Wickama
Platinum Member
- Mar 8, 2009
- 1,568
- 1,350
Wakuu, ndio kwanza narejea toka mikoa ya kanda ya ziwa kwa kupitia Kenya. Nilifuata barabara ya Tanga-Mombasa-Nairobi-Narok-Kisii-Tarime. Nilichojionea ni kama ifuatavyo;
NAULIZA KWA NINI HAPA BONGO HALI NI TOFAUTI?
- Matuta ya barabarani kwa upande wa Kenya ni machache sana. Kiasi kikubwa ni kuwa highway nzima inapitika bila matuta kasoro sehemu chache sana. Tena matuta yapo zaidi eneo la Kisii kwenye highway ya Sirari-Kisii kuelekea Kericho, sio kwenye highway ya Kisii-Narok.
- Mizani ya kupima magari uzito kwa njia nzima ipo Mombasa eneo jirani na Mariakani. Hii ina maana kwa kilometer zaidi ya 1000 ni mizani hii pekee niliyoiona.
- Magari ya abiria (mabasi) hayasimami mizani kupima uzito.
NAULIZA KWA NINI HAPA BONGO HALI NI TOFAUTI?