Matatizo: Je, ni uthibitisho wa kutokuwepo kwa Mungu?

Sang'udi

JF-Expert Member
May 16, 2016
8,291
19,185
Habari za wakati huu!

Katika maisha, kumekuwa na nyakati ambapo tunawaza na kuwa na wasiwasi juu ya uwepo wa Mungu. Uwepo wa matatizo mbalimbali kama matatizo ya kiuchumi, matatizo ya kiafya, matatizo ya kijamii, matatizo ya kisiasa, n.k. umechangia kwa kiasi kikubwa hali hii.

Ukweli mchungu, ni kuwa; Mwenyezi Mungu alipoiumba dunia, aliweka utaratibu wake ambao ulikuwa mwema kabisa. Akatutaka tuishi kwa upendo ili kuendeleza uzuri huu wa dunia.

Kwahiyo, matatizo haya yanadhihirisha uwepo wa Mungu na wakati huohuo kutukumbusha kuwa ili tuishi kwa wema na amani, tunapaswa kufuata utaratibu wake sahihi, tupendane.

Sio wakati wote tunapopata matatizo ni kwa sababu tumekosea au tumeshindwa kufuata utaratibu. La, wakati mwingine tunapitia majaribu ili Mwenyezi Mungu aweze kupata sifa na utukufu.

Tujitahidi kudumu kwa Mwenyezi Mungu wakati wote. Hatutakuwa na vita, ugomvi wala mlipuko wa magonjwa mbalimbali. Na hata tukiwa nayo, au pale majanga ya asili yanapotokea, tutakuwa na nguvu na uwezo wa kuyastahimili huku tukibaki kuwa waaminifu kwa Mungu.

Wasalaam!
 
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Ni fictionsl character, katungea na watu.

Ulimwengu huu unakanusha kuwepo kwake.

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Ni fictionsl character, katungea na watu.

Ulimwengu huu unakanusha kuwepo kwake.

Sent from my typewriter using Tapatalk
Uwepo wa ulimwengu unadhihirisha kuwa Mungu yupo; anajua yote, anaweza yote, na Yeye ndio Upendo.
 
Uwepo wa ulimwengu unadhihirisha kuwa Mungu yupo; anajua yote, anaweza yote, na Yeye ndio Upendo.
Kivipi, nyambulisha hoja yako hatua kwa hatua, kwa mifano hai, yenye mantiki, inayothibitishika bila kuweza kupingika.
 
Kivipi, nyambulisha hoja yako hatua kwa hatua, kwa mifano hai, yenye mantiki, inayothibitishika bila kuweza kupingika.
Haiwezekani tu kuwa ulimwengu ulijikuta upo wenyewe, sio? Lazima kitakuwa na chanzo (origin) chake.

Wewe, kwa mfano, haukujikuta tu upo. Ulizaliwa kutoka kwa wazazi wako, ambao walizaliwa na wazazi wao. Chain hiyo utaendelea hadi kufikia sehemu tutapata wazazi wa kwanza kabisa.

Sasa, hao nao lazima wawe na chanzo ambacho kilichowaumba ambacho hakikuumbwa. Hicho chanzo, ndio Mungu.
 
Kivipi, nyambulisha hoja yako hatua kwa hatua, kwa mifano hai, yenye mantiki, inayothibitishika bila kuweza kupingika.
Lakini pia, kila kitu hai ni matokeo ya movements.

Hizi movements zinakuwa controlled na kitu kingine externally. Ukiifuata hiyo chain, mwisho wa siku utakuta kuna chanzo kimoja kinachozi-control ambacho hakiwi-controlled.

Hicho chanzo ndio Mungu mwenyewe. Kwahiyo vyote vilivyomo ulimwenguni, vinathibitisha uwepo wa Mungu.
 
Lakini pia, kila kitu hai ni matokeo ya movements.

Hizi movements zinakuwa controlled na kitu kingine externally. Ukiifuata hiyo chain, mwisho wa siku utakuta kuna chanzo kimoja kinachozi-control ambacho hakiwi-controlled.

Hii ni assumption, unawezaje kuhakikisha hili? Unaelewa habari nzima ya mwanzo na mwisho inatokana na udogo wa mawazo yetu na umasikini wa uzoefu wetu?

Unaelewa kwamba katika quantum physics ukizama sana, muda unapotea, mambo yanaweza kuwa hayana muda, na chanzo kinaweza kuja baada ya matokeo (the cause appearing after the effect, instead of the cause causing the effect?

Hicho chanzo ndio Mungu mwenyewe. Kwahiyo vyote vilivyomo ulimwenguni, vinathibitisha uwepo wa Mungu.

Kwa hiyo kama chanzo ni nothingness, non existence, Mungu ni nothingness?
 
Haiwezekani tu kuwa ulimwengu ulijikuta upo wenyewe, sio? Lazima kitakuwa na chanzo (origin) chake.

Wewe, kwa mfano, haukujikuta tu upo. Ulizaliwa kutoka kwa wazazi wako, ambao walizaliwa na wazazi wao. Chain hiyo utaendelea hadi kufikia sehemu tutapata wazazi wa kwanza kabisa.

Sasa, hao nao lazima wawe na chanzo ambacho kilichowaumba ambacho hakikuumbwa. Hicho chanzo, ndio Mungu.
Dhana nzima ya muda, ambayo inazaa dhana ya chanzo na cha badaye, ni dhana inayotokana na kutoelewa ulimwengu ulivyo complex.

Kwa mfano, ukiiangalia dunia kutoka jicho la mshale wa mwanga (photon), dunia inakuwa haina muda unaoendelea, haina past, haina future, past na future zote zimeunganishwa katika present.

Kwa sababu photons zinasafiri kwa speed of light.

Fundamentally, time is not real, it is a manifestation of limitations in speed and relative movement.

Ukisoma Einstein's Relativity utaona hilo.

So why do you treat time as fundamentally real and important?
 
Hii ni assumption, unawezaje kuhakikisha hili? Unaelewa habari nzima ya mwanzo na mwisho inatokana na udogo wa mawazo yetu na umasikini wa uzoefu wetu?

Unaelewa kwamba katika quantum physics ukizama sana, muda unapotea, mambo yanaweza kuwa hayana muda, na chanzo kinaweza kuja baada ya matokeo (the cause appearing after the effect, instead of the cause causing the effect?



Kwa hiyo kama chanzo ni nothingness, non existence, Mungu ni nothingness?
Tuachane na quantum Physics, hata mimi nina theory zangu sijazi-publish, one day I will.

Tutumie simple logic tu. Babu yake na Babu yako alishawahi ku-exist? Kama ni ndio, unathibitisha vipi?

Nikikuambia kuwa ni fictions tu utapinga?
 
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Ni fictionsl character, katungea na watu.

Ulimwengu huu unakanusha kuwepo kwake.

Sent from my typewriter using Tapatalk
Ulimwengu ndo unathibitisha kuwepo kwa Mungu.

Nadharia ya kusema kuwa Mungu mwenye upendo wote inamaana gani na umeipata wapi ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dhana nzima ya muda, ambayo inazaa dhana ya chanzo na cha badaye, ni dhana inayotokana na kutoelewa ulimwengu ulivyo complex.

Kwa mfano, ukiiangalia dunia kutoka jicho la mshale wa mwanga (photon), dunia inakuwa haina muda unaoendelea, haina past, haina future, past na future zote zimeunganishwa katika present.

Kwa sababu photons zinasafiri kwa speed of light.

Fundamentally, time is not real, it is a manifestation of limitations in speed and relative movement.

Ukisoma Einstein's Relativity utaona hilo.

So why do you treat time as fundamentally real and important?
Existence ya time inakuja kuwa proved na theory yangu ya air kama source ya energy and everything. Hiyo air pia source yake ni Mungu.

Kwa maelezo yako hayo movement ya hizo photons na photons zenyewe zinamtegemea Mungu.
 
Back
Top Bottom