Maumivu ya mapenzi na msiba, yapi makali zaidi?

Maumivu ya mapenzi na msiba, yapi makali zaidi?

Mtanzanika

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2012
Posts
2,389
Reaction score
1,131
Mtu anapopatwa na maumivu ya mapenzi ama msiba ni kipi hasa humuuma kati ya roho na moyo?Maana utamsikia mtu akisema roho inaniuma sana au moyo unaniuma sana. Mimi nikijaribu kuyafikiria maumivu ya namna hiyo nashindwa kupata jibu sahihi kama kile kiumacho ni kipi kati ya hivyo viwili.

Thread ya namna hii nilipata kuisoma humu Jf lakini mleta mada hakuwa na dhana kama niliyokuwa nayo mimi.

Hivyo nimeona nipate mawazo kutoka kwenu wadau
 
Sijui moyo sijui roho yani hata sielewi aiseee maana maumivu ya mapenzi ni yakipekee
 
Maumivu ya mapenzi yanaisha...na ndio maana tunakuwa na ma ex...maumivu ya msiba kwa kweli kwangu mimi hayaishi...nikimfikiria tu mpendwa wangu nalia ..lkn mpenz siwezi kumlilia milele..nitalia mwanzoni tu ...
 
Wewe yani mtu aniache ndo nilie kama nimefiwa? Maumivu ya kufiwa hayaelezeki, mpenzi ataniacha ila ntapata mingine/wengine. Lakini mpendwa wangu aliyefariki sitokuwa naye wala kumuona tena milele.
 
Mtanzanika

Hivi kabla sijajibu ulichouliza nipate kujua kutoka kwako yafuatayo?
1. Umewahi kukutana na maumivu ya mapenzi wewe au huwa unasikia na kuona kwa majirani na mashost zako?
2. Je umewahi kufiwa kweli na mtu wa nguoni/ karibu jeneza linatokea chumbani kwako au sitting room kwako/ kwenu? Au huwa unasikia tu mtoto wa mjomba binamu kafa huko kijijini hata kumjua humjui?

Kweli kabisa kama umepitia hayo hapo juu usingekuja na swali hilo but nasikitika kwa bahati mbaya kabisa hakuna hata moja umepitia ndio maana una nafasi na raha ya kufananisha KIFO na USINGIZI

Mungu lakini si mchoyo nakuombea uzima ukishapitishwa kote huko utatupa majibu humu ukipata nguvu.

Maana kuna mwenzio mmoja aliomba msamaha wote aliowahi kuwaconfort walipopata msiba ilipofika zamu yake aliwaomba msamaha.

Haya Gudluck
 
Last edited by a moderator:
Maumivu ya msiba hayaelezeki yani ni maumivu ambayo unajua huwezi muona tena huyo mtu ila mapenzi nitaumia then nasonga mbele maana nothing last forever
 
Asante sana Nyakati umempatia jibu linalomfaa

Karibu!
Muache akafikiri kama "Great Thinker" akifikiri vyote vinahitaji watu waumize akili kufikiri hajui kama kuna vingine ni ubinadam zaidi.
Na ni ubinadam usiozuilika.
 
Upo serious mkuu??? Maumivu ya msiba Wa mtu wa karibu unayajua au unaskia tu story? moja kwa moja hujawah pitia situations ngumu za namna hyo ndio maana unaleta uzi km huu
 
maumivu ya msiba ni matokeo ya mapenz ulionayo kwa mhusika.
 
wee msiba zaidi kama ni mtu wa karibu, mpenzi inaumiza but ukipata mwingine tuu mambo byeeeee ila ndugu hata iweje wazaliwe wengapi alokufa utamkumbuka tuu
 
Nilifiwa na mpendwa wngu mwezi wa tatu lkn hd leo maumivu bado hayajaisha wala kupungua yaan bado sijapata nafuu moyoni kila siku naona.km vl amefariki jana. Anyway maumivu ya mapenzi yana unafuu zaidi kuliko ya kufiwa kwsbb mtu akifa hutamuona milele.
Wadau hapo juu wamekujibu vzr,subiri siku.ukipata msiba wa mtu anaekuhusu ndio utapata majibu mazuri.
 
Wenzako wanajiuliza maumivu ya kukatwa pale dodoma na kushindwa pale october yepi yanauma ?? Ww unaleta ujinga wako hapa soma alama za nyakati kama uko dar kawe foren ya kujiandikisha kachukue kichchio
 
Hivi kabla sijajibu ulichouliza nipate kujua kutoka kwako yafuatayo?
1. Umewahi kukutana na maumivu ya mapenzi wewe au huwa unasikia na kuona kwa majirani na mashost zako?
2. Je umewahi kufiwa kweli na mtu wa nguoni/ karibu jeneza linatokea chumbani kwako au sitting room kwako/ kwenu? Au huwa unasikia tu mtoto wa mjomba binamu kafa huko kijijini hata kumjua humjui?

Kweli kabisa kama umepitia hayo hapo juu usingekuja na swali hilo but nasikitika kwa bahati mbaya kabisa hakuna hata moja umepitia ndio maana una nafasi na raha ya kufananisha KIFO na USINGIZI

Mungu lakini si mchoyo nakuombea uzima ukishapitishwa kote huko utatupa majibu humu ukipata nguvu.

Maana kuna mwenzio mmoja aliomba msamaha wote aliowahi kuwaconfort walipopata msiba ilipofika zamu yake aliwaomba msamaha.

Haya Gudluck

1. Maumivu ya mapenzi nimewahi kukutana nayo kiasi.
2. Maumivu ya msiba nilikutana nayo vilevile, niliondokewa na mtu muhimu mno.
Kwa hiyo nimepita huko kote na maumivu niliyahisi. Haya maumivu ndiyo yamenipa maswali maana siwezi kusema kama moyo ndo ulokuwa ukiuma, ninachoweza kubaini tu ni kwamba maumivu hupelekea moyo kushtuka hivyo kupeleka damu kwa kasi, lakini napata shida kama kinachouma ni moyo kama moyo "that blood pumping organ", na pia natatizika kama yale maumivu niliyoyahisi ilikuwa ni roho ndo yenye kuuma.

Mimi sikuwa na nia mbaya kuuliza jambo hili, kama itakuwa nimetonesha watu vidonda naomba nisamehewe kwani mimi ni mwanadamu dhaifu.

Labda pengine kama kutakuwa na mtaalamu wa masuala ya kisayansi na kibaiolojia anisaidie katika hili ili nipate kuelewa kama kweli huu moyo unaosukuma damu unahusika na maumivu ya hisia?
Maana huenda ni mazoea yetu tu kusema kwamba roho inauma, moyo unauma lakini kumbe hivyo vitu haviwakilishi maumivu tunayoyasikia. Na vile vile kuna neno NAFSI, vipi nikisema nafsi ndo inayouma?
 
Maumivu ya msiba hayaelezeki yani ni maumivu ambayo unajua huwezi muona tena huyo mtu ila mapenzi nitaumia then nasonga mbele maana nothing last forever

Naomba nikuulize kwenye mapenzi...kitu gani unahisi ndo chenye kuuma unapopatwa na maumivu ya mapenzi, Moyo au Roho? Unawezaje kuhusisha maumivu hayo na kitu kimoja wapo kati ya hivyo viwili?
 
Maumivu ya msiba yanazidi maana yule mtu haumuoni teeena, lakini mapenzi unaweza kutana na mwingine na maisha yakaendelea,

Huwezi kuniambia machungu ya kufiwa baba angu yafanane na ya kuachwa na John No way
 
Back
Top Bottom