Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,359
- 4,814
Ripoti mpya ya kila mwaka ya Shirika la Afya Duniani WHO kuhusu tumbaku, inaonesha matumizi ya tumbaku kwa wanaume yameanza kupungua kwa mara ya kwanza.
Kwa mujibu wa shirika hilo idadi ya wanawake wanaotumia tumbaku imepungua kwa takribani milioni 100 kati ya 2000 na 2018, na kwa wanaume imeongezeka kwa kiasi ya watu milioni 40.
Shirika hili linakadiria kuwa idadi hiyo ya wanaume itapungua kwa watu milioni 2 katika mwaka ujao, na milioni 6 zaidi itakapofikia 2025. Hata hivyo ripoti ya WHO inaonesha pia wanawake wanaweza kukabiliana na uraibu wa tumbaku haraka ikilinganishwa na wanaume.
Kwa ujumla shirika hilo limesema idadi ya watumiaji wa tumbaku umepungua kutoka bilioni 1.4 kwa mwaka 2000 hadi kufikia bilioni 1.3 kwa mwaka 2018.
Kwa mujibu wa shirika hilo idadi ya wanawake wanaotumia tumbaku imepungua kwa takribani milioni 100 kati ya 2000 na 2018, na kwa wanaume imeongezeka kwa kiasi ya watu milioni 40.
Shirika hili linakadiria kuwa idadi hiyo ya wanaume itapungua kwa watu milioni 2 katika mwaka ujao, na milioni 6 zaidi itakapofikia 2025. Hata hivyo ripoti ya WHO inaonesha pia wanawake wanaweza kukabiliana na uraibu wa tumbaku haraka ikilinganishwa na wanaume.
Kwa ujumla shirika hilo limesema idadi ya watumiaji wa tumbaku umepungua kutoka bilioni 1.4 kwa mwaka 2000 hadi kufikia bilioni 1.3 kwa mwaka 2018.
