Mazoea

Red Scorpion

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2012
Posts
5,736
Reaction score
4,254
*MITOMINGI*; nadhani sasa mgeni amekwisha kumaliza kula hebu nenda kaondoe vyombo

*MAMA_MAZOEA*; Basi fanya haraka (Mazoea anatoka, anaenda kwa Ngoswe alipo).

*MAZOEA*; Hodi! Hodi!

*NGOSWE*; Karibu

*MAZOEA*; (Akiingia). Ahsante. Nimekuja kuchukua vyombo.

*NGOSWE*; Vyombo! Kaa basi mbona unasimama kama vile hakuna viti.

*MAZOEA*; Nimeambiwa nifanye haraka.

*NGOSWE*; Mmm! Haya ngoja ninawe basi (Ngoswe ananawa kwa taratibu jicho likiwa usoni mwa Mazoea ambaye anatazama kando). Hivo mzima wee?

*MAZOEA*; Bee?

*NGOSWE*; Salama?

*MAZOEA*; Salama tu.

*NGOSWE*; Sasa ndio umekataa kukaa?

*MAZOEA*; (Ajidai hakusikia) Si umekwisha maliza?

*NGOSWE*; Bado kidogo.

*MAZOEA*; Basi nitakuja chukua baadaye. (Ataka kutoka)

*NGOSWE*; Basi nenda navyo. (Mazoea anarudi kuinama kuvichukua. (Ngoswe kwa sauti ndogo). Hivyo waitwa nani?

*MAZOEA*; Mie?

*NGOSWE*; Ndio wewe hapo kisura.

*MAZOEA*; (anatabasamu huku akiondoka). Mazoea!i

Story ni tamu ila tulishaambiwa ya Ngoswe tumuachie Ngoswe! ! !

 
Waambie Bavicha....
Wamuache Mukulu apige Kazi..!
 
Penzi kitovu cha uzembe, hiki ni kitabu cha Taifa
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…