Mawazo ya mama

cold water

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2021
Posts
323
Reaction score
1,128
Aisee kuna dada yangu mtoto wa mjomba ana watoto Wana akili Sana mmoja alivyomaliza kidato Cha nne alipata two, mwingine alipata one na advance wamefanya vizuri tu, mmoja amemaliza chuo, mwingine amemaliza form six lakini amekosa mkopo. Nimemtafutia shule fulani hivi ya msingi anafundisha watoto (kujitolea tu)

Issue ni kwamba huyo dada ambaye ni binamu yangu maisha yake ni magumu sana, na ni single mother na kila mtoto baba yake. Mmoja kati ya hao wawili alikataliwa na baba yake tangu akiwa mdogo, Sasa nimemsaidia kutafuta kazi kwa ajili ya watoto wake na wote wawili wamepata lakini kila nikimshirikisha mama yangu wala hana furaha haoneshi kufurahia.

Nikamwambia mama namtafutia mtoto wa dada kazi ni binamu lakini namwita tu dada Yani haonyeshi furaha kabisa🥲🥲🥲
 
Hivi kuna watu huwa hamna akili za kujitegemea wala kujiongoza??? Huku mara umemshirikisha mama huku mara umeshirikisha wana JF, ni muda gani unatumia akili yako binafsi kutatua hata masuala madogo madogo kama haya??!!
 
kama uliamua kusaidia ungepiga kimya umemweleza mama yako akupe jibu gan sasa?
 
Kwa hiyo anafurahia anavyoteseka 😂😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…