Matangazo kwenye Jamii forum

Matangazo kwenye Jamii forum

Mlima meru

Senior Member
Joined
Dec 30, 2012
Posts
114
Reaction score
20
Wapendwa wa jamii forum,
Naona watu wengi wanaweka matangazo hapa kwa Jf ila zaidi ya 80% hawajui nini kinatakiwa kujumuishwa ili uweze kuuza bidhaa yako.
Kama upo serious kuuza chochote zingatia yafuatayo;
1. Jina la bidhaa
2. Ipo kwenye hali gani (ubora) na kama ni mpya au used.
3. Jitahidi kuelezea bidhaa yako japo kidogo kwani sio wote wanafaham vitu mf. Nauza vaseline lotion, haina harufu, inafaa kutumiwa na aina zote za ngozi japo wanaume wanaitumia zaidi.nk
4. Weka picha kama unazo
5. Weka bei (rasmi au hata ya kuanzia)
6. Kama ni bidhaa kama gari onesha Kilometa zilizotembea, ukubwa wa Engine (CC) na pengine mwaka (japo sio muhimu sana) na kama inadaiwa kodi za serikali.
7. Andika unapatikana wapi na kama watu wa mikoani wakitaka kununua wataipataje bidhaa yako
8. Weka mawasiliano (yaliyo rasmi na sio namba za simu ambazo hazipatikani)

NB: Najua katika selling techniques hatushauriwi kutanguliza bei katika bidhaa, ila hapa ni Gulio hivyo bei ni muhimu sana.

Wengi wanauza bidhaa zao hapa kwa urahisi kabisa wakati wengine ukisoma tangazo lake hapa unabaki kumuhurumia kwani...unaona kabisa amepoteza muda wake kwani hawezi pata mteja.
Kazi kwenu!
 
Mimi nimeshuhudia wengi walioweka matangazo yanayo jitosheleza wakiuza ndani ya siku moja ...hivyo kama ulipata critics nakushauri uzingatie vigezo hapo juu halafu toa tena tangazo.
Ie. Critics zinakuwa nyingi kwani matangazo hayajitoshelezi...
 
Mimi nimeshuhudia wengi walioweka matangazo yanayo jitosheleza wakiuza ndani ya siku moja ...hivyo kama ulipata critics nakushauri uzingatie vigezo hapo juu halafu toa tena tangazo.
Ie. Critics zinakuwa nyingi kwani matangazo hayajitoshelezi...

96% of all ads. here are crticized au watu wanakua wanaleta utani tu bana au we mgeni
 
Kumbuka hii jamii forum inao pia vijana wa shule ambao kila kitu wanafanya ni mchezo ILA ukweli unabaki pale pale kuwa
Critics nyingi zinatokana ...na mapungufu yaliyoko kwenye Tangazo

Mf: Mtu Anandika nauza Laptop ya Toshiba, 500gb na 1gb ram. Bei maelewano. mawasiliano 0713XXXXXXX
Unategemea atauza hapo?...kama sio kejeli tu atapata
 
Kumbuka hii jamii forum inao pia vijana wa shule ambao kila kitu wanafanya ni mchezo ILA ukweli unabaki pale pale kuwa
Critics nyingi zinatokana ...na mapungufu yaliyoko kwenye Tangazo

Mf: Mtu Anandika nauza Laptop ya Toshiba, 500gb na 1gb ram. Bei maelewano. mawasiliano 0713XXXXXXX
Unategemea atauza hapo?...kama sio kejeli tu atapata

Sio that hazijajitosheleza kuna nyingine watu wana crticize tu ili kuannoy watu kama. kuna cku jamaa alikua anauza modem ya airtel iliyochakachuliwa basi kuna bmtu akaja akaanza kusema acha njaa we dogo na fujo nyingine nyingi sa hiyo ndo nn
 
Mimi nimepata simu nzuri mno kuwahi kuwa nayo katika maisha yangu kupitia jukwaa hili
 
Forum ya hii imejaa critics kuliko buyer au dealers
Si kweli kaka hapa ndio soko kubwa ,mimi ni mmoja kati ya wanunuzi wakubwa wa vitu kupitia hii forum,nimewajua watu wengi pia ambao huuza na kununua vitu kupitia forum hii,tatizo wauzaji wengi huweka matangazo hasi,yaani hawaweki bei au model,hata ukipiga hizo simu zao walizoweka hawapatikani,wengine mkiahidiana mkutane sehemu mumalizane hawafiki.
 
Back
Top Bottom