Maumivu ya moyo

Maumivu ya moyo

mahirtwahir

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2013
Posts
614
Reaction score
322
Wenzangu natumaini hamujambo,

Ametukuka yule mbora wa kuumba aloumba ulimwengu na sisi tuliomo katika ulimwengu

Siku ya leo mwenzenu mungu kanipa mtihani mkubwa unyonge wangu nililimbikiza kwa muda wa zaidi ya mwaka na nusu hatuli vizuri wala kuvaa vizuri mimi na mke wangu na watoto ili tupate kijibanda angalau nisitirike na watoto wangu tu pamoja na mke wangu nguvu nyingi nilizozipoteza ni kweli nilifikia malengo na nikajenga nyumba ya vyumba vi 4.

Na ilikua imeshafikia kozi 8 nilikua nimeshakopa na kutafuta saruji nondo na kokoto na bati ili niweke vyumba viwili nikae na watoto maana nyumba ya kupanga nimeshapewa notes nihame.

Mungu si athumani leo imenyesha mvua nyumba yote imebebwa na maji hakuna jiwe lililokamatana na mwenzake hakuna tufali lililoshikana na mwenzake jitihada zangu ni bure nyumba haipo na shida ipo ni kweli wa moja ni wa moja tu.

INNA LILAHI WAINA ILAIHI RAJIUN
 
We Ni Mpumbafu.Huna Tofauti Na Abunuwasi.Unapotezaje Mda Wako Na Rasilimali Zako Kujenga Mabondeni?.
 
ukisikia matatizo ya mwenzako unajiona wewe ni afadhali
 
Pole sana mkuu ila tunajifunza kwa kuona i hope next time utakuwa makini kuchagua sehemu ya kujenga.
 
hahahahahaha nacheka huku machozi yananitoka uchungu moyoni kweli ni maumivu ya moyo
 
Mh! pole, kusema ni kuponde siwezi nikutetee siwezi, mh! pole sana
 
utajengaje mabondeni pole mabondeni tulime na kuachia chura na kenge nao wapate wapate sehemu ya kukaa na kuzaliana
 
Pole sana mkuu, ila shukuru Mungu janga limetokea mapema, je yangetokea wakati tayari umeshahamia na familia si ingekua majanga zaidi
 
Kwa waliojenga tu au wanaojenga tu ndo wanaweza kuelewa hisia zako hapa, plus wenye moyo wa utu...pole sana ndugu yangu na MUNGU akujaalie mbadala ulio bora zaidi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom