Mayanja asema yanga bingwa ,awataka viongozi wa simba wasiingilie benchi la ufundi

py thon

JF-Expert Member
Sep 11, 2016
2,471
4,424
Aliyekuwa kocha msaidizi wa simba Jackson mayanja ,amesema iwapo uongozi wa simba utaendelea kuingilia kazi za benchi la ufundi,wasijeshangaa yanga ikiendelea kupeta msimu huu kwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara.

Mganda huyo alisema kuwa ubora wa kikosi cha simba msimu huu unaweza kuzaa matunda ,ikiwamo kutwaa ubingwa msimu huu iwapo tu viongozi hawataingilia kazi za benchi la ufundi .

Mayanja amesema kocha anatakiwa kufanya majukumu yake ya uwanjani na kuangalia kikosi chake anachokiamini na kuona wachezaji ambao watamfaa katika mechi hiyo kutokana na wapinzani anaokutana nao.

Amesema kama endapo watafanya hivyo ,hana shaka kabisa na ubingwa kwa msimu huu kwenda simba ,lakini kama uongozi utaingilia majukumu ,ana imani ubingwa utakuwa ni historia na mashabiki wa timu ya simba watajikuta wakiendelea kulizwa na watani wao wa jadi ,yanga.

Aliendelea kusema simba ina wachezaji wazuri na wenye uzoefu mkubwa wa michuano mikubwa,hivyo anaamini kila mmoja akifanya majukumu yake timu hiyo itafikia malengo ya kutwaa ubingwa.
ee8b9207a9406206c4ad0fae55811e4f.jpg


Mayanja kaondoka kwa kile kinachodaiwa matatizo ya kifamilia lakini kilio chake angependa kuona viongozi wa timu wakiendeleza mikakati yao huku wakiwaachia bench la ufundi linaloongozwa na Omog kufanya majukumu yao kwa Uhuru bila kubughudhiwa.
 
Kasema ukweli kabisa, Viongozi wasimpangie Kocha la sivyo kila mwaka Yanga tutawashangaza...

Walilia point fc badilikeni
 
Kasema ukweli kabisa, Viongozi wasimpangie Kocha la sivyo kila mwaka Yanga tutawashangaza...

Walilia point fc badilikeni
Mkuu, acha waendelee kumpangia Yanga ipete kama kawaida.
Ugonjwa wa kumuingilia kocha kwenye kazi zake ulimalizwa na Manji pale Jangwani. Matunda yake tumeyaona
 
Simba na ubingwa wapi na wapi?Mikia kwa sasa wamebakia kua wasema ovyo tu ishu ya ubingwa wamejua sio saizi yao.
 
Hii sio habari nzuri kwa wadau wa Simba lkn ina kila dalili ya ukweli mtupu.

Tabia ya kupangia makocha timu imepelekea hadi mashabiki nao bila aibu wameanza kumpangia kocha kikosi. Simba iko too desperate lkn hawapaswi kupeana pressure kupita kawaida, wakituliza mpira, hakuna timu ya kunyakua kombe lolote mbele yao msimu.
 
Mkuu, acha waendelee kumpangia Yanga ipete kama kawaida.
Ugonjwa wa kumuingilia kocha kwenye kazi zake ulimalizwa na Manji pale Jangwani. Matunda yake tumeyaona
ni kweli kabisa SHAURI ZAO mbumbumbu fc
 
Back
Top Bottom