Matukio ktk picha - chadema

Matukio ktk picha - chadema

ilboru1995

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2007
Posts
2,329
Reaction score
269
Kumekuwa na ufisadi mkubwa unaofanywa na vyombo vya habari kwa kuipendelea CCM hususan wakati huu wa kampeni. hivi karibuni mimi binafsi nilisitisha kusikiliza Clauds FM kutokana na wao kubadili mwelekeo, utashi na misingi waliojiwekea hapo nyuma uliokuwa unalenga kuelimisha umma na kufikisha kero za wananchi kwa walengwa.
bila ya kupoteza mantiki ya hoja yangu, naomba nikiri kuwa chama pekee kinachoonyesha utashi wa kweli wa kuikomboa nchi yetu ktk lindi la umaskini, ufisadi ktk kila nyanja za kiuchumi ni chadema. hivyo basi; 1. nawaombeni wanabodi muwe mnatuwekea habari picha zinazohusu kampeni za Chadema 2. chadema wenyewe nao wafanye jitihada za kipekee kuweza kutuhabarisha yanayojiri katika kampeni zao kupitia tovuti yao Tovuti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)

Nawasilisha
Ndimi mtaka mabadiliko chanya.
 
Wadau tafadhali tuwekeeni picha.. siku ya pili leo sijaona matukio ya kampeni za chadema kwenye luninga... hata ITV nayo haionyeshi kampeni za chadema....
 
Wanabania tu
safari hii hata marais wastaafu wanaona ngoma nzito wamejiweka pembeni
wacha dogo ajichakachue ajibu hoja zake mwenyewe.
Ila kwa msaada wa waandishi mafisadi bado Tanzania itabakia nyuma sana kwa kumchangua KIKWETE tena
 
Nasikia mapokezi ya Slaa ktk mji wa Moshi yamevunja record... Mkuu invisible tafadhali tujuze kwa habari picha...
 
Wanabania tu
safari hii hata marais wastaafu wanaona ngoma nzito wamejiweka pembeni
wacha dogo ajichakachue ajibu hoja zake mwenyewe.
Ila kwa msaada wa waandishi mafisadi bado Tanzania itabakia nyuma sana kwa kumchangua KIKWETE tena

Hao marais wastaafu hawawezi kumpigia debe, kwani kufanya hivyo ni sawa kutembea kwenye eneo la mabomu ya kutegwa ardhini - Mwinyi ndiye aliyeanzisha ununuzi wa radar, mkapa ndiye aliyeruhusu EPA, Kiwira, Mama Anna kuchukua NBC Holdings n.k.
 
Mimi sikutegemea KAMA HATA UraIS ccmWATAMWAGA CHINI NA CHADEMA..KWA KAMPENI NILIZOZIONA JANA MOSHI...ccm BYE BYE...NA WAKIJARIBU KUIBA KURA MARA HII WAJUE YALIYOTOKEA KENYA YATATOKEA TANZANIA. ILA WASIWASI WANGU NI KUHUSU HAO WASIMAMIZI WA KURA ZA VYAMA VYA UPINZANI NA UMASKINI WALIO NAO NA SISIEM WALIVYO NA PESA ZA KUMNUA NUA HATA GAVAN AWA BOT NACHELEA KUSEMA TUTARUDI KULE KULE KWA 1995(YALIYOMKUTA MHESHIMIWA NDUMILAKUWILI LYAYATONGOLI MREEHEMA)
 
yah website inafunguka ila upande wa picha inaleta 500 internal server error
 
Back
Top Bottom