Mkuu Nyerere aliwabeba sana Watutsi (kwa sababu anazozijua yeye mwenyewe) hadi wakati ule wa Arusha peace negotiation alipowageuka. Nyerere hakutaka kuonekana mpuuzi mbele ya jamii ya kimataifa kwa kuwakumbatia Watutsi kwenye ujinga wao. Aliona kwamba alishawabeba kwa muda mrefu sasa iliwapasa wabadilike waukubali ukweli kwamba hawatatawala milele Burundi. Watutsi walipoona Nyerere amewageuka walimtukana eti ni k'kojoz!
Tangu uhuru Nyerere aliwabeba sana Watutsi.
Mwaka 1965 aliuawa waziri mkuu wa Burundi Pierre Ngendandumwe, Nyerere aka mute!
Mwaka 1972 mauaji ya kimbari yakafanyika dhidi ya Wahutu (wahutu laki 3 wengi wao wasomi waliuawa), UN ikataka kupeleka jeshi Burundi Nyerere akasema Warundi wasiingiliwe masuala yao ya ndani ya nchi.
Mwaka 1994 walipouawa maraisi Ntaryamira na Habyalimana kwa kutunguliwa ndege yao, kuna Watutsi kule Mwanza walifanya sherehe kushangilia. RPC alipowatia ndani Nyerere akamtaka awaweke huru akasema 'adui yako akifa huwezi kufurahi'?
Upo mkono wa Nyerere uliojificha nyuma ya nguvu za kiutawala za Watutsi kuanzia Uganda, Rwanda, Burundi na DRC.