Mawaziri wengi wapya ni majeruhi

AMARIDONG

JF-Expert Member
Jun 24, 2010
2,502
180
BARAZA la Mawaziri 50 lililotangazwa na Rais Jakaya Kikwete Jumatano wiki hii limebeba idadi kubwa ya mawaziri wengi walio na majeraha makubwa ya kisiasa, kiuongozi, kimaadili na kitaaluma, Tanzania Daima limebaini.

Udadisi uliofanywa na gazeti hili kwa kuangalia rekodi za utendaji wa mawaziri hao hususan wale ambao wamerejeshwa kutoka katika baraza la mawaziri lililopita unaonyesha kwamba ni mawaziri wachache ambao utendaji na rekodi zao zinaweza kubeba taswira ya kutukuka na isiyo na doa.

Mbali ya rekodi hizo, uchambuzi wa kina wa gazeti hili unaonyesha kwamba, baadhi ya mawaziri wanaounda baraza hilo ni watu wanaotajwa kuwa vinara wa siasa za makundi, kuhasimiana, kichimvi na fitina ambazo kwa kiwango kikubwa ndizo zilizoigawa serikali iliyopita na Chama cha Mapinduzi (CCM) wanachotoka.
Dk. Shukuru Kawambwa

Taarifa ambazo gazeti hili limezipata zinaeleza kuwa miongoni mwa mawaziri ambao rekodi zao za utendaji zimekuwa ni za kutia shaka ni pamoja na Dk. Shukuru Kawambwa ambaye katika baraza jipya litakaloapishwa leo anakuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

Shaka kutokana na utendaji wa kazi wa Kawambwa unatokana na ukweli kwamba, katika kipindi chote cha miaka mitano alichokuwa waziri amekuwa ni majeruhi wa kuhamishwa wizara kila yanapofanyika mabadiliko.

Kwa sababu hiyo basi katika kipindi cha miaka mitano alichokuwa serikalini, Kawambwa ambaye ni mbunge wa Bagamoyo anakotoka Rais Kikwete amepata kuwa Waziri wa Maji, Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Waziri wa Miundombinu kwa vipindi tofauti.

Mary Nagu

Kama ilivyo kwa Kawambwa waziri mwingine ambaye katika kipindi chote cha miaka mitano amekuwa akihamishwa kutoka wizara moja kwenda nyingine ni Mary Nagu ambaye kwa sasa ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji).

Kabla ya kushika wadhifa huo mpya tena katika wizara inayoundwa kwa mara ya kwanza, Nagu amepata kuwa Waziri wa Sheria na Katiba kabla ya kuhamishiwa kwenda kuwa Waziri wa Viwanda Biashara na Masoko katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Akiwa Waziri wa Sheria na Katiba, Nagu, ndiye aliyekuwa mhanga wa kwanza wa msuguano mkubwa ulioibuliwa na hoja ya kuundwa kwa Mahakama ya Kadhi iliyokuwa imejumuishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005.

Prof. Jumanne Maghembe

Waziri mwingine aliyekalia kuti kavu ni Jumanne Maghembe ambaye katika baraza la sasa ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika wizara ambayo katika kipindi cha miaka mitano imeshuhudia kuhamahama kwa mawaziri wake wengi.

Kabla ya kutua katika wizara hiyo, Maghembe alikuwa ni Waziri wa Elimu, wizara ambaye alimalizia ngwe ya kwanza ya Rais Kikwete baada ya kupata kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii na baadaye Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana kwa vipindi tofauti.

Mustafa Mkulo

Wengine ambao pia wanaingia katika kundi la utendaji wao kuzusha maswali na mashaka ni Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, ambaye kwa baadhi ya watu anatajwa kuwa mmoja wa mawaziri katika baraza lililopita waliopwaya.

Mkulo ambaye baadhi ya taarifa zinamtaja kushindwa kumudu vyema nafasi yake hiyo hata kusababisha baadhi ya watendaji wa taasisi za kimataifa za fedha na uchumi kutilia shaka uwezo wake ni mmoja miongoni mwa mawaziri wachache waliobakia katika nyadhifa zao za awali.

Celina Kombani

Mbali ya Mkulo katika orodha ya mawaziri ambao uwezo wao unatiliwa shaka wamo pia Celina Kombani aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Katiba na Sheria akihama kutoka TAMISEMI ambako hajaacha urithi wowote wa kukumbukwa zaidi ya kuvurugwa kwa uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika mwaka juzi.

Uamuzi wa Kikwete kumteua kushika wadhifa huo wakati huu wa vuguvugu kubwa la mabadiliko ya sheria nyingi na Katiba huku akiwa na rekodi isiyovutia TAMISEMI ni moja ya ufa mkubwa katika baraza la mawaziri ambalo litaapishwa leo.

Hussein Mwinyi

Waziri mwingine ambaye utendaji wake unaacha maswali na kuzusha mashaka ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Hussein Mwinyi, anayeendelea kubakia katika wizara aliyokuwa akiingoza.

Upole, ukimya wake na utulivu ni mambo ambayo kwa baadhi ya wanajeshi wamekuwa wakiyaona kuwa udhaifu wa kiuongozi kwa waziri ambaye anabeba dhamana ya kuongoza majeshi ya ulinzi. Hata hivyo uadilifu na tabia yake ya kutopenda makuu inatajwa na baadhi ya watu kuwa silaha kubwa inayoweza kumuweka katika nafasi nzuri kikazi kuliko ilivyo kwa mwingine yeyote.

Ukiacha jeraha kubwa la utendaji la mawaziri hao, kundi jingine la mawaziri majeruhi ni lile linalojumuisha mawaziri ambao nyuma ya pazia wanaonekana kubeba ajenda ya mgawanyiko wa kimakundi ndani ya serikali na ndani ya CCM.

Bernard Membe

Majeruhi wa kwanza miongoni mwa mawaziri hao yuko, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, mwanasiasa ambaye ni miongoni mwa mawaziri wachache waliofanikiwa kubakia katika wizara ambazo walikuwa wakiziongoza katika kipindi kilichopita.

Ingawa Membe anaonekana kumridhisha Rais Kikwete kiutendaji, anatajwa kuwa mmoja wa wanasiasa ambao kwa kiwango kikubwa wamekuwa nyuma ya mpasuko mkubwa wa kimakundi ndani ya CCM na serikalini.

Membe ambaye amekuwa karibu na Kikwete kwa miaka mingi tangu wakiwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam miaka ya 1970 anatajwa kuwa ndiye mwanasiasa aliyechangia kwa kiwango kikubwa kuvunjika kwa ‘ndoa ya urafiki wa kimtandao’ kati ya Rais Kikwete na wanasiasa wengine kama Rostam Aziz na Edward Lowassa.

Wachambuzi wa siasa za ndani ya CCM wanasema ingawa, Samuel Sitta, ndiye aliyekuwa akitajwa zaidi kuwa kinara wa kundi la makamanda wa ufisadi ndani ya Bunge hata yeye na Lowassa kusababisha kuundwa kwa Kamati ya Mzee Mwinyi kuwasuluhisha wanasiasa hao wawili (Sitta na Lowassa), ukweli ni kwamba, Membe ndiye anayetajwa kuwa mpinzani mkubwa wa kundi linalomuunga mkono Lowassa kuliko ilivyo kwa Sitta.

Muonekano huo wa mambo ambao baadhi ya wadadisi wa mambo wanauhusisha na siasa za urais wa 2015, unawafanya baadhi ya watu kumtaja Membe kuwa kinara wa siasa za kihasama na kimakundi ambazo zimekuwa zikimpa shida kubwa Rais Kikwete kuiongoza CCM na serikali yake.

Ni kwa sababu hiyo basi, hatua ya Kikwete kumrejesha Membe katika wizara ile ile kwa watu wenye mtazamo wa namna hiyo ilionekana kuwa ni pigo kubwa kwa maadui zake na ushindi kwa timu inayopambana kuhakikisha zama za uvuli wa nguvu kubwa za chini kwa chini za kundi la Lowassa na Rostam zinafikia kikomo serikalini na ndani ya CCM.

Wengine wanaotajwa kuwa majeruhi wa siasa hizo za kimakundi ambazo asili yake ni kundi la mtandao lililomwingiza madarakani Rais Kikwete ni Stephen Wassira aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu na Naibu Waziri wa Kazi na Ajira Makongoro Mahanga.

Mbali ya majeraha hayo, uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima umebaini pia kwamba, kundi jingine la mawaziri ni wale ambao wanatarajia kuapishwa leo huku wakizongwa kwa kuwa na rekodi za kuwa na vyeti vya kitaaluma vyenye kutiliwa shaka.
Miongoni mwa mawaziri hao ambao shahada zao za udaktari wa falsafa ziliibua msuguano mkubwa ambao pengine ndiyo uliosababisha hata Rais Kikwete alazimike kuondoa sifa ya udaktari kwenye orodha ya majina yao wakati wa uteuzi ni pamoja na Emmanuel Nchimbi ambaye anakuwa Waziri wa Habari, Michezo na Vijana na Mahanga.

Mbali ya hao wako pia Dk. Nagu, William Lukuvi, Dk. Mathayo David Mathayo aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ambaye hata hivyo yeye alifanikiwa kusafisha rekodi yake siku chache baada ya elimu yake kutiwa msukosuko.

Ukiacha hilo, jeraha jingine kubwa wanaloingia nalo mawaziri wengine wa Kikwete ni lile linalotokana na matokeo ya uchaguzi mkuu yaliyowapa ushindi katika majimbo yao.

Miongoni mwa wale walio katika kundi hili ambao kwa wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaingia katika kundi la wanasiasa ambao ushindi wao unatajwa kuwa ulipatikana kwa njia ya uchakachuaji kura wamo Mahanga na Kapteni George Mkuchika aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Katika tuhuma hizo, Mahanga ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Segerea (CCM) amelalamikiwa mahakamani na aliyekuwa mpinzani wake, Fred Mpendazoe aliyegombea kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Kwa upande wake, Mkuchika ambaye ni Mbunge wa Newala, mbali ya matokeo yake kuzusha gumzo na maswali mengi hakuna taarifa kwamba yamepingwa mahakamani. Hata hivyo akizungumza na Gazeti hili juzi, Mahanga alisema wanaobeza uteuzi wake wamejikita kwenye propaganda za kisiasa zaidi badala ya kuangalia uwezo wake kiutendaji.
 
BARAZA la Mawaziri 50 lililotangazwa na Rais Jakaya Kikwete Jumatano wiki hii limebeba idadi kubwa ya mawaziri wengi walio na majeraha makubwa ya kisiasa, kiuongozi, kimaadili na kitaaluma, Tanzania Daima limebaini.

Udadisi uliofanywa na gazeti hili kwa kuangalia rekodi za utendaji wa mawaziri hao hususan wale ambao wamerejeshwa kutoka katika baraza la mawaziri lililopita unaonyesha kwamba ni mawaziri wachache ambao utendaji na rekodi zao zinaweza kubeba taswira ya kutukuka na isiyo na doa.

Mbali ya rekodi hizo, uchambuzi wa kina wa gazeti hili unaonyesha kwamba, baadhi ya mawaziri wanaounda baraza hilo ni watu wanaotajwa kuwa vinara wa siasa za makundi, kuhasimiana, kichimvi na fitina ambazo kwa kiwango kikubwa ndizo zilizoigawa serikali iliyopita na Chama cha Mapinduzi (CCM) wanachotoka.
Dk. Shukuru Kawambwa

Taarifa ambazo gazeti hili limezipata zinaeleza kuwa miongoni mwa mawaziri ambao rekodi zao za utendaji zimekuwa ni za kutia shaka ni pamoja na Dk. Shukuru Kawambwa ambaye katika baraza jipya litakaloapishwa leo anakuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

Shaka kutokana na utendaji wa kazi wa Kawambwa unatokana na ukweli kwamba, katika kipindi chote cha miaka mitano alichokuwa waziri amekuwa ni majeruhi wa kuhamishwa wizara kila yanapofanyika mabadiliko.

Kwa sababu hiyo basi katika kipindi cha miaka mitano alichokuwa serikalini, Kawambwa ambaye ni mbunge wa Bagamoyo anakotoka Rais Kikwete amepata kuwa Waziri wa Maji, Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Waziri wa Miundombinu kwa vipindi tofauti.

Mary Nagu

Kama ilivyo kwa Kawambwa waziri mwingine ambaye katika kipindi chote cha miaka mitano amekuwa akihamishwa kutoka wizara moja kwenda nyingine ni Mary Nagu ambaye kwa sasa ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji).

Kabla ya kushika wadhifa huo mpya tena katika wizara inayoundwa kwa mara ya kwanza, Nagu amepata kuwa Waziri wa Sheria na Katiba kabla ya kuhamishiwa kwenda kuwa Waziri wa Viwanda Biashara na Masoko katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Akiwa Waziri wa Sheria na Katiba, Nagu, ndiye aliyekuwa mhanga wa kwanza wa msuguano mkubwa ulioibuliwa na hoja ya kuundwa kwa Mahakama ya Kadhi iliyokuwa imejumuishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005.

Prof. Jumanne Maghembe

Waziri mwingine aliyekalia kuti kavu ni Jumanne Maghembe ambaye katika baraza la sasa ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika wizara ambayo katika kipindi cha miaka mitano imeshuhudia kuhamahama kwa mawaziri wake wengi.

Kabla ya kutua katika wizara hiyo, Maghembe alikuwa ni Waziri wa Elimu, wizara ambaye alimalizia ngwe ya kwanza ya Rais Kikwete baada ya kupata kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii na baadaye Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana kwa vipindi tofauti.

Mustafa Mkulo

Wengine ambao pia wanaingia katika kundi la utendaji wao kuzusha maswali na mashaka ni Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, ambaye kwa baadhi ya watu anatajwa kuwa mmoja wa mawaziri katika baraza lililopita waliopwaya.

Mkulo ambaye baadhi ya taarifa zinamtaja kushindwa kumudu vyema nafasi yake hiyo hata kusababisha baadhi ya watendaji wa taasisi za kimataifa za fedha na uchumi kutilia shaka uwezo wake ni mmoja miongoni mwa mawaziri wachache waliobakia katika nyadhifa zao za awali.

Celina Kombani

Mbali ya Mkulo katika orodha ya mawaziri ambao uwezo wao unatiliwa shaka wamo pia Celina Kombani aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Katiba na Sheria akihama kutoka TAMISEMI ambako hajaacha urithi wowote wa kukumbukwa zaidi ya kuvurugwa kwa uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika mwaka juzi.

Uamuzi wa Kikwete kumteua kushika wadhifa huo wakati huu wa vuguvugu kubwa la mabadiliko ya sheria nyingi na Katiba huku akiwa na rekodi isiyovutia TAMISEMI ni moja ya ufa mkubwa katika baraza la mawaziri ambalo litaapishwa leo.

Hussein Mwinyi

Waziri mwingine ambaye utendaji wake unaacha maswali na kuzusha mashaka ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Hussein Mwinyi, anayeendelea kubakia katika wizara aliyokuwa akiingoza.

Upole, ukimya wake na utulivu ni mambo ambayo kwa baadhi ya wanajeshi wamekuwa wakiyaona kuwa udhaifu wa kiuongozi kwa waziri ambaye anabeba dhamana ya kuongoza majeshi ya ulinzi. Hata hivyo uadilifu na tabia yake ya kutopenda makuu inatajwa na baadhi ya watu kuwa silaha kubwa inayoweza kumuweka katika nafasi nzuri kikazi kuliko ilivyo kwa mwingine yeyote.

Ukiacha jeraha kubwa la utendaji la mawaziri hao, kundi jingine la mawaziri majeruhi ni lile linalojumuisha mawaziri ambao nyuma ya pazia wanaonekana kubeba ajenda ya mgawanyiko wa kimakundi ndani ya serikali na ndani ya CCM.

Bernard Membe

Majeruhi wa kwanza miongoni mwa mawaziri hao yuko, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, mwanasiasa ambaye ni miongoni mwa mawaziri wachache waliofanikiwa kubakia katika wizara ambazo walikuwa wakiziongoza katika kipindi kilichopita.

Ingawa Membe anaonekana kumridhisha Rais Kikwete kiutendaji, anatajwa kuwa mmoja wa wanasiasa ambao kwa kiwango kikubwa wamekuwa nyuma ya mpasuko mkubwa wa kimakundi ndani ya CCM na serikalini.

Membe ambaye amekuwa karibu na Kikwete kwa miaka mingi tangu wakiwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam miaka ya 1970 anatajwa kuwa ndiye mwanasiasa aliyechangia kwa kiwango kikubwa kuvunjika kwa ‘ndoa ya urafiki wa kimtandao' kati ya Rais Kikwete na wanasiasa wengine kama Rostam Aziz na Edward Lowassa.

Wachambuzi wa siasa za ndani ya CCM wanasema ingawa, Samuel Sitta, ndiye aliyekuwa akitajwa zaidi kuwa kinara wa kundi la makamanda wa ufisadi ndani ya Bunge hata yeye na Lowassa kusababisha kuundwa kwa Kamati ya Mzee Mwinyi kuwasuluhisha wanasiasa hao wawili (Sitta na Lowassa), ukweli ni kwamba, Membe ndiye anayetajwa kuwa mpinzani mkubwa wa kundi linalomuunga mkono Lowassa kuliko ilivyo kwa Sitta.

Muonekano huo wa mambo ambao baadhi ya wadadisi wa mambo wanauhusisha na siasa za urais wa 2015, unawafanya baadhi ya watu kumtaja Membe kuwa kinara wa siasa za kihasama na kimakundi ambazo zimekuwa zikimpa shida kubwa Rais Kikwete kuiongoza CCM na serikali yake.

Ni kwa sababu hiyo basi, hatua ya Kikwete kumrejesha Membe katika wizara ile ile kwa watu wenye mtazamo wa namna hiyo ilionekana kuwa ni pigo kubwa kwa maadui zake na ushindi kwa timu inayopambana kuhakikisha zama za uvuli wa nguvu kubwa za chini kwa chini za kundi la Lowassa na Rostam zinafikia kikomo serikalini na ndani ya CCM.

Wengine wanaotajwa kuwa majeruhi wa siasa hizo za kimakundi ambazo asili yake ni kundi la mtandao lililomwingiza madarakani Rais Kikwete ni Stephen Wassira aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu na Naibu Waziri wa Kazi na Ajira Makongoro Mahanga.

Mbali ya majeraha hayo, uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima umebaini pia kwamba, kundi jingine la mawaziri ni wale ambao wanatarajia kuapishwa leo huku wakizongwa kwa kuwa na rekodi za kuwa na vyeti vya kitaaluma vyenye kutiliwa shaka.
Miongoni mwa mawaziri hao ambao shahada zao za udaktari wa falsafa ziliibua msuguano mkubwa ambao pengine ndiyo uliosababisha hata Rais Kikwete alazimike kuondoa sifa ya udaktari kwenye orodha ya majina yao wakati wa uteuzi ni pamoja na Emmanuel Nchimbi ambaye anakuwa Waziri wa Habari, Michezo na Vijana na Mahanga.

Mbali ya hao wako pia Dk. Nagu, William Lukuvi, Dk. Mathayo David Mathayo aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ambaye hata hivyo yeye alifanikiwa kusafisha rekodi yake siku chache baada ya elimu yake kutiwa msukosuko.

Ukiacha hilo, jeraha jingine kubwa wanaloingia nalo mawaziri wengine wa Kikwete ni lile linalotokana na matokeo ya uchaguzi mkuu yaliyowapa ushindi katika majimbo yao.

Miongoni mwa wale walio katika kundi hili ambao kwa wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaingia katika kundi la wanasiasa ambao ushindi wao unatajwa kuwa ulipatikana kwa njia ya uchakachuaji kura wamo Mahanga na Kapteni George Mkuchika aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Katika tuhuma hizo, Mahanga ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Segerea (CCM) amelalamikiwa mahakamani na aliyekuwa mpinzani wake, Fred Mpendazoe aliyegombea kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Kwa upande wake, Mkuchika ambaye ni Mbunge wa Newala, mbali ya matokeo yake kuzusha gumzo na maswali mengi hakuna taarifa kwamba yamepingwa mahakamani. Hata hivyo akizungumza na Gazeti hili juzi, Mahanga alisema wanaobeza uteuzi wake wamejikita kwenye propaganda za kisiasa zaidi badala ya kuangalia uwezo wake kiutendaji.

sahihi
 
Cha ajabu hapo nini,mbona rais mwenyewe majeruhi.Kwa kifupi timu nzima majeruhi sasa sijui performance hapo itakuwaje.
 
BARAZA la Mawaziri 50 lililotangazwa na Rais Jakaya Kikwete Jumatano wiki hii limebeba idadi kubwa ya mawaziri wengi walio na majeraha makubwa ya kisiasa, kiuongozi, kimaadili na kitaaluma, Tanzania Daima limebaini.

Udadisi uliofanywa na gazeti hili kwa kuangalia rekodi za utendaji wa mawaziri hao hususan wale ambao wamerejeshwa kutoka katika baraza la mawaziri lililopita unaonyesha kwamba ni mawaziri wachache ambao utendaji na rekodi zao zinaweza kubeba taswira ya kutukuka na isiyo na doa.

Mbali ya rekodi hizo, uchambuzi wa kina wa gazeti hili unaonyesha kwamba, baadhi ya mawaziri wanaounda baraza hilo ni watu wanaotajwa kuwa vinara wa siasa za makundi, kuhasimiana, kichimvi na fitina ambazo kwa kiwango kikubwa ndizo zilizoigawa serikali iliyopita na Chama cha Mapinduzi (CCM) wanachotoka.
Dk. Shukuru Kawambwa

Taarifa ambazo gazeti hili limezipata zinaeleza kuwa miongoni mwa mawaziri ambao rekodi zao za utendaji zimekuwa ni za kutia shaka ni pamoja na Dk. Shukuru Kawambwa ambaye katika baraza jipya litakaloapishwa leo anakuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

Shaka kutokana na utendaji wa kazi wa Kawambwa unatokana na ukweli kwamba, katika kipindi chote cha miaka mitano alichokuwa waziri amekuwa ni majeruhi wa kuhamishwa wizara kila yanapofanyika mabadiliko.

Kwa sababu hiyo basi katika kipindi cha miaka mitano alichokuwa serikalini, Kawambwa ambaye ni mbunge wa Bagamoyo anakotoka Rais Kikwete amepata kuwa Waziri wa Maji, Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Waziri wa Miundombinu kwa vipindi tofauti.

Mary Nagu

Kama ilivyo kwa Kawambwa waziri mwingine ambaye katika kipindi chote cha miaka mitano amekuwa akihamishwa kutoka wizara moja kwenda nyingine ni Mary Nagu ambaye kwa sasa ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji).

Kabla ya kushika wadhifa huo mpya tena katika wizara inayoundwa kwa mara ya kwanza, Nagu amepata kuwa Waziri wa Sheria na Katiba kabla ya kuhamishiwa kwenda kuwa Waziri wa Viwanda Biashara na Masoko katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Akiwa Waziri wa Sheria na Katiba, Nagu, ndiye aliyekuwa mhanga wa kwanza wa msuguano mkubwa ulioibuliwa na hoja ya kuundwa kwa Mahakama ya Kadhi iliyokuwa imejumuishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005.

Prof. Jumanne Maghembe

Waziri mwingine aliyekalia kuti kavu ni Jumanne Maghembe ambaye katika baraza la sasa ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika wizara ambayo katika kipindi cha miaka mitano imeshuhudia kuhamahama kwa mawaziri wake wengi.

Kabla ya kutua katika wizara hiyo, Maghembe alikuwa ni Waziri wa Elimu, wizara ambaye alimalizia ngwe ya kwanza ya Rais Kikwete baada ya kupata kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii na baadaye Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana kwa vipindi tofauti.

Mustafa Mkulo

Wengine ambao pia wanaingia katika kundi la utendaji wao kuzusha maswali na mashaka ni Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, ambaye kwa baadhi ya watu anatajwa kuwa mmoja wa mawaziri katika baraza lililopita waliopwaya.

Mkulo ambaye baadhi ya taarifa zinamtaja kushindwa kumudu vyema nafasi yake hiyo hata kusababisha baadhi ya watendaji wa taasisi za kimataifa za fedha na uchumi kutilia shaka uwezo wake ni mmoja miongoni mwa mawaziri wachache waliobakia katika nyadhifa zao za awali.

Celina Kombani

Mbali ya Mkulo katika orodha ya mawaziri ambao uwezo wao unatiliwa shaka wamo pia Celina Kombani aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Katiba na Sheria akihama kutoka TAMISEMI ambako hajaacha urithi wowote wa kukumbukwa zaidi ya kuvurugwa kwa uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika mwaka juzi.

Uamuzi wa Kikwete kumteua kushika wadhifa huo wakati huu wa vuguvugu kubwa la mabadiliko ya sheria nyingi na Katiba huku akiwa na rekodi isiyovutia TAMISEMI ni moja ya ufa mkubwa katika baraza la mawaziri ambalo litaapishwa leo.

Hussein Mwinyi

Waziri mwingine ambaye utendaji wake unaacha maswali na kuzusha mashaka ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Hussein Mwinyi, anayeendelea kubakia katika wizara aliyokuwa akiingoza.

Upole, ukimya wake na utulivu ni mambo ambayo kwa baadhi ya wanajeshi wamekuwa wakiyaona kuwa udhaifu wa kiuongozi kwa waziri ambaye anabeba dhamana ya kuongoza majeshi ya ulinzi. Hata hivyo uadilifu na tabia yake ya kutopenda makuu inatajwa na baadhi ya watu kuwa silaha kubwa inayoweza kumuweka katika nafasi nzuri kikazi kuliko ilivyo kwa mwingine yeyote.

Ukiacha jeraha kubwa la utendaji la mawaziri hao, kundi jingine la mawaziri majeruhi ni lile linalojumuisha mawaziri ambao nyuma ya pazia wanaonekana kubeba ajenda ya mgawanyiko wa kimakundi ndani ya serikali na ndani ya CCM.

Bernard Membe

Majeruhi wa kwanza miongoni mwa mawaziri hao yuko, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, mwanasiasa ambaye ni miongoni mwa mawaziri wachache waliofanikiwa kubakia katika wizara ambazo walikuwa wakiziongoza katika kipindi kilichopita.

Ingawa Membe anaonekana kumridhisha Rais Kikwete kiutendaji, anatajwa kuwa mmoja wa wanasiasa ambao kwa kiwango kikubwa wamekuwa nyuma ya mpasuko mkubwa wa kimakundi ndani ya CCM na serikalini.

Membe ambaye amekuwa karibu na Kikwete kwa miaka mingi tangu wakiwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam miaka ya 1970 anatajwa kuwa ndiye mwanasiasa aliyechangia kwa kiwango kikubwa kuvunjika kwa ‘ndoa ya urafiki wa kimtandao' kati ya Rais Kikwete na wanasiasa wengine kama Rostam Aziz na Edward Lowassa.

Wachambuzi wa siasa za ndani ya CCM wanasema ingawa, Samuel Sitta, ndiye aliyekuwa akitajwa zaidi kuwa kinara wa kundi la makamanda wa ufisadi ndani ya Bunge hata yeye na Lowassa kusababisha kuundwa kwa Kamati ya Mzee Mwinyi kuwasuluhisha wanasiasa hao wawili (Sitta na Lowassa), ukweli ni kwamba, Membe ndiye anayetajwa kuwa mpinzani mkubwa wa kundi linalomuunga mkono Lowassa kuliko ilivyo kwa Sitta.

Muonekano huo wa mambo ambao baadhi ya wadadisi wa mambo wanauhusisha na siasa za urais wa 2015, unawafanya baadhi ya watu kumtaja Membe kuwa kinara wa siasa za kihasama na kimakundi ambazo zimekuwa zikimpa shida kubwa Rais Kikwete kuiongoza CCM na serikali yake.

Ni kwa sababu hiyo basi, hatua ya Kikwete kumrejesha Membe katika wizara ile ile kwa watu wenye mtazamo wa namna hiyo ilionekana kuwa ni pigo kubwa kwa maadui zake na ushindi kwa timu inayopambana kuhakikisha zama za uvuli wa nguvu kubwa za chini kwa chini za kundi la Lowassa na Rostam zinafikia kikomo serikalini na ndani ya CCM.

Wengine wanaotajwa kuwa majeruhi wa siasa hizo za kimakundi ambazo asili yake ni kundi la mtandao lililomwingiza madarakani Rais Kikwete ni Stephen Wassira aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu na Naibu Waziri wa Kazi na Ajira Makongoro Mahanga.

Mbali ya majeraha hayo, uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima umebaini pia kwamba, kundi jingine la mawaziri ni wale ambao wanatarajia kuapishwa leo huku wakizongwa kwa kuwa na rekodi za kuwa na vyeti vya kitaaluma vyenye kutiliwa shaka.
Miongoni mwa mawaziri hao ambao shahada zao za udaktari wa falsafa ziliibua msuguano mkubwa ambao pengine ndiyo uliosababisha hata Rais Kikwete alazimike kuondoa sifa ya udaktari kwenye orodha ya majina yao wakati wa uteuzi ni pamoja na Emmanuel Nchimbi ambaye anakuwa Waziri wa Habari, Michezo na Vijana na Mahanga.

Mbali ya hao wako pia Dk. Nagu, William Lukuvi, Dk. Mathayo David Mathayo aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ambaye hata hivyo yeye alifanikiwa kusafisha rekodi yake siku chache baada ya elimu yake kutiwa msukosuko.

Ukiacha hilo, jeraha jingine kubwa wanaloingia nalo mawaziri wengine wa Kikwete ni lile linalotokana na matokeo ya uchaguzi mkuu yaliyowapa ushindi katika majimbo yao.

Miongoni mwa wale walio katika kundi hili ambao kwa wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaingia katika kundi la wanasiasa ambao ushindi wao unatajwa kuwa ulipatikana kwa njia ya uchakachuaji kura wamo Mahanga na Kapteni George Mkuchika aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Katika tuhuma hizo, Mahanga ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Segerea (CCM) amelalamikiwa mahakamani na aliyekuwa mpinzani wake, Fred Mpendazoe aliyegombea kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Kwa upande wake, Mkuchika ambaye ni Mbunge wa Newala, mbali ya matokeo yake kuzusha gumzo na maswali mengi hakuna taarifa kwamba yamepingwa mahakamani. Hata hivyo akizungumza na Gazeti hili juzi, Mahanga alisema wanaobeza uteuzi wake wamejikita kwenye propaganda za kisiasa zaidi badala ya kuangalia uwezo wake kiutendaji.

Kila waziri miongoni mwa hao uliowataja ana strength yake na mtu pekee anayefahamu strengths hizo ni jk basi.
 
BARAZA la Mawaziri 50 lililotangazwa na Rais Jakaya Kikwete Jumatano wiki hii limebeba idadi kubwa ya mawaziri wengi walio na majeraha makubwa ya kisiasa, kiuongozi, kimaadili na kitaaluma, Tanzania Daima limebaini.

Udadisi uliofanywa na gazeti hili kwa kuangalia rekodi za utendaji wa mawaziri hao hususan wale ambao wamerejeshwa kutoka katika baraza la mawaziri lililopita unaonyesha kwamba ni mawaziri wachache ambao utendaji na rekodi zao zinaweza kubeba taswira ya kutukuka na isiyo na doa.

Mbali ya rekodi hizo, uchambuzi wa kina wa gazeti hili unaonyesha kwamba, baadhi ya mawaziri wanaounda baraza hilo ni watu wanaotajwa kuwa vinara wa siasa za makundi, kuhasimiana, kichimvi na fitina ambazo kwa kiwango kikubwa ndizo zilizoigawa serikali iliyopita na Chama cha Mapinduzi (CCM) wanachotoka.
Dk. Shukuru Kawambwa

Taarifa ambazo gazeti hili limezipata zinaeleza kuwa miongoni mwa mawaziri ambao rekodi zao za utendaji zimekuwa ni za kutia shaka ni pamoja na Dk. Shukuru Kawambwa ambaye katika baraza jipya litakaloapishwa leo anakuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

Shaka kutokana na utendaji wa kazi wa Kawambwa unatokana na ukweli kwamba, katika kipindi chote cha miaka mitano alichokuwa waziri amekuwa ni majeruhi wa kuhamishwa wizara kila yanapofanyika mabadiliko.

Kwa sababu hiyo basi katika kipindi cha miaka mitano alichokuwa serikalini, Kawambwa ambaye ni mbunge wa Bagamoyo anakotoka Rais Kikwete amepata kuwa Waziri wa Maji, Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Waziri wa Miundombinu kwa vipindi tofauti.

Mary Nagu

Kama ilivyo kwa Kawambwa waziri mwingine ambaye katika kipindi chote cha miaka mitano amekuwa akihamishwa kutoka wizara moja kwenda nyingine ni Mary Nagu ambaye kwa sasa ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji).

Kabla ya kushika wadhifa huo mpya tena katika wizara inayoundwa kwa mara ya kwanza, Nagu amepata kuwa Waziri wa Sheria na Katiba kabla ya kuhamishiwa kwenda kuwa Waziri wa Viwanda Biashara na Masoko katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Akiwa Waziri wa Sheria na Katiba, Nagu, ndiye aliyekuwa mhanga wa kwanza wa msuguano mkubwa ulioibuliwa na hoja ya kuundwa kwa Mahakama ya Kadhi iliyokuwa imejumuishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005.

Prof. Jumanne Maghembe

Waziri mwingine aliyekalia kuti kavu ni Jumanne Maghembe ambaye katika baraza la sasa ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika wizara ambayo katika kipindi cha miaka mitano imeshuhudia kuhamahama kwa mawaziri wake wengi.

Kabla ya kutua katika wizara hiyo, Maghembe alikuwa ni Waziri wa Elimu, wizara ambaye alimalizia ngwe ya kwanza ya Rais Kikwete baada ya kupata kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii na baadaye Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana kwa vipindi tofauti.

Mustafa Mkulo

Wengine ambao pia wanaingia katika kundi la utendaji wao kuzusha maswali na mashaka ni Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, ambaye kwa baadhi ya watu anatajwa kuwa mmoja wa mawaziri katika baraza lililopita waliopwaya.

Mkulo ambaye baadhi ya taarifa zinamtaja kushindwa kumudu vyema nafasi yake hiyo hata kusababisha baadhi ya watendaji wa taasisi za kimataifa za fedha na uchumi kutilia shaka uwezo wake ni mmoja miongoni mwa mawaziri wachache waliobakia katika nyadhifa zao za awali.

Celina Kombani

Mbali ya Mkulo katika orodha ya mawaziri ambao uwezo wao unatiliwa shaka wamo pia Celina Kombani aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Katiba na Sheria akihama kutoka TAMISEMI ambako hajaacha urithi wowote wa kukumbukwa zaidi ya kuvurugwa kwa uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika mwaka juzi.

Uamuzi wa Kikwete kumteua kushika wadhifa huo wakati huu wa vuguvugu kubwa la mabadiliko ya sheria nyingi na Katiba huku akiwa na rekodi isiyovutia TAMISEMI ni moja ya ufa mkubwa katika baraza la mawaziri ambalo litaapishwa leo.

Hussein Mwinyi

Waziri mwingine ambaye utendaji wake unaacha maswali na kuzusha mashaka ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Hussein Mwinyi, anayeendelea kubakia katika wizara aliyokuwa akiingoza.

Upole, ukimya wake na utulivu ni mambo ambayo kwa baadhi ya wanajeshi wamekuwa wakiyaona kuwa udhaifu wa kiuongozi kwa waziri ambaye anabeba dhamana ya kuongoza majeshi ya ulinzi. Hata hivyo uadilifu na tabia yake ya kutopenda makuu inatajwa na baadhi ya watu kuwa silaha kubwa inayoweza kumuweka katika nafasi nzuri kikazi kuliko ilivyo kwa mwingine yeyote.

Ukiacha jeraha kubwa la utendaji la mawaziri hao, kundi jingine la mawaziri majeruhi ni lile linalojumuisha mawaziri ambao nyuma ya pazia wanaonekana kubeba ajenda ya mgawanyiko wa kimakundi ndani ya serikali na ndani ya CCM.

Bernard Membe

Majeruhi wa kwanza miongoni mwa mawaziri hao yuko, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, mwanasiasa ambaye ni miongoni mwa mawaziri wachache waliofanikiwa kubakia katika wizara ambazo walikuwa wakiziongoza katika kipindi kilichopita.

Ingawa Membe anaonekana kumridhisha Rais Kikwete kiutendaji, anatajwa kuwa mmoja wa wanasiasa ambao kwa kiwango kikubwa wamekuwa nyuma ya mpasuko mkubwa wa kimakundi ndani ya CCM na serikalini.

Membe ambaye amekuwa karibu na Kikwete kwa miaka mingi tangu wakiwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam miaka ya 1970 anatajwa kuwa ndiye mwanasiasa aliyechangia kwa kiwango kikubwa kuvunjika kwa ‘ndoa ya urafiki wa kimtandao’ kati ya Rais Kikwete na wanasiasa wengine kama Rostam Aziz na Edward Lowassa.

Wachambuzi wa siasa za ndani ya CCM wanasema ingawa, Samuel Sitta, ndiye aliyekuwa akitajwa zaidi kuwa kinara wa kundi la makamanda wa ufisadi ndani ya Bunge hata yeye na Lowassa kusababisha kuundwa kwa Kamati ya Mzee Mwinyi kuwasuluhisha wanasiasa hao wawili (Sitta na Lowassa), ukweli ni kwamba, Membe ndiye anayetajwa kuwa mpinzani mkubwa wa kundi linalomuunga mkono Lowassa kuliko ilivyo kwa Sitta.

Muonekano huo wa mambo ambao baadhi ya wadadisi wa mambo wanauhusisha na siasa za urais wa 2015, unawafanya baadhi ya watu kumtaja Membe kuwa kinara wa siasa za kihasama na kimakundi ambazo zimekuwa zikimpa shida kubwa Rais Kikwete kuiongoza CCM na serikali yake.

Ni kwa sababu hiyo basi, hatua ya Kikwete kumrejesha Membe katika wizara ile ile kwa watu wenye mtazamo wa namna hiyo ilionekana kuwa ni pigo kubwa kwa maadui zake na ushindi kwa timu inayopambana kuhakikisha zama za uvuli wa nguvu kubwa za chini kwa chini za kundi la Lowassa na Rostam zinafikia kikomo serikalini na ndani ya CCM.

Wengine wanaotajwa kuwa majeruhi wa siasa hizo za kimakundi ambazo asili yake ni kundi la mtandao lililomwingiza madarakani Rais Kikwete ni Stephen Wassira aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu na Naibu Waziri wa Kazi na Ajira Makongoro Mahanga.

Mbali ya majeraha hayo, uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima umebaini pia kwamba, kundi jingine la mawaziri ni wale ambao wanatarajia kuapishwa leo huku wakizongwa kwa kuwa na rekodi za kuwa na vyeti vya kitaaluma vyenye kutiliwa shaka.
Miongoni mwa mawaziri hao ambao shahada zao za udaktari wa falsafa ziliibua msuguano mkubwa ambao pengine ndiyo uliosababisha hata Rais Kikwete alazimike kuondoa sifa ya udaktari kwenye orodha ya majina yao wakati wa uteuzi ni pamoja na Emmanuel Nchimbi ambaye anakuwa Waziri wa Habari, Michezo na Vijana na Mahanga.

Mbali ya hao wako pia Dk. Nagu, William Lukuvi, Dk. Mathayo David Mathayo aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ambaye hata hivyo yeye alifanikiwa kusafisha rekodi yake siku chache baada ya elimu yake kutiwa msukosuko.

Ukiacha hilo, jeraha jingine kubwa wanaloingia nalo mawaziri wengine wa Kikwete ni lile linalotokana na matokeo ya uchaguzi mkuu yaliyowapa ushindi katika majimbo yao.

Miongoni mwa wale walio katika kundi hili ambao kwa wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaingia katika kundi la wanasiasa ambao ushindi wao unatajwa kuwa ulipatikana kwa njia ya uchakachuaji kura wamo Mahanga na Kapteni George Mkuchika aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Katika tuhuma hizo, Mahanga ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Segerea (CCM) amelalamikiwa mahakamani na aliyekuwa mpinzani wake, Fred Mpendazoe aliyegombea kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Kwa upande wake, Mkuchika ambaye ni Mbunge wa Newala, mbali ya matokeo yake kuzusha gumzo na maswali mengi hakuna taarifa kwamba yamepingwa mahakamani. Hata hivyo akizungumza na Gazeti hili juzi, Mahanga alisema wanaobeza uteuzi wake wamejikita kwenye propaganda za kisiasa zaidi badala ya kuangalia uwezo wake kiutendaji.

Kila waziri miongoni mwa hao uliowataja ana strength yake na mtu pekee anayefahamu strengths hizo ni jk basi.
 
Back
Top Bottom