Ntaramuka
Senior Member
- May 2, 2008
- 169
- 27
Kuna watu wengi ambao bado hutumia baadhi ya maneno ya kiswahili kimakosa. Leo nimeona kidogo nielekeze japo kwa ufupi usahihi wa matumizi ya baadhi ya maneno
1. Tafadhali sema, Huu ufunguo na siyo hii funguo
2. Huu wimbo na siyo hii nyimbo, ila hizi nyimbo (katika wingi).
3. Usiseme amesharudi kazini, kumaanisha kutoka kazini, sema, umeshatoka kazini au umesharudi kutoka kazini
4. Usiseme, alikuja siku ya Jumapili, sema alikuja Jumapili, kwa sababu inajulikana Jumapili ni siku.
5. Usiseme shati jingine, sema shati lingine.
Naomba kuwasilisha.
1. Tafadhali sema, Huu ufunguo na siyo hii funguo
2. Huu wimbo na siyo hii nyimbo, ila hizi nyimbo (katika wingi).
3. Usiseme amesharudi kazini, kumaanisha kutoka kazini, sema, umeshatoka kazini au umesharudi kutoka kazini
4. Usiseme, alikuja siku ya Jumapili, sema alikuja Jumapili, kwa sababu inajulikana Jumapili ni siku.
5. Usiseme shati jingine, sema shati lingine.
Naomba kuwasilisha.
Last edited: