Katika video inayozunguka kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, inamuonyesha mwandishi wa habari nguli ambaye pia ni mwanasheria na mwanaJF ndugu Pascal Mayalla , akidai kuwa alilazimishwa kukiri kosa alipoitwa na JAB kujitetea kwanini ametoa maoni yasiyopendwa na utawala kuhusu tukio moja la kisiasa lililotokea hivi karibuni.
Your browser is not able to display this video.
Katika video hiyo, ambayo Mayalla ameonekana amevaa miwani myeusi huku akihojiwa na mwandishi nguli wa DW, Sudi Mnede, ameonekana wazi kukerwa na wito alioitwa na mamlaka kujitetea kwanini ametoa maoni ya kuudhi watawala. Ukimwangalia usoni na jinsi anavyojibu utaona wazi kuwa hakupendezwa na kitendo cha kulazimishwa kukiri kosa kinyume cha sheria. Soma
Kufuatia kukamiwa kwa jukwaa la JF na utawala, nimeshindwa kuambatanisha video hiyo kwani kila nikiweka inagoma kupakilika. Tafadhali kama kuna mods au mtu yeyote anayeweza kunisaidia kuweka video hiyo nitashukuru sana.
Katika video inayozunguka kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, inamuonyesha mwandishi wa habari nguli ambaye pia ni mwanasheria na mwanaJF ndugu Pascal Mayalla , akidai kuwa alilazimishwa kukiri kosa alipoitwa na JAB kujitetea kwanini ametoa maoni yasiyopendwa na utawala kuhusu tukio moja la kisiasa lililotokea hivi karibuni.
Katika video hiyo, ambayo Mayalla ameonekana amevaa miwani myeusi huku akihojiwa na mwandishi nguli wa DW, Sudi Mnede, ameonekana wazi kukerwa na wito alioitwa na mamlaka kujitetea kwanini ametoa maoni ya kuudhi watawala. Ukimwangalia usoni na jinsi anavyojibu utaona wazi kuwa hakupendezwa na kitendo cha kulazimishwa kukiri kosa kinyume cha sheria. Soma
Kufuatia kukamiwa kwa jukwaa la JF na utawala, nimeshindwa kuambatanisha video hiyo kwani kila nikiweka inagoma kupakilika. Tafadhali kama kuna mods au mtu yeyote anayeweza kunisaidia kuweka video hiyo nitashukuru sana.