Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 87,498
- 151,717
Kwa sababu mtu mwenye kiu ya kuona maji sehemu ambayo hamna maji hata akiona taswira inayotokana na jua kali kupiga ardhi ya jangwa (mirage) atakimbilia na kutumaini ni maji.Tuseme labda uko sawa lkn swali langu ni kwamba ni kwa nini wote au wengi wanafikiri kwamba ni Raisi bora hasa nje ya mipaka ya Tanzania? Kwa maana siyo mara ya kwanza kusikia watu wa nje ya Tanzania wakitamani kuwa na Raisi kama Magufuli na wengi wanamtumia kwenye Kampeni zao kuanzia Zambia, Malawi, Ghana mpaka Afrika Kusini kuna article nimesoma wakimtaka J. Zuma ajifunze ktk kwa Raisi Magufuli tena niliona wanafunzi wameshika poster wakiandamana AK na na jina la Raisi Maguguli sasa Je ni kwa nini? Labda kuna kitu wewe unakiona kumhusu Raisi Magufuli ambacho wengi wetu ndani na nje ya Tanzania hatukioni?
Hili halijaanza leo. Miaka ya 1990s dunia nzima ilikuwa inamuandika vizuri sana Museveni, angalia leo wanavyomsema.
Kuna article moja kwenye Wall Street Journal la Ijumaa au Jumamosi wameandika hiyo habari ya Museveni alivyowabadilikia watu.
Magufuli hatakuwa wa kwanza kuwahadaa watu.
Hao wanasiasa wa Afrika wote wanatapatapa tu, wakiona jina lolote jipya linaweza kuwapa kick wanalitumia.