Ubavu
JF-Expert Member
- Jun 19, 2012
- 2,791
- 3,236
Nikiwa kama kijana niliyekulia Mwananyamala na kuishi wilaya ya Kinondoni, nimesikitishwa sana na kitendo cha kujiuzuru ndugu Maulid Said Mtulia kuwa Mbunge pamoja nafasi zake zote ndani ya chama cha CUF.
Sijashangaa kutokana na kitendo hicho hasa ukizingatia kwa jinsi upepo wa kisiasa unavyo vuma, kilichonipata naweza kukielezea kama kukata tamaa (disappointment) na kijana mwenzangu.
Wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, nakumbuka jinsi Mtulia alipopata shida kuyafikia masikio ya wanakinondoni kupitisha azma yake ya kuwawakilisha Bungeni, hasa ukizingatia kuwa alikuwa ni mpya kwenye macho ya wengi. Kwa juhudi kubwa tawi la KUNDUS Mwananyamala pamoja na Ofisi ya CUF wilaya zilisababisha kijana huyu kupata kutambulika na mwisho kuibuka kidedea!
Ni kweli usiopingika kuwa juhudi binafsi za bwana Mtulia zilisaidia yeye kupata ridhaa ya wananchi, lakini kwa asilimia kubwa (zaidi ya sabini) zilitokana na juhudi za wananchi hasa wakereketwa wa CUF na CHADEMA waliohamasisha watu wengi kujitokeza kupiga kura na mwisho walikesha usiku kucha kuzilinda kura zile ili zisiibiwe na CCM.
Chakushangaza baada ya kazi kubwa iliyozaa mafanikio makubwa ya Vijana wa UKAWA kuisambaratisha ngome ya CCM KINONDONI na kumuibua Mtulia kidiedea miaka miwili pekee imetosha kumsahaulisha bwana huyu NGUVU YA UMMA iliyomuweka pale alipo.
Sijui kama amenunuliwa au ni kwa mapenzi yake toka moyoni, ila ninachosema mimi ni kuwa MTULIA UMEPOTEA! Mtulia wewe uliyefungua kesi mahakamani ili kuzuia serikali ya rais Magufuli isivunje nyumba za watu masikini zilizopo maeneo ya Kinondoni Mkwajuni, leo hii unaungana na serikali ileile iliyosababisha majonzi na simanzi kwa wananchi hawa! SIJUI UTAWAANGALIA VIPI WANANCHI HAWA!
Ninachoweza kukwambia ndugu yangu Mtulia ni kuwa waliokuweka hapo ulipo ndio watakao kushusha. Mark my words Mr. Mtulia, mwaka 2020 usitegemee kurudi na kuwa mbunge wa Kinondoni kwani WANANCHI HATUTASAHAU!
Kama umeahidiwa kuwa utapatiwa jimbo la Kinondoni jua fika kuwa UMEONGOPEWA!
NGUVU ILIYOTUMIKA KUKUWEKA HAPO ULIPO NDIO NGUVU HIYOHIYO ITAKAYOTUMIKA KUKUTOA HAPO ULIPO!
Na Zuberi Mohamed Ubavu
Sijashangaa kutokana na kitendo hicho hasa ukizingatia kwa jinsi upepo wa kisiasa unavyo vuma, kilichonipata naweza kukielezea kama kukata tamaa (disappointment) na kijana mwenzangu.
Wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, nakumbuka jinsi Mtulia alipopata shida kuyafikia masikio ya wanakinondoni kupitisha azma yake ya kuwawakilisha Bungeni, hasa ukizingatia kuwa alikuwa ni mpya kwenye macho ya wengi. Kwa juhudi kubwa tawi la KUNDUS Mwananyamala pamoja na Ofisi ya CUF wilaya zilisababisha kijana huyu kupata kutambulika na mwisho kuibuka kidedea!
Ni kweli usiopingika kuwa juhudi binafsi za bwana Mtulia zilisaidia yeye kupata ridhaa ya wananchi, lakini kwa asilimia kubwa (zaidi ya sabini) zilitokana na juhudi za wananchi hasa wakereketwa wa CUF na CHADEMA waliohamasisha watu wengi kujitokeza kupiga kura na mwisho walikesha usiku kucha kuzilinda kura zile ili zisiibiwe na CCM.
Chakushangaza baada ya kazi kubwa iliyozaa mafanikio makubwa ya Vijana wa UKAWA kuisambaratisha ngome ya CCM KINONDONI na kumuibua Mtulia kidiedea miaka miwili pekee imetosha kumsahaulisha bwana huyu NGUVU YA UMMA iliyomuweka pale alipo.
Sijui kama amenunuliwa au ni kwa mapenzi yake toka moyoni, ila ninachosema mimi ni kuwa MTULIA UMEPOTEA! Mtulia wewe uliyefungua kesi mahakamani ili kuzuia serikali ya rais Magufuli isivunje nyumba za watu masikini zilizopo maeneo ya Kinondoni Mkwajuni, leo hii unaungana na serikali ileile iliyosababisha majonzi na simanzi kwa wananchi hawa! SIJUI UTAWAANGALIA VIPI WANANCHI HAWA!
Ninachoweza kukwambia ndugu yangu Mtulia ni kuwa waliokuweka hapo ulipo ndio watakao kushusha. Mark my words Mr. Mtulia, mwaka 2020 usitegemee kurudi na kuwa mbunge wa Kinondoni kwani WANANCHI HATUTASAHAU!
Kama umeahidiwa kuwa utapatiwa jimbo la Kinondoni jua fika kuwa UMEONGOPEWA!
NGUVU ILIYOTUMIKA KUKUWEKA HAPO ULIPO NDIO NGUVU HIYOHIYO ITAKAYOTUMIKA KUKUTOA HAPO ULIPO!
Na Zuberi Mohamed Ubavu