kijembeee
JF-Expert Member
- Jun 6, 2012
- 409
- 105
Nitoe rai kwa waziri na wizara husika, tume ya ushindani na kwa raisi kuangalia kwa ukaribu jambo hili.
Nimefanya uchunguzi mdogo nimegundua madudu haya, uchunguzi wa kina utagundua mengi zaidi, hivyo vyombo husika vifanye majukumu yake ipasavyo
USHAURI: KAMPUNI YA MAXCOM ICHUNGUZWE KATIKA HAYA MACHACHE, NA MENGI ZAIDI YATAGUNGULIKA KWENYE HII KAMPUNI YA KITAPELI
Usalama wa servers na taarifa za wateja na usalama wa taifa
Usalama wa server zao unatia mashaka, natumai uchunguzi ukifanyika hili litabainika, labda wawe wamefanya mabadiliko baada ya kusoma makala hii.
Ukizingatia kua mfumo wao unaunganishwa na mitandao ya serikali kama TRA, ni vyema kujiridhisha na usalama wa server zao, ili kuhakikisha hali ya usalama.
Pia kwakua ni kampuni inayokua na ipo kwenye sekta nyeti sana, ni vyema iwe lazima wapate kibali cha ISO , ili kuhakikisha hawafanyi biashara zao kienyeji enjeji.
Ni vyema kujua Kuna cyber attacks, na shambulio kwa kampuni hii ni kwamba mwendokasi haitafanya kazi,matrafki nao siku hio wataweka pesa mfukoni etc, na kadri siku zinavyokwenda na wanavyohonga kupata tenda, itafika wakati wamepata tenda kwenye sekta nyeti zaidi na cyber attack itakua na madhara makubwa sana.
Mfumo wa biashara kwa mikoani umeambatana na utapeli
Kampuni hii inafanya kazi Tanzania nzima, na pia ina wasambazaji wa bidhaa mikoa yote, kwa miaka mingi tatizo ni kwa baadhi ya mikoa mingi kampuni haina ofisi, na biashara zinafanyikia barabarani hivyo kusababisha watu wengi kutapeliwa fedha na watu wanaojifanya kua ni maajenti wa maxcom, na pia wateja waliotoa pesa taslimu hawapewi risiti, hivyo kukosa kielelezo kama kweli walitoa pesa
.Ni jukumu la kampuni kulinda wateja wake na kuhakikisha kua ina ofisi isiyohamishika, ili kulinda maslahi ya mteja.
Matangazo ya uongo kwa bidhaa ambazo hazipo kwenye mashine.
Tume ya ushindani na serikali kwa ujumla imekalia kimya swala la wateja wa bidhaa kutoka maxcom kulaghaiwa mchana kweupe. Kampuni hii kwa miaka mingi kupitia matangazo yake imedai kutoa huduma nyingi, ambazo nyingine ni mapambo tu, hazipo kwenye mashine, na timu ya mauzo imedanganya wateja kuhusu uwepo wa bidhaa hizo kwenye mashine ilihali bidhaa hizo hazipo, au zipo kwa kiwango kidogo tofauti na ilivoelezwa kwa tangazo. Mfano wa bidhaa hizo ni huduma za tigo pesa, airtel money ambazo kiuhalisia hazipo, mambo ya pensheni na huduma za hospitali zote zimewekwa kama mapambo kuvutia wateja. Wanaponunua ndio wanagundua wametapeliwa.
Hii si haki kwa mteja. Inabidi walipe faini kwa kudanganya uma.
Tume ya ushindani kumlinda mteja juu ya bidhaa ambayo mara nyingi mtandao upo chini
POS za maxmalipo zinakumbwa na tatizo ambalo ni la muda mrefu, na limekua sugu la mtandao kua chini, hivyo mteja alienunua bidhaa hio kwa sababu ya kuzungusha pesa yake anapokumbwa na tatizo la mtandao siku nzima kisa hio siku kuna mawingu, au mtandao umekorofisha siku nzima sio haki, na uonevu kwa mteja na kampuni inatakiwa imlipe mteja kwa biashara aliopoteza kwa siku hio.
Kuvunja mkataba na mteja kuhusu umbali wa msambazaji mmoja na mwingine.
Mkataba kati ya mteja wa mashine na kampuni ni kwamba, kampuni haitamuuzia mtu mwingine mashine wa eneo jirani na biashara ya mteja wa kwanza ili kulinda maslahi ya mteja huyo(kumlinda na ushindani).kampuni haijatekeleza sharti hili la mkataba, na imekua ikiuza mashine bila kuzingatia hili, hivyo kuwafanya wateja wa mashine hizo walizonunua awali wakijua kua katika maeneo husika watakua ndio watoa huduma pekee, kupatwa na hali ya simanzi na kuhisi kutapeliwa.
Kufukuza wafanyakazi bila kufata taratibu
Wafanyakazi wa kampuni hii hawajaandikishwa kwenye vyama vya wafanyakazi, na hivyo kuna uonevu mkubwa kwa wafanyakazi, na uchunguzi ukifanyika utabaini ubabe na kufukuzwa kazi kwa wafanyakazi wengi pasipo kufata taratibu za wafanyazi (Tanzania Labor Laws)
Nimefanya uchunguzi mdogo nimegundua madudu haya, uchunguzi wa kina utagundua mengi zaidi, hivyo vyombo husika vifanye majukumu yake ipasavyo
USHAURI: KAMPUNI YA MAXCOM ICHUNGUZWE KATIKA HAYA MACHACHE, NA MENGI ZAIDI YATAGUNGULIKA KWENYE HII KAMPUNI YA KITAPELI
Usalama wa servers na taarifa za wateja na usalama wa taifa
Usalama wa server zao unatia mashaka, natumai uchunguzi ukifanyika hili litabainika, labda wawe wamefanya mabadiliko baada ya kusoma makala hii.
Ukizingatia kua mfumo wao unaunganishwa na mitandao ya serikali kama TRA, ni vyema kujiridhisha na usalama wa server zao, ili kuhakikisha hali ya usalama.
Pia kwakua ni kampuni inayokua na ipo kwenye sekta nyeti sana, ni vyema iwe lazima wapate kibali cha ISO , ili kuhakikisha hawafanyi biashara zao kienyeji enjeji.
Ni vyema kujua Kuna cyber attacks, na shambulio kwa kampuni hii ni kwamba mwendokasi haitafanya kazi,matrafki nao siku hio wataweka pesa mfukoni etc, na kadri siku zinavyokwenda na wanavyohonga kupata tenda, itafika wakati wamepata tenda kwenye sekta nyeti zaidi na cyber attack itakua na madhara makubwa sana.
Mfumo wa biashara kwa mikoani umeambatana na utapeli
Kampuni hii inafanya kazi Tanzania nzima, na pia ina wasambazaji wa bidhaa mikoa yote, kwa miaka mingi tatizo ni kwa baadhi ya mikoa mingi kampuni haina ofisi, na biashara zinafanyikia barabarani hivyo kusababisha watu wengi kutapeliwa fedha na watu wanaojifanya kua ni maajenti wa maxcom, na pia wateja waliotoa pesa taslimu hawapewi risiti, hivyo kukosa kielelezo kama kweli walitoa pesa
.Ni jukumu la kampuni kulinda wateja wake na kuhakikisha kua ina ofisi isiyohamishika, ili kulinda maslahi ya mteja.
Matangazo ya uongo kwa bidhaa ambazo hazipo kwenye mashine.
Tume ya ushindani na serikali kwa ujumla imekalia kimya swala la wateja wa bidhaa kutoka maxcom kulaghaiwa mchana kweupe. Kampuni hii kwa miaka mingi kupitia matangazo yake imedai kutoa huduma nyingi, ambazo nyingine ni mapambo tu, hazipo kwenye mashine, na timu ya mauzo imedanganya wateja kuhusu uwepo wa bidhaa hizo kwenye mashine ilihali bidhaa hizo hazipo, au zipo kwa kiwango kidogo tofauti na ilivoelezwa kwa tangazo. Mfano wa bidhaa hizo ni huduma za tigo pesa, airtel money ambazo kiuhalisia hazipo, mambo ya pensheni na huduma za hospitali zote zimewekwa kama mapambo kuvutia wateja. Wanaponunua ndio wanagundua wametapeliwa.
Hii si haki kwa mteja. Inabidi walipe faini kwa kudanganya uma.
Tume ya ushindani kumlinda mteja juu ya bidhaa ambayo mara nyingi mtandao upo chini
POS za maxmalipo zinakumbwa na tatizo ambalo ni la muda mrefu, na limekua sugu la mtandao kua chini, hivyo mteja alienunua bidhaa hio kwa sababu ya kuzungusha pesa yake anapokumbwa na tatizo la mtandao siku nzima kisa hio siku kuna mawingu, au mtandao umekorofisha siku nzima sio haki, na uonevu kwa mteja na kampuni inatakiwa imlipe mteja kwa biashara aliopoteza kwa siku hio.
Kuvunja mkataba na mteja kuhusu umbali wa msambazaji mmoja na mwingine.
Mkataba kati ya mteja wa mashine na kampuni ni kwamba, kampuni haitamuuzia mtu mwingine mashine wa eneo jirani na biashara ya mteja wa kwanza ili kulinda maslahi ya mteja huyo(kumlinda na ushindani).kampuni haijatekeleza sharti hili la mkataba, na imekua ikiuza mashine bila kuzingatia hili, hivyo kuwafanya wateja wa mashine hizo walizonunua awali wakijua kua katika maeneo husika watakua ndio watoa huduma pekee, kupatwa na hali ya simanzi na kuhisi kutapeliwa.
Kufukuza wafanyakazi bila kufata taratibu
Wafanyakazi wa kampuni hii hawajaandikishwa kwenye vyama vya wafanyakazi, na hivyo kuna uonevu mkubwa kwa wafanyakazi, na uchunguzi ukifanyika utabaini ubabe na kufukuzwa kazi kwa wafanyakazi wengi pasipo kufata taratibu za wafanyazi (Tanzania Labor Laws)