chake cha NCCR kipate wabunge angalua wengi kuliko CHADEMA na kuwa upinzani rasmi bungeni. FUATILIENI KWA KARIBU NA SIKU MOJA MTAKUMBUKA THREAD HII

Hawezi kitu kama wenyewe wameshindwa kuisambaratisha CDM pamoja na pesa itakuwa yeye? acheni tu naye apate kaugali kake jamani. Mi wala haniumizi kichwa.
 
spika kuivunja poac ni dhahiri kabisa...
Mbatiya sio mbunge kutoka upinzani, ni mbunge wa ikulu japo ni mwanachama wa upinzani. NCCR haikumwingiza Mbatiya bungeni, kwa maneno mengine hata akihamia CCM leo, atabaki na ubunge wake!
Bottom line he is always a pain in .....
 
ifikapo 2015 ameahidiwa kuwa atasaidiwa pesa za kampeni ili chama chake cha Nccr kipate wabunge angalua wengi kuliko cdm

Mkuu hapo kwenye wekundu hakuna kiasi cha fedha kinachoweza kufanikisha hilo lengo.

Hizo pesa wampe sana, zitaliwa na wabunge atapata wachache kuliko alionao sasa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom