Mzee
Mohamed Said historia ya ANC kuanzia kuanzishwa kwake na harakati nzima za mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika ya Kusini ziko well documented na zinasisimua sana
Utapata kuona uzalendo, kujitolea na kuhatarisha maisha kwa ajili ya heshima ya watu wao na taifa lao kutoka kwa akina Giovani Mbeki(baba yake Thabu Mbeki), Oli Tambo(kama Oliver Tamba alivyokua akiitwa na makomred wenzake), Walter Sisulu na Ahmed Kathrandu
Walikuwepo kina mama kama Florence Matomela, Mama Nomzane Winnie Medikizela (Winnie Mandela) na wanaharakati wengi wake kwa waume na hata viongozi wa vyama vya wafanyakazi chini ya COSATU
Sidhani kama kuna historia ya harakati za kupambania uhuru na haki katika nchi iliyohifadhiwa vizuri na kubakia salama mpaka sasa kama ya Afrika ya Kusini
Ukiisoma ukiisoma utakutana na watu walikua na misimamo mikali sana dhidi ya ubaguzi wa rangi kuliko Nelson Mandela
Walikuwemo kina Chris Honey, Steve Bantu Biko na wengine wengi. Hata Mama Winnie alikua mtu wa misimamo mikali sana tena wakati huo mumewe yupo gerezani
Nakumbuka hata baada ya ANC kushika dola na ilipoundwa tume ya ukweli na maridhiano zilitumika nguvu za ziada kumshawishi Winnie akubali kuomba radhi kwa aliyoyafanya dhidi ya waliokua wapinga harakati za kupinga siasa, sheria na sera za Apartheid
Kuna wakati Nelson Mandela baada ya kua ametoka gerezani alisema akiwa ziarani nchini Sweden kua lolote analosema Oli Tambo(wakati huo Baba Tambo akiwa Mwenyekiti wa ANC) ndio msimamo wake yeye Mandela na hakika anamuelezea Baba Tambo kua ni kiongozi mahiri kwelikweli
Kwa kifupi wametajwa watu wengi na ushiriki wa kila mmoja katika mapambano ya kudai haki zao na historia imehifadhiwa vyema
Katika nchi za Afrika Mashariki( Angalau Kenya Uganda na Tanganyika kuna kasoro hiyo. Harakati zao za kupigania uhuru wa nchi zao zimerekodi na kuwatambua watu wachache sana ambao walikuaja kua viongozi wakuu wa nchi hizo
Tena angalau Kenya na harakati za MauMau unakutana na watu wengi zaidi yaani kina Dedan Kimathi, General Mathenge na wengine wengi na vitabu vimeandikwa juu yao. Japo Jomo Kenya ndio alikua kinara lakini wametajwa watu waliopambana kwa machozi jasho na damu
Zanzibar pengine sababu ya udogo wa nchi yao oral tradition imesaidia ku preserve utajiri wa historia yao kabda, wakati na baada ya mapinduzi
Wito wangu tusome. Tusome kila kila kitu na tusijifunge kwenye box.
Tusome historia rasmi ya nchi yetu kama inavyo fundishwa shuleni, tusome historia kama ilivyo andikwa na watu wengine kama Joseph Mihangwa, Mohamed Said, Pius Msekwa na hata kina Mohsi Ali Baruani (au Ali Muhsin Baruan) kwa Zanzibar na wengine wengi
AIdha masimulizi ya mdomo kwa watu walio iishi historia yenyewe ni vyanzo muhimu vya kujua historia zetu. Tutakapo jielewesha na kujua zaidi tutakua katika nafasi nzuri ya kuhakiki, kukubali au kukosoa