Mawaziri wa Serikali, kwanini utekelezaji wa bajeti kuu uko chini ya asilimia 50?

tatum

JF-Expert Member
Jan 16, 2018
5,786
4,490
Ukilisikiliza kila siku Bunge kutoka upande wa Mawaziri wakijibu maswali na hata Bajeti zao mipango ya wizara zao wanakuwa wanaongelea mikakati,mipango,ahadi kwa asilimia kubwa kuliko utekelezaji wa mambo ambayo yanafanyika au hata kukamilika utekelezaji wake.

Wakati wenzetu majirani wa Africa Mashariki wakieleza utekelezaji wa mipango yao na kuweka mambo hadharani sisi bado tunaongea sana maneno mengi sana na mipango mingi sana lakini kasi ya utekelezaji ni kwa mwendo wa konokono.

Kuna haja hata ku review mikutano ya Bunge kama ina tija hasa Mkutano wa Bajeti kukaa miezi mitatu huko ukisikiliza hotuba za Mawaziri ni muendelezo ule ule tu miaka yote...utekelezaji wa bajeti zilizopita unakuta uko chini ya 50% kiukweli sioni sababu ya kukaa muda wote wa siku 90 huko outcome ya kukaa huko ni chini ya 50%.
 
Hapo unakuta Mishahara minono na posho za wabunge hao zinalipwa na walipa kodi wa nchi hii

Wanachofanya hapo bungeni kwa zaidi ya miezi 3 ni kupiga tu story za vijiweni
 
Ndugu, kila mwezi Jiwe, Mtoto wa Dada na Katibu Mkuu Kiongozi ndio huwa wanajifungia kwenye kachumba pale Magogoni na kupanga matumizi ya Nchi..

Wizara hii ipewe hiki, hii isipewe, hii lipia Bombardier, hii peleka kwa fulani, hizi za Chato Airport nk nk wanapanga wao na SIO kama Bunge lilivyopanga.

Unategemea nini..?

Nini unasema Wizara hazijatimiza 50% utekelezaji wa Bajeti zao, Wizara ya Mifugo na Uvuvi haikupewa hata SENT TANO ya bajeti ya Maendeleo 2017/18.
 
35% iko chini 50% kwahiyo sentensi yangu iko sawa ...rudi kusoma hisabati tena.
Bajeti iliyopita ilitekelezwa kwa 34% , hii ni kwa mujibu wa bunge , sasa ni vema mkaweka kiwango halisi badala ya kuwapa sifa za bure , natambua kwamba kiwango hiki ni chini ya 50% lakini siyo 49%
 
Bajeti iliyopita ilitekelezwa kwa 34% , hii ni kwa mujibu wa bunge , sasa ni vema mkaweka kiwango halisi badala ya kuwapa sifa za bure , natambua kwamba kiwango hiki ni chini ya 50% lakini siyo 49%
ok powa nashukuru kwa kutambua hilo......diplomatic language....
 
Sidhani kama ipo wizara ambayo imetekeleza mipango yake kwa asilimia 50, hakuna! zote ni chini ya asilimia 35!
 
Sidhani kama ipo wizara ambayo imetekeleza mipango yake kwa asilimia 50, hakuna! zote ni chini ya asilimia 35!

Kuwa Na Malengo au mipango isiyokuwa Na uwezekano wa kutekeleza ni sawa na ndoto za mchana....

Nchi inapelekwa pelekwa tu. Ni matamko Na usanii wa kisiasa...
 
Back
Top Bottom