Hili Silo tunda la kunazi ni Tunda linaitwa kwa jina hili Plums halipo hapo nchini Tanzania hili Tunda Mkuu Totos Boss Matunda haya yanapatikana Uaraubi na ulaya Afrika hakuna hayo matunda.
Mkuu, matunda ulioweka hapo juu ni hayo niliyoyaorodhesha hapa chini ukifuatilia mstari mmoja baada ya mwengine. Mimi nilitembele na kuishi sehemu za Usambaa, Tanga na ndipo nilipokutana na haya matunda. Tunda namba 5 na 7 ndio unayoyakuta kwa wingi sokoni (Tanga au DSM). Haya mengine hayalimwi kwa wingi ili kufanya biashara lakini utaikuta miti yake kwenye nyumba za zamani za wakoloni - hasa wa kiJerumani.
Unajua, Tanzania kuna climatic zones zote zilizoko duniani. Unapotoka milimani (kama usambaani) na kuteremka kwenye tambarare utakutana na climate zones kutoka temperate hadi tropical. Ukienda Dodoma utakutana na hali ya jangwa na kuna matunda mazuri tu yanayopenda ukame yanajiotea porini na wenyewe hawayauzi sokoni. Nili-enjoy sana haya matunda nilipokuwa JKT Makutupora.
Matunda ulioweka hapo juu
1 Apricot---Apricoti (utakuta miti michache ya haya matunda kwenye nyumba za zamani za wakoloni usambaani)
2 Cherry----Cheri (micheri ipo usambaani lakini matunda yake mara nyingi yanaliwa na ndege. Kuna meupe/pink pia)
3 Fig--------Tini (haya yapo zaidi sehemu za Amani Tanga lakini sijayaona sokoni)
4 Kiwi-------Kiwi (haya utayakuta kati ya Amani na Muheza - Tanga.
5 Peach-----Pichi au fyoksi (wasambaa wanayaita mafyoksi - inashabihiana na jina lake kijerumani - Pfirsich)
6 Prune-----Pruni (hutumiwa kulainisha choo kama una constipation)
7 Plum------Plamu (matunda damu)
Hili Silo tunda la kunazi ni Tunda linaitwa kwa jina hili Plums halipo hapo nchini Tanzania hili Tunda Mkuu Totos Boss Matunda haya yanapatikana Uaraubi na ulaya Afrika hakuna hayo matunda.
Hili tunda tokea Niko mdogo. Nalitafuta jina lake nilijue. Hadi Leo hii bado sijalijua.
Linaitwa Kiwi fruit. Linapatikana sana New Zealand. Sina uhakika kama Tanzania yapo. Sijawahi kuyaona.
absolutely correct matunda yote uliyoyataja yanapatikana katika maeneo ya Tanga sana sana Lushoto ambako nafkiri kila aina ya tunda linalomea ULAYA basi na huko Lushoto utalipata
The kiwifruit or Chinese gooseberry (sometimes shortened to kiwi) is the edible berry of a woodyvine in the genus Actinidia.[SUP][1][/SUP][SUP][2][/SUP] The most common cultivar group of kiwifruit ('Hayward')[SUP][3][/SUP] is oval, about the size of a large hen's egg (5–8 cm (2.0–3.1 in) in length and 4.5–5.5 cm (1.8–2.2 in) in diameter). It has a fibrous, dull greenish-brown skin and bright green or golden flesh with rows of tiny, black, edible seeds. The fruit has a soft texture and a sweet but unique flavor, It is a commercial crop in several countries, such as Italy, New Zealand, Chile, Greece, and France.[SUP][4][/SUP]In New Zealand the word kiwi usually refers to the kiwi bird or the people of New Zealand, so it is seldom used to refer to the fruiLushoto kuna hali ya hewa nzuri, Nakuabaliana nawe kuwa kuna karibu kila tunda linalopatikana Ulaya
Nadhani yapo mengi mikoa ya nyanda za juu kusini. Hata pale nyumbani kwani nina miti nimeipanda.