Matatizo ya maji Dar es Salaam yataisha lini?

Matatizo ya maji Dar es Salaam yataisha lini?

Kwa kweli haya mambo yanaumiza sana,cha ajabu majoritty ya wananchi wa Dar es salaam uwaga wanakaa kimya kabisa na kuridhika na hali hizi!shida ya maji toka last week kwa Dar ni kubwa,na kuna uwezekano wa kutokea mlipuko wa magonjwa!

Hivi mwenye dhamana mbona hasikiki au naye anaumwa kama Ndugai?
 
Ni siku ya tano mfululizo sasa maeneo kadhaa wa kadhaa ya jiji la Dar es laam yamekua kavu bila huduma ya maji kupatikana,na kinachokera zaidi mamlaka husika zimekuwa kimya kabisa bila kutoa tamko wala tangazo lolote juu ya tatizo ilo!

Viongozi wetu nao na wawakilishi wetu wamekaa kimya kabisa kama vile wananchi wao hawana adha yeyote,na hii yote inatokana na kua wao na family zao hawaathiriki lolote juu ya matatizo haya!

Uwa najiuliza sana hivi ni lini jiji ili litakua na huduma za maji na umeme za uhakika? maana sasa hivi mbali ya maji huduma ya umeme nayi kwa maeneo mengi kama Kimara,Boko,Ubungo,Mtongani na maeneo mengine imekua ni kama mchezo wa bahati nasibu!

Hivi hawa tuliowapa dhamana ya kutuongoza ni lini watalitendea haki taifa ili na kuthamini na kuzitendea haki hizi kodi zetu lukuki wanazokusanya na kuzinyonya bila huruma?

dar es salaam ni sehemu ambayo ccm ilishinda kwa kishindo so wanajua wanaweza kufanya chochote hao viongoz kwa kuwa wanakubalika kufunga maji bila taarifa na sijui wanafikiliaje watu kukosa maji kwa mji wa dar inakuwaje na wingi wa watu je hao watu waliwatoni wanaendaje sio watoe tamko hapo wachomoke wezi waliopo dawasco matamko ni mengi yashatolewa.
 
Hivi mwenye dhamana mbona hasikiki au naye anaumwa kama Ndugai?

Kwa kweli hawa watu wanatudharau sana mkuu,mwenye dhamana apige kelele za nini wakati yeye,family yake na wenye dhamana wenzake hawapati athari yoyote?sana sana atarudi tena kua mnyenyekevu kipindi cha kuomba kura!matatizo yetu hayatakwisha na tutaendelea kua walalamikaji kama tutaendelea kuwakumbatia hawa wanaotujali kipindi cha kampeni tu,na kutu laghai kama mazuzu vile!
 
Jamani mwenye mawasiliano ya mawaziri husika,katibu au hata Dawasco tunaomba atuwekee hapa,jambo linazidi kuwa worse,ni bora kukosa umeme kuliko maji,week ya pili sasa inakwenda huku Mbezi watu hatuna maji kabisa na hatujuhi lini yatapatikana!
 
Nilishawahi kuandika humu juu ya hawa maprofesa kupewa uwaziri. Hakuna kwa hakika wizara iliyowahi na hata inayoongozwa na profesa ikafanya kazi kwa uhakika. Huyo Maghembe na Makala (mzee wa vijana jazz) ni mizigo ya kufa mtu hata mnyamwezi hawezi kuibeba. Sijui wanawaza nini kwa nchi yenye vyanzo lukuki vya maji kukosa maji. Ni aibu kwa uprofesa wake kutokuwa creative ili kusolve tatizo.
Isitoshe, ccm wanatoa huduma za msingi kama rushwa hasa kwa maeneo wanayoongoza na yale ya upinzani. Na wananchi tujiulize, ni lini huduma za jamii zitaimarika ili tupate nafasi ya kufanya maendeleo? Tutafakari tena iwapo ccm inahitajika kuchagiza maendeleo kwa sasa.
 
Nilishawahi kuandika humu juu ya hawa maprofesa kupewa uwaziri. Hakuna kwa hakika wizara iliyowahi na hata inayoongozwa na profesa ikafanya kazi kwa uhakika. Huyo Maghembe na Makala (mzee wa vijana jazz) ni mizigo ya kufa mtu hata mnyamwezi hawezi kuibeba. Sijui wanawaza nini kwa nchi yenye vyanzo lukuki vya maji kukosa maji. Ni aibu kwa uprofesa wake kutokuwa creative ili kusolve tatizo.
Isitoshe, ccm wanatoa huduma za msingi kama rushwa hasa kwa maeneo wanayoongoza na yale ya upinzani. Na wananchi tujiulize, ni lini huduma za jamii zitaimarika ili tupate nafasi ya kufanya maendeleo? Tutafakari tena iwapo ccm inahitajika kuchagiza maendeleo kwa sasa.

Ni kweli kabisa mkuu,ilikua wrong kufikiria na kuamini kua maprofesa wanapopewa uwaziri watakua msaada na ufumbuzi wa matatizo yetu lukuki,hawa watu ni mizigo katika wizara zao husika,walitakiwa wafanye vitu vingine zaidi ya siasa!Tanzania ni moja ya nchi chache kabisa duniani zinatokumatia nadharia ya kua maprofesa wakipewa uongozi wa nafasi za kisiasa basi wata deliver!
 
Kila Mtu tz ana ndoto za kuishi Dar
Jiji limefurika kila kona,huduma za Maji na umeme lazima ziwe za wasiwasi
Kila siku makundi kwa makundi ya watu wanahamia Dar!!
 
Ngoja wakazi wa dsm mkome maana mnakera kwa uzuzu ccm washinda kwa kishindo why msiemde lumumba kutoa hizo hoja za maji..
 
Kila Mtu tz ana ndoto za kuishi Dar
Jiji limefurika kila kona,huduma za Maji na umeme lazima ziwe za wasiwasi
Kila siku makundi kwa makundi ya watu wanahamia Dar!!

Why do people leave their places and go to.DSM? There must be problems where they come from. The Government should address these problems. I am sure even in the areas where these people come.from water problem.is the same. The Government is on leave. Period. Nitajie waziri au katibu mkuu mwenye shida ya maji.
 
Kila Mtu tz ana ndoto za kuishi Dar
Jiji limefurika kila kona,huduma za Maji na umeme lazima ziwe za wasiwasi
Kila siku makundi kwa makundi ya watu wanahamia Dar!!

Muda mwingine serikali inapaswa kulaumiwa,maana kila kitu wao wanaelekeza Dar,ni kama vile hatuna viongozi wenye vission,viwanda vyote Dar,kila kitu Dar,unafuu ungekuwepo mikoani nani angahika na karaha hizi za Dar?kumbuka Morogoro kulikua na viwanda vingi sana enzi za Mwl Nyerere,ila vyote nadiriki kusema kwa makusudi kabisa baadhi ya viongozi waliviua viwanda hivi huku serikali ya ccm ikiangalia tu!
 
mi nadhani yataisha siku watu watakapoacha kukimbilia mji na kujazana
 
mi nadhani yataisha siku watu watakapoacha kukimbilia mji na kujazana

Ilo suala halitokuja kwisha mkuu,inachotakiwa ni serikali kuboresha miondombinu na huduma kwy majiji huku pia ikijaribu kujenga vyanzo vya uchumi huko mikoani ili kupunguza wimbi la kukimbilia Dar lakini si kusema kuua ilo jambo litakuja kwisha kabisa
 
Back
Top Bottom