Maumivu ya ndoa Vs maumivu ya uchumba

Maumivu ya ndoa Vs maumivu ya uchumba

jungle boy

Senior Member
Joined
Aug 6, 2015
Posts
107
Reaction score
27
Habarini za weekend wandugu wapendwaaa?
Naomba tupanuane mawazo katika jambo hili.

Mara nyingi watu hutendwa katika mahusiano yaweza kuwa mahusiano ya mke na mume au ya mtu na mchumba wake.Mtu akitendwa katika hatua ya uchumba wengi wetu huumia saanaa na wakati mwingine hufikia hatua ya kumchukia aliyemtenda na wengine woote wa jinsia hiyo iliyomtenda, wakati mwingine maumivu huzid kipimo hali ambayo huleta majeraha ya moyo.

Utajikuta husikii hamu ya kula,,siku nzima hujanywa maji lakin hata kiu husikii kweli huumiza wengine huapa sitokuja kupenda tenaa na wengine kila wanapokumbuka walivyotendwa hujihis kububujikwa na machozi its so painful...

Sina maana kuwakumbusheni machungu mliyoyapata mimi nikiwa mmojawapo...

Katika hali hii ya uchumba wengi huvunjika moyo na hata kutotamani kuingia tena kwenye mahusiano.Lakini pia la kujiuliza hapa uyu nayemlilia ndie angenifaa hapo baadae asingenifanya nije nijute zaid katk ndoa?

Katika hali hii huwa hakuna kukumbuka maswali kama haya ni kwa sababu ya kuamin uyu ndie angekuwa wangu daima..Lakin ni jambo la maana pia kutafakari endapo uyu aliyenitenda hiv kama angenitenda ndani ya ndoa ingekuwa bora au ingekuwa maumiv plus.

Nisiwachoshe sana nirudi kwenye topic kutokana na maelezo hayo hapo juu.

Je nikipi huumiza zaidi kutendwa kwenye uchumba au kutendwa ndani ya ndoa?
Au maumiv ni yale yale.

Karibuni wana jamvi tulibabadue hili.
Naomba kuwasilisha.

Wenu Jungle boy
 
bora uchumba maaana unaweza badili uelekeo sasa km ni ndani ya ndoa unafanyaje ? maumivu mara mbili.
 
bora uchumba maana utakuwa huru kumchagua unayeona anafaa ila ukishaingia kwenye ndoa tayari ushaingia kwenye sheria
 
Bora upate maumivu kipindi cha uchumba kuliko cha ndoa.
Maana ndoa inakuwa tayari mmeingia kwenye sheria, hata kuachana itakuwa ni gharama. Hadi muende mahakamani.
 
Inategemea kwako uchumba ni stage ipi. Wengine "wakishakutana" tu wanaitana wachumba
 
Maumivu ya ndoa yanawaumiza wanandoa sana,ila hilo la uchumba vijana wengi wameshakuwa sugu,akitendwa na huyu siku hiyohiyo anahamia kwa mwingine.
 
Kumbe mapenzi yanavuruga wengi,ila uzuri ukishavurugwa unakuwa mkomavu Kisha unasonga.
 
Back
Top Bottom