Watu wana ajira zao bado wanakuja kweny usaili wa TRA? Jibu ni kwamba kutokana na baadhi ya maafisa wa TRA kupata utajiri wa harakaharaka kwa njia za rushwa na ufisadi na jamii kuona ni jambo la kawaida kwa mtu wa TRA kupata utajiri wa haraka bila kuhoji wala kuchukia anachokifanya, tena jamii ndo inamsifia kuwa ni mjanja. Hapa ndo tulipofika kuona kila kijana anataka kuingia TRA hata kama huko aliko ana mshahara mzuri kushinda hata huo wa TRA atakaopewa, bali nia na dhamira yake akaibe, ale rushwa naye apate utajiri wa haraka bila ya kufanya kazi kwa juhudi na maarifa. Sio vijana wote ila wengi wao hiyo ndo dream. Hapa ndo tulipofikia tukaipenda Rushwa, na ndiyo maana leo wengi wetu hatushangai hilo nyomi la vijana wenye ajira na bado wanakuja kweny usaili wa TRA.