Matokeo ya Darasa la Saba yatangazwa rasmi

Neiwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
728
633
Wakuu,

Leo tuangalie upande wa shule za Msingi, matokeo kutupa picha ya mwelekeo wa elimu kama unazidi kudorola ama kuna matumaini ya kunyooka.


Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) Dk Charles Msonde akionyesha moja ya karatasi za majibu ya mtihani wa darasa la saba kwa waandishi wahabari Dar es Salaam jana, wakati wa kutangaza matokeo ya mtihani huo wa mwaka huu.



Source: Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 - wavuti.com


 
Kulikuwa na fununu kuwa matokeo yalikuwa mabaya sana......sasa kama wameamua kuwapeleka hata wasiojua kusoma secondary ili kuepuka aibu ya 0MR itajulikana tu.....
 
Na hiyo multiple choice questions hata kwenye Hisabati, watakuwa wamefaulu wabahatishaji
 
Na hiyo multiple choice questions hata kwenye Hisabati, watakuwa wamefaulu wabahatishaji

Mkuu hata UDSM siku hizi nasikia eti kuna multiple choice sasa kwa primary si ndiyo kabisa? Multiple Choice kwa hesabu sikuwahi kuiona!!!! enzi zetu? Ndiyo maana graduate ukimwambia akuandikie report ni bora ukae mwenyewe uandike utamaliza haraka zaidi kuliko kusahihisha document mpaka inabidi upate kikombe cha kahawa!!
 
Leo Waziri wa Elimu,Shukuru Kawambwa ametangaza rasmi maotokeo na kueleza kuwa kiwango cha ufaulu kwa mwaka huu kimeongezeka. Amesemawaliofaulu ni sawa na asilimia 64 ya wanafunzi walioandika paper ya D7 mwaka huu

Hongera madogo wote mliofaulu wazazi wawaandae kuanza shule Za sekondari january 2013
 
 
Watoto wao wanasoma nje kwenye shule bora na za ndani wanaziua ili watoto wao waje kuwatawala watoto wenu

na huku ndiko tunakoelekea jamani inasikitisha sanasana si unawaona watoto wa MAKAMBA wewe
 
Wamechakachua weee..wamekuja na mbinu hii ya kuongezeka kiwango cha ufaulu,laiti script zingekuwa zinarudi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…