Matukio muhimu yanapuuzwa,nani alaumiwe?

Matukio muhimu yanapuuzwa,nani alaumiwe?

Gesi Kwanza

Member
Joined
Feb 16, 2013
Posts
14
Reaction score
1
Wakati mvua kubwa ikiwa imeanza kunyesha maeneo mbalimbali hapa nchini kuna matukio yaa kutokea maafa maeneo tofauti yakiwemo kuharibika miundombinu na vifo.Tukio lililotokea eneo ambalo nilikuwepo jana J4 asb ni kijiji cha Kibaoni-Mgeta wilayani Mvomero.Mwanaume mmoja amekutwa amenasa mtoni baada ya kusombwa na maji ya mto Mzinga kijijini hapo.Hadi natoka eneo la tukio polisi walifuatwa kuja kuchunguza maiti na kutoa uamuzi wa kuitoa.
Nimeshangazwa kutosikia chombo chochote cha habari(hata hivi vya mjini MOROGORO)kikiripoti maafa hayo na kutoa tahadhari kwa wananchi ili wawe makini ktk maeneo hatarishi.Najiuliza viongozi wa serikali,diwani,mwenyekiti,katibu,polisi n.k kwanini hawatoi taarifa kama hizi lakini likifanyika tukio fulani la kipuuzi tu la kichama(mfano;kufungua shina la wakereketwa) basi mhusika atakuja na waandishi wa habari ili waripoti,lkn haya nyeti hakuna anaejali.Kwanini? uzembe au kutowajibika au dharau au nini hasa?:lock1:
 
kiongozi
habari zimekuwa nyingi sana, kiasi kwamba wanachagua, hao wanaochagua za kuzitangaza nao wanaangalia zipi kwa mujibu wa wao au wanaowalipa kuwa zina tija.

hata waandishi wakati mwingine wakiona habari ambayo haitakuwa na maslai kwao au wakubwa wao huwa pia hawatoi matukio ya "muhimu"
 
Back
Top Bottom